ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 24, 2016

Airtel Money YAGAWA BILIONI 3 KWA WATEJA NA MAWAKALA.

Kulia Meneja wa Airtel Money Bw, Asupya Nalingigwa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi Mr Money wa Airtel Money atakavyogawa faida ya shilingi billion 3 kwa wateja wa Airtel Money na mawakala wake nchi nzima ikiwa ni faida yao kutokana na kutumia Airtel Money kuanzia Januari hadi juni mwaka huu kushoto ni Meneja wa uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando jana.
Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mpango wa kugawa gawio la faida ya shilingi billion 3 kwa wateja wa Airtel Money na mawakala wake nchi nzima ikiwa ni faida yao kutokana na kutumia Airtel Money kuanzia Januari hadi juni mwaka huu. Kulia ni Meneja wa Airtel Money Bw, Asupya Nalingigwa jana.
Press Release

Airtel Money yagawa billion 3 kwa wateja na Mawakala

Dar es Salaam, Jumanne 23 Agosti 2016, Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetoa gawio la faida la kila kiasi cha shilingi billion 3 kwa wateja wake wa Airtel Money na mawakala wakubwa na wadogo nchi nzima

Airtel imetoa gawio la faida kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi juni mwaka huu ambapo kila mteja atalipwa sehemu ya faida kulingana na kiasi cha salio lake katika akaunti yake ya Airtel Money kila siku

Akiongea na waandishi wa habari , Meneja Uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando alisema “Tunayofuraha kutoa gawio la faida la shilingi bilioni 3 kwa wateja wetu na wakala nchi nzima. Tunaamini gawio hili la faida litawawezesha wateja wetu kutatua mahitaji yao ya kifedha na hivyo kuthibitisha dhamira yetu ya kuendelea kutoa huduma za kifedha”

“Tumejipanga kuwawezesha wateja wetu kwa kupitia huduma na bidhaa tunazozitoa. huduma ya Airtel Money imelenga kuleta unafuu na kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha katika maeneo mbalimbali nchini hususani ya maeneo ya pembezo mwa nchi. Aliongeza Mmbando

Mpaka sasa Airtel imeshatoa kiasi cha shilingi billion 10 kwa wateja na mawakala wa Airtel money tangu  2014

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.