ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 30, 2016

RITA YAJA KUZIKAGUA TAASISI NA ASASI ZA KIJAMII MKOA WA MWANZA

Wakala wa Usajili Ufilisi naUdhamini (RITA) unapenda kuwatangazia wadhamini wote wa Taasisi na Asasi za kijamii Mkoani Mwanza kwamba kutakuwa na zoezi la kukagua na kuhakiki uhai na utekelezaji wa Majukumu ya taasisi hizo. 

 Zoezi hili litahusisha Watendaji wa RITA kupita katika Ofisi za Asasi na taasisi zao kama ilivyooneshwa katika Fomu za maombi ya usajili.

 RITA inawakumbusha wananchi kwamba ni lazima taasasi na Asasi yoyote ya kijamii inayomiliki mali kuwa chini ya Usimamizi wa Bodi ya Wadhamini ambayo nilazima isajiliwe kwa Mdhamini Mkuu (RITA) naitatakiwa kutekeleza majukumu yake kama ilivyoainishwa katika katiba na kufanya marejesho kila mwisho wa Mwaka. 

Taasisi zinazohusika ni pamoja na Misikiti, Makanisa, taasisi za kidini, Vyama vya Siasa, Klabu za Michezo, Shule na nyinginezo. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa namba 0719 017 217 

Tangazo hili Limetolewa na Emmy K. Hudson 
KAIMU MSIMAMIZI MKUU WA WADHAMINI

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.