ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 22, 2016

JESHI LA POLISI LAFUNGUKA KUHUSU ASKARI WAKE KUONEKANA KUFANYA MAZOEZI.

 Jeshi la Polisi leo limetoa ufafanuzi kuhusu Askari wake wanaoonekana kufanya mazoezi sehemu mbalimbali nchini kuwa ni kawaida kwa Jeshi hilo kufanya hivyo.

Jeshi hilo limesema ni utaratibu wa vikosi vyake kufanya mazoezi ya wazi.

Mazoezi hayo yamefanyika katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Singida, Mwanza na Mtwara.

Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani Singida Mayala Towo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi pamoja na Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara Thobias Sedoyeka wameeleza dhima ya mazoezi hayo.

ZIFUATAZO NI KAULI ZA MAKAMANDA WA MIKOA ILIYOHUSISHWA NA MAZOEZI HAYO.

MAYALA TOWO - SINGIDA

"Ni vizuri wananchi wakayaona mazoezi ya jshi lao yako vipi, tukifanya usiku itakuwa ni wakati wamelala au tunaweza kuwapa hofu zaidi na nyie waandishi wa Habari mtakuwa mmelala, hata leo mmejitokeza kwa kuwa mmetuona tuko kimazoezi"

Kisha akaongeza " Jeshi linaundwa na wananchi wenyewe na wanalipwa mishahara na Serikali, ni kodi zao zinawalipa, kwa hiyo tukaona ni vyema watuone kukiwa kumekucha ili wajue kodi zao zinakwenda wapi, na wanaotulinda wakoje....!!!"

AHMED MSANGI - MWANZA
"Siku zote unafanya mazoezi porini, saa nyingine yatupasa kufanya mijini, hivyo tunafanya mazoezi kulingana na michoro ya mjini, tupite tuone mji uko vipi na maeneo kama hayo yako vipi. Kwa hiyo hayo ni mazoezi ya kawaida tu! Siyo ya kumtisha mtu" alisema Kamanda Msangi na kisha kuongeza

" Wengine wanasema kwanini wanafanya mazoezi hadharani? Hatuwezi kujiweka vichakani muda wote lazima saa nyingine tuuvae uasilia, tutinge ndani ya mji"

THOBIAS SEDOYEKA - MTWARA.
"Wananchi wasiwe na hofu kwa milio waliyoisikia, madhumuni ya mazoezi haya ni kwaajili ya ukakamavu na pia kujipima kwa wakati wowote na kwa lolote" alisema Kamanda Sedoyeka na kisha kuongeza

" Hatuna nia mbaya na wananchi na hatuna sababu ya kukurupushana na wananchi isipokuwa waamini kuwa haya ni mazoezi ya kawaida kabisa.






Jeshi la polisi nchini limewatoa hofu wananchi kuhusiana na mazoezi yanayoendelea kufanywa na jeshi hilo katika maeneo mbalimbali ya nchi kuwa ni kawaida kwa jeshi kufanya hivyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.