ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 25, 2016

KOCHA LWANDAM AONDOKA NCHINI BILA KUSAINI MKATABA YANGA.

Kocha George Lwandamina amemalizana na Yanga kwa maana ya mazungumzo lakini amerejea nchini mwao bila ya kusaini mkataba na Yanga.

Kocha huyo ameondoka nchini leo alfajiri kurejea Lusaka Zambia kwa ajili ya kumalizia mambo ya kifamilia.

“Baada ya hapo atarejea na kusaini mkataba, utakuwa ni wa miaka miwili nimeelezwa,” kilisema chanzo.

Lwandamina ndiye anatarajiwa kuchukua nafasi ya Kocha Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi.

Kocha huyo wa zamani wa Zesco, alitua nchini juzi na kufanya mazungumzo na uongozi wa Yanga.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.