ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 30, 2016

AIRTEL TANZANIA NA PUMA ENERGY WAUNDA USHIRIKA.

Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso (kulia) na Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti wakibadilishana mikataba mara baada ya kusaini makubaliano  rasmi ya  ushirikiano mpya ambao unawawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma zote za Puma Energy kwa kutumia kadi ya “Airtel Money Tap Tap” katika vituo vya mafuta vya PUMA nchini kote. Wakishuhudia (kushoto) Meneja Bidhaa wa Puma , Adam Sipe na Meneja Mauzo wa Airtel, Bi Bartleth Omari
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso (kulia) na Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti wakiwa katika picha ya pamoja  mara baada ya kusaini makubaliano  rasmi ya  ushirikiano mpya ambao unawawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma zote za Puma Energy kwa kutumia kadi ya “Airtel Money Tap Tap” katika vituo  vya mafuta vya PUMA nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso (kulia) na Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti wakisaini mkataba wa  makubaliano  rasmi ya  ushirikiano mpya ambao unawawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma zote za Puma Energy kwa kutumia kadi ya “Airtel Money Tap Tap” kwenye vituo vyao vya mafuta vya PUMA nchini. Wakishuhudia (kushoto) Meneja Bidhaa wa Puma , Adam Sipe na Meneja Mauzo wa Airtel, Bi Bartleth Omari
Meneja kitengo cha Airtel Money, Asupya Naligingwa, akitoa maelezo jinsi ya kuweka na kulipa mafuta kupitia kadi ya Airtel Tap Tap  wakati wa uzinduzi wa ushirika mpya kati ya Airtel na PUMA utakaowezesha wateja kulipia bidhaa na huduma zote za PUMA energy kwa kadi maalumu iliyounganishwa na huduma ya Airtel Money ya Tap Tap.  Pichani ni mpiga picha mkuu wa jambo leo,  Richard Mwaikenda akiwekewa mafuta na muhudumu wa kituo cha PUMA oyesterbay  kupitia huduma ya Airtel Tap Tap wakati wa uzinduzi huo
Meneja kitengo cha Airtel Money , Asupya Naligingwa akiongea na Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso (kulia) na Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti  mara baada ya uzinduzi wa huduma ya Airtel Tap Tap katika vituo vya puma
Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti   akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya Airtel na PUMA utakaowawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma za PUMA kupitia Airtel Money TapTap
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso  akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya Airtel na PUMA utakaowawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma za PUMA kupitia Airtel Money TapTap
 Airtel Tanzania na Puma Energy waunda ushirika.

  • Puma Energy kupokea malipo ya huduma zote na mafuta kupitia Airtel Money Tap Tap

Airtel Tanzania na Puma Energy Tanzania imezindua rasmi ushirikiano mpya ambao unawawezesha wateja kulipia bidhaa na huduma zote za Puma Energy kwa kutumia kadi ya “Airtel Money Tap Tap” kwenye vituo 46 nchini kote.

Ushirikiano huu sasa utawawezesha wateja wa Airtel na Puma Energy kulipia mafuta na bidhaa nyingine bila kutumia fedha taslimu bali watatumia kadi ya Airtel Tap Tap ambayo imeunganishwa na akaunti zao za Airtel Money.  Huduma hii ni salama na rahisi kutumia inapatikana katika vituo vyote vya Puma Energy nchi nzima,  Huduma ya Airtel Money Tap Tap inatekelezwa kwa awamu 2 ambapo awamu ya kwanza itahusu vituo vyote 20 vya Puma jijini Dar es Salaam na awamu ya pili ni kwa ajili ya vituo vya mikoani kuanzia mapema mwakani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ushirikiano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Bwn Sunil Colaso alisema “Sisi kama Airtel tunafuraha kuanzisha njia hii ya malipo tukishirikiana na kampuni ya Puma Energy Tanzania. Ushirika huu utaleta ushirikiano katika kutanua huduma zetu katika maeneo mengi zaidi na kutoa usalama na uhakika wa huduma bora zaidi kwa wateja wote wa Airtel na Puma Energy kwa masaa 24 na siku 7 za wiki

Tunaamini kuwa ushirika huu na Puma Energy utaongeza ufanisi na kubadilisha maisha ya jamii kuwa bora zaidi kwani wateja wetu wote wataweza kuzipata huduma muhimu kwa urahisi kupitia kadi zao za Tap Tap” aliongezea Colaso

Katika hotuba yake, Meneja mkuu wa Puma Energy, Philippe Corsaletti aliishukuru Airtel Tanzania kwa ushirika huo wa kibiashara na alieleza imani yake katika ushirika huo akisema kwamba itaongeza thamani ya biashara ya rejareja kwa kutoa fursa kwa watumiaji wa Airtel kutumia vituo vya Puma Energy kama sehemu ya kulipia ununuzi wa mafuta na vilainishi vya magari.

Alisema Puma Energy itaendelea kufanya kazi na Airtel na kuhakikisha inapanua upatikanaji wa huduma hii kwa vituo vyote vya mauzo vya  Puma nchini kote. Kufanikisha hili, Bwana Corsaletti aliitaka Airtel kupanua huduma ya Tap Tap katika mikoa mingine nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.