ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 1, 2016

HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA MWANZA, WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA KAWAIDA WA ROBO MWAKA WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU (JMAT) TAREHE 01 OKTOBA, 2016 MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella, akifunngua Mkutano wa Robo Mwaka wa Chama cha Majaji na Mahakimu JMAT, tawi la Mwanza na Geita, unaofanyika leo kwenye ukumbi wa jengo la NSSF Jijini Mwanza.

HOTUBA YA MHESHIMIWA JOHN V.K.MONGELLA, MKUU WA MKOA WA MWANZA,WAKATI  WA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUUWA KAWAIDA WA ROBO MWAKA WA CHAMA CHAMAJAJI NA MAHAKIMU (JMAT) TAREHE 01 OKTOBA, 2016MWANZA

Mheshimiwa Robert Vicent Makaramba, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Mheshimiwa Francis Kishenyi, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Mkoa wa Mwanza (JMAT), Mheshimiwa Bittony Mwakisu, Katibu wa Chama cha Majaji na Mahakimu Mkoa wa Mwanza (JMAT),

 Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza,Mheshimiwa Francis Kabwe, Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mwanza,Wajumbe wa Kamati Tendaji wa Chama cha Majaji na Mahakimu Mkoa wa Mwanza (JMAT), 

1Waheshimiwa Mahakimu wote wa Mkoa wa Mwanza na Geita, Wanachama wote wa Chama cha Majaji na Mahakimu Mkoa wa Mwanza na Geita (JMAT),Ndugu wageni waalikwa, Wanahabari, mabibi na mabwana.Naomba  kwanza  nitoe  shukrani  zangu  za  dhati
kwako,  Mhe. 
Jaji Mfawidhi Kanda ya Ziwa, Mhe.Robert Makaramba, akichangia wakati wa maswali na majibu ndani ya mkutano huo.

   Jaji  Mfawidhi,  kwa  kunialika  kujakushirikiana  nanyi  katika  mkutano  huu  muhimu.  Nifursa  ya  pekee  kwangu kukutana  nanyi,  WaheshimiwaMajaji   na   Mahakimu  na  wadau  wote  wa    sekta    yasheria.  Asanteni sana.

Kwa  sasa  niruhusuni  nisimame  mbele  yenu  kwaunyenyekevu mkubwa kwa kazi ambayo nitaifanya hivipundeNimearifiwa kuwa  maudhui ya mkutano huu ni kujadilimaadili ya kazi za waheshimiwa majaji na waheshimiwamahakimu  kama njia  bora ya kuboresha utendaji kaziwa Mahakama na Utendaji haki.

 Nafurahi  kufahamu  kuwa  mkutano   kama   huuunafanyika  kila   robo   mwaka  kwa  nia  ya  kujitathmini.Nafahamu  kuwa  pamoja  na mkutano  huu,  Mahakamahuwa  inafanya  mikutano  mingine  kama  vile  Baraza  laWafanyakazi  na    ya    watendaji    wa  Mahakama.

Mkutano  mnaofanyika  leo  na  mingine  ya  aina  yakeimeiwezesha  Mahakama  kuendelea  kujitathminiyenyewe kiutendaji. 
Wawasilishaji wa mada wakiongozwa na muongoza mjadala Jaji Rose Ebrahim (katikati)
Muwasilishaji kutoka NSSF.
Katubu wa JMAT MWANZA Mhe. BITTONY MWAKISU  (kulia) akiongoza sekretarieti katika mkutano huo. pembeni yake ni  Mhe DENICE MLASHANI kutoka Sengerema.

2Nitoe  rai  kwa  mhimili  huu  kuimarisha  utaratibu  huukwani ni wa pekee. Kwa taasisi nyeti na muhimu kamaya  kwenu  kujitathmini  ni  nyenzo  kuu  ya  kuboreshautendaji.Waheshimiwa Majaji na Mahakimu,        Mihimili  yote  ya  dola  yaani  Serikali,  Bunge  naMahakama   inapata  mamlaka  yake  kutoka  kwawananchi  kupitia  Katiba.  

Hivyo  siku  zote  inatarajiwakwamba katika utekelezaji wa majukumu yake mihimilihii  itazingatia maslahi  ya  wananchi,  Katiba  na  sheriaza nchi. 

Mahakama, kama  zilivyo  nguzo  nyingine  za  dola,  inawajibu  mkubwa  wa  kuhakikisha  kwamba  inaelekezajuhudi  zake  zote  katika  kuwahudumia  wananchi  kwaufanisi  na  kwa  wakati. 






