ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 6, 2016

ATIBU TAWALA BAGAMOYO AWATAKA WATENDAJI KUACHA NA TABIA YA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA RUSHWA

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Erica Yegella wa kati kati wakati wa kufungua mafunzo ya wajumbe wa mabaraza ya ya ardhi ngazi ya kata Wilayani humo kwa ajili ya kuwaongezea uwezo katika uwajibikaji wa kutatua migogoro ya ardhi
(PICHA NA VICTOR MASANGU) 
 
NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO

WATUMISHI wa umma Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  wametkakiwa kuachana na vitendo vya kuwa na tamaa, ya kupokea rusha au kutoa kwa lengo la kuweza kuuza viwanja kiholela bila ya kuzingatia sheria na utaratibu kwani kufanya hivyo kunachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha  kuwepo migogoro ya ardhi ya mara kwa mara kwa wananchi.  

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo Erica Yegella kikao maalumu cha mafunzo ya kazi kilichoandaliwa  kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuweza kutimiza majukumu  yao ipasavyo wajumbe wa mabaraza ya ardhi na nyumba ngazi ya kata zilizopo  katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Yegella alisema kwamba watendaji wa ngazi zote kwa kushirikiana na wajumbe wa mabaraza wanapaswa kuitambua vizuri sheria ya ardhi ambayo itaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa  katika kutatua migogoro ambayo imedumu kwa kipindi cha muda mrefu  ikiwa sambamaba na kutenda haki bila ya kuwa na upendeleo wowote ili kuepukana na vurugu ambazo zinapelekea uvunjifu wa amani.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Erica Yegella akizungumza na wajumbe wa mabaraza ya ardhi na nyumba ngazi ya kata hawapo pichani  katika  ufunguzi wa kikao kazi maalumu kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao katika kutatua migogoro ya ardhi kilichofanyika katika shule ya sekondari Lugoba. 
(PICHA NA VICTOR MASANGU)
“Jamani nyinyi ni watendaji hivyo ni lazima kuhakikisha mnafanya kazi kwa misingi ambayo inatakiwa kitendo cha kuuza mashamba au vinnja ni kinyume kabisa na sheria, na kingine tuache tama kabisa ya kufanya mambo bila kuangalia madhara yake kwani baadhi ya maeneo migogoro ya ardhi inachangiwa na baaadhi yetu,”alisema Yegella.

Aidha alisema kwamba ana imani baada ya watendaji hao kupatiwa mafunzo hayo yataweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kutatua migogoro ya ardhi ambayo wakati mwingine inapelekea kuwepo kwa vurugu kutokana na kugombania viwanja.

 Naye Afisa kutoka tume ya maadili ya viongozi wa umma  kanda ya Mashariki Seleman Shaban amewataka watendaji nawatumishi wa umma kuhakikisha wanazingatia maadili na taraibu zote  za kazi zao ili kuepukana na suala la kutoa au kupokea rushwa kwani ni kinyume kabisa  na sheria za nchi.

Jerome Njiwa ni Mwenyekiti wa baraza la ardhi katika Wilaya ya Kibaha ambaye alihudhuria katika kikao hicho na hapa anafafanua zaidi kuhusina na migogoro mingi ambayo imekuwa ikijitokeza katika mabaraza ya ardhi ya kata na nyumba kutokana na kutozifahamu sheria vizuri.

Kwa upande wao baadhi ya wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya  kata  na nyumba warioshiriki katika mafunzo hayo  akiwemo Mwinyikondo Asia, Mariamu Swala pamoja na Hassan Ally wamesema kwamba walikuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi katika ufanya maamuzi kutokana na kutozijua vizuri sheria za ardhi.

Mafunzo hayo  ya kuwajengea uwezo wamewashirikisha wajumbe mbali mbali kutoka katika mabaraza ya ardhi ya kata  zilizopo  katika Wilaya ya Bagamoyo  Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuweza kupunguza kero na migogoro ya aradhi ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara na kusababisha vurugu kwa wananchi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.