ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 23, 2016

MPIRA WA MIGUU SASA WATENGENEZWA KUTOKA MWANZA.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akizungumza mbele ya wahitimu wa kozi ya utengenezaji mipira ya soka katika Chuo cha D.I.T Tawi la Mwanza, mara baada ya kuleta mapinduzi makubwa katika kutekeleza adhma ya Serikali ya kuwa na viwanda vya ndani vyenye tija.
Rais wa TFF Jamal Malinzi amesema "Soka dunia nzima linaendeshwa kwa muhimili mmoja unaotambulika, wenye sheria zake 17, na suala la kuzingatia katika utengenezaji mpira ni uzito wa mpira kulingana na size ya mpira, kwani kuna size 4 kwa watoto na size 5, na yote hulindwa kwa vipimo vya mzunguko na uzito vinavyotambulika. Mkitengeneza mipira yenye kukubalika kwa viwango vya FIFA na kuwa na usanifu wa kimataifa kwenye sura ya nje ya mpira mna kila sababu ya kutinga kwenye soko la kimataifa"
"Katika vitu vinavyokwamisha soka la nchi hii mbali na kuwa na changamoto ya ukosefu wa viwanja na mtaji kwa wakufunzi changamoto nyingine ni mipira. Hivyo hii ni Fursa kubwa ambayo mkiitumia mkawa na Chapa ya kwenu kwa viwango vinavyotambulika na FIFA mmeula, kwani mbali na timu za Ligi kuu pia tuna timu za Shule za msingi ambazo ni 19,300 ukipeleka mipira 10 kwa mwaka hiyo ni karibu mipira laki 2, Shule za Sekondari 5,000 ukipeleka mipira 10 kwa kila shule kwa mwaka ni mipira elfu 50, Vilabu vya nchi hii vilivyo sajiliwa na ambavyo havijasajiliwa, amachan, professional havipungui 5,000, na timu kubwa zinapokwenda kwenye mechi za kimataifa zinaenda na mipira isiyopungua 40 au pengine 50 hivyo ni kwa maandalizi ya mchezo mmoja tu, Premium League tuna timu 16, Daraja la Kwanza 24, daraja la pili 24, Kwa hiyo kwa kifupi na mahesabu ya haraka haraka tunahitaji mipira isiyopungua laki 5 kwa mwaka. Jeh hii siyo fursa?"
Alisema Rais wa TFF Jamal Malinzi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiongoza zoezi la kukabidhi vyeti kwa wahitimu kozi ya utengenezaji mipira ya soka katika Chuo cha D.I.T Tawi la Mwanza,
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiongoza zoezi la kukabidhi vyeti kwa wahitimu kozi ya utengenezaji mipira ya soka katika Chuo cha D.I.T Tawi la Mwanza,
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiongoza zoezi la kukabidhi vyeti kwa wahitimu kozi ya utengenezaji mipira ya soka katika Chuo cha D.I.T Tawi la Mwanza,
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipokea zawadi yake toka kwa mmoja wa wahitimu.
Rais wa TFF Jamal Malinzi akipokea zawadi yake toka kwa mmoja wa wahitimu.
WANAFUNZI 14 wamehitimu mafunzo ya kutengeneza mpira wa miguu yaliyotolewa kwa wiki mbili kwenye Chuo cha Taasisi ya Ufundi (D.I.T) tawi la Mwanza.
Akizungumza katika hafla ya kuwapongeza wahitimu hao, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema anawapongeza wahitimu hao na wakitumia taaluma yao vizuri wataleta mabadiliko makubwa katika soka nchini.
Mongella ameahidi kushawishi wakurungenzi wa halmashauri za mkoani hapa kununua mipira hiyo iliyotengenezwa na wanafunzi hao kutoka chuo hicho ili kusaidia katika kukuza mchezo wa soka.
Mongella amewaomba wanafunzi hao waendelee kutengeneza mipira bora ili kuhakikisha mipira hiyo inatumika katika Ligi Kuu Bara.
Mongella amenunua mipira 40 kwa ajili ya kuzipa timu ya Mbao fc na Toto Africans zinazoshiriki Ligi Kuu, kila timu ikijinyakulia mipira 20. Kaimu Mkurugenzi wa TAN-TRADE, Edwin Rutageruka amekipongeza chuo hicho kwa kukubali mwito wa TanTrade katika kutoa mafunzo hayo.
Rutageruka ameiomba serikali iunge mkono juhudi za kununua bidhaa zinazotengenezwa nchini. Rutageruka ameliomba pia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lifanye utafiti kujua mahitaji ya mipira nchini na ameahidi kushirikiana na Rais wa TFF, Jamal Malinzi katika kutafuta soko la mpira wa miguu ndani na nje ya nchi.
Mkuu wa chuo hicho, tawi la Mwanza, Albert Mmari alisema wataendelea kutoa mafunzo hayo ili kuzidi kupata wataalamu zaidi na amewapongeza wahitimu wa mafunzo hayo ambao ni Abdallah Juma, Frank Nickson, Zacharia Gervas na Moukthtar Ahmed.
Wengine waliohitimu mafunzo hayo ni Nestory Mkumbi, Seleman Seleman, Asimwe Mganyizi, Magesa Nyakwarya, Mary Massala, Loyce Manyenye na Praxeda Lazary, Kulwa Paul, Benedicto Thomas, Malando Emmanuel, Rashid Kitambi, Clement Mange na Mouktar Ally.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.