 Ninyi   mnafahamu  wazi  kuwahaki  ni  eneo  muhimu  la  utawala  wa   sheria,  ni  eneo
linalogusa  uhai  na  ustawi  wa  jamii,  na  ni   eneolinalogusa  utulivu  na  utangamano  wa  Taifa.  Hivyoutendaji  wa Mahakama una  mchango wa  pekee katikataifa letu.

Ili  kuhakikisha  kwamba  Mahakama  inatimizawajibu  huu  bila  hofu  wala  huba,  katika  nchi  nyingi, ikiwemo  nchi  yetu,  imewekwa misingi  ya  kikatiba  nakisheria  ambayo   imezipa  Mahakama  uhuru  mkubwakatika  kuendesha  shughuli  zake  ikilinganishwa  namihimili mingine.

3Waheshimiwa Majaji na Mahakimu, Dhana  ya  upekee  wa  Mahakama  inatokana  nauhuru  unaotolewa  ili  kuuwezesha  mhimili  huukutekeleza  kazi  zake  bila  kubanwa  na  mifumo  yakawaida  ya  upimaji  inayotumiwa  na  taasisi  nyingine.Ni  wazi,  hata  hivyo,  kwamba  uhuru  huu  una  mipakayake.  Kwani  vipo  vyombo  vya kisheria    vya   kufuatiliamwenendo  na  nidhamu  ya watoa haki: mahakimu namajaji.

    Pamoja  na  ukweli  huu,  utaratibu  waMahakama  kupimwa  ni   wa    aina  yake.  Ni  vigumukwa  watu  wa  kawaida  kuujua  au  kuuona  unavyofanyakazi.

  Tofauti  na  nguzo  nyingine  za  dola,   imekuwarahisi,  kwa  mfano,  kwa  wabunge  kupimwa  na  wapigakura wao kila baada ya kipindi Fulani.

Sina  shaka  mpango  wenu  wa  kujitathminiutaiwezesha  Mahakama  kujiweka  karibu  sana  nawananchi  na  kujua  nini   matarajio  yao,  ili  nanyi  kwaupande  wenu  muone  namna  nzuri  ya  kutekeleza majukumu  yenu  kama  sehemu  ya  uwajibikaji  waMahakama kwa umma. Waheshimiwa Majaji na Mahakimu, Mwanzoni  mwa  hotuba  hii  nimezungumzia  uhuru  waMahakama.  


Kama    nilivyosema,  uhuru    waMahakama  ni  muhimu  sana  katika  upatikanani  haki,
kwani  Mahakama  ambayo  siyo  huru,  haiwezi  kutendahaki.  Kama  ninyi  wenyewe  wanasheria  mnavyosema:haki inatakiwa siyo  tu   itendeke,  bali  ionekaneinatendeka. 

4Kama  kuna  wasiwasi  wowote  ule  wa  jinsi  hakiinavyotolewa,  hasa  kutokana  na  tuhuma  za  kukosauadilifu,  basi  haki  haiwezi  kuchukuliwa  kama  kweliimetendeka.  Wajibu  wa  Mahakama  ni  kufanya  yotemawili:  kutenda  haki,  na  kufanya  haki  ionekaneimetendeka.Ni  matumaini yangu kwamba katika mkutano huupia   mtaendelea  kuyazungumza   masuala  ya  maadilikwa uwazi. 

Lakini msiishie hapa, napenda kutoa mwitokwamba   masuala  ya  maadili  katika  utendaji  waMahakama yawe yanaendelea kuwa ajenda ya kudumu.Waheshimiwa Majaji na Mahakimu,Nimefurahishwa  na  uamuzi  wenu  wakuwashirikisha katika mkutano huu wadau mbali mbaliwa  Mahakama na sekta  ya  sheria  kwa  ujumla ambaopia ni wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa. 

Waheshimiwa Majaji na Mahakimu,Nina  matumaini  kuwa  mkutano  huu  utakuwa  wamafanikio  siyo  tu  kwa  Mahakama bali  kwa  wananchiwa Mkoa wa Mwanza, Geita na taifa letu kwa ujumla.Nakutakieni majadiliano yenye  tija kwenu na kwa nchiyetu.

5Baada  ya  kusema  hayo  nafurahi  sasa  kutamka kuwaMkutano    huu    Mkuu    wa  kawaida wa robo  Mwaka wa   Majaji  na Mahakimu  wa Mkoa wa Mwanza na Geita umefunguliwa rasmi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.