ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 12, 2016

MHE. GODFREY ZAMBI APOKEA KADI YA MFUMO WA "WOTE SCHEME" KUTOKA MFUKO WA PENSHENI WA PPF

PPF Kadi ya Wote Scheme
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akipokea kadi ya Mfumo wa "Wote Scheme" kupitia Mfuko wa Pensheni wa PPF kutoka kwa Meneja wa PPF kanda ya Kusini Ndg. Kwame Temu.

PPF Kadi ya Wote Scheme

Meneja wa PPF kanda ya Kusini Ndg. Kwame Temu akimueleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi wakati wa kumkabidhi Kadi ya Mfumo wa "Wote Scheme".

PPF Kadi ya Wote Scheme
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akitoa neno la shukrani kwa Meneja wa PPF (Hayupo pichani) wakati wa kupokea kadi ya Mfumo wa "Wote Scheme" kupitia Mfuko wa Pensheni wa PPF.


Na. Fungwa Kilozo, Lindi
Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi ameweza kupokea Kadi ya Mfumo wa "Wote Scheme" kupitia Mfuko wa Pensheni wa PPF. 

Mhe. Zambi amepatiwa kadi hiyo ikiwa ni Siku nne tu zimepita baada ya Kujiunga na Mfumo huo katika Banda la PPF lililokuwa katika maonyesho ya Kilimo na Biashara Nane nane yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Lindi katika Viwanja vya Ngongo.

Katika Hafla hiyo ya makabidhiano ya Kadi hiyo Mh. Zambi ameutaka Mfuko wa PPF kutanua wigo na kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa wale wa vijijini kwani amesema kuwa mfuko huo unafaida nyingi ambazo wananchi hao ambao hawajabahatika kufika katika banda la maonyesho ya Nane nane watazikosa hasa mfumo wa "Wote Scheme" ambao hata yeye amefurahishwa nao na akaamua kujiunga.

MSIKILIZE HAPA AKIELEZEA....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.