Kituo hicho kilichopo kwenye makutano ya barabara ya Pamba na Kenyata mara ya mwisho kilifungwa juni 27 mwaka huu na Ofisa Mazingira Mkuu wa NEMC Dr.Yohana Mtoni lakini ujenzi huo umekuwa ukiendelea kimya kimya hususani nyakati za usiku jambo ambalo mkuu huyo wa idara ya ukaguzi wa NEMC amedai ni ukiukwaji mkubwa wa sheria no 20 ya mwaka 2004 inayokataza kufanyika kwa shughuli zozote kwa miradi inayohusisha vituo vya mafuta kutojengwa hadi tathimin ya athari kwa mazingira kutolewa. BOFYA PLAY KUMSIKILIZA.
BOFYA KUSIKILIZA YANAYOWASIBU.
Kutoka moja ya kuta za nyumba ukingoni mwa vilima hivi vya Igogo, ardhi ikiendelea kupuputika nao wajenzi wa kituo wakiwa wamekinga udongo unaoporomoka kwa kutumia mabati. |
Ibrahim Shahban ni mkazi wa maeneo haya akionyesha moja ya barua zilizopuuzwa awali toka Baraza la Ardhi na makazi Igogo. |
Kwa ukaribu zaidi. |
Baada ya udongo na mawe kuanza kuporomoka hivi ndivyo muwekezaji alivyo weka kingizo za mawe yaliyofungwa na waya kuzuia, ingawa hazifui dafu hasa kipindi cha mvua. |
Mwanasheria Mkuu wa NEMC Manchare Suguta amesema sheria kali zitaendelea kuchukuliwa dhidi ya watu wanaokaidi maagizo ya Serikali huku akibainisha kwamba hiyo ni mara ya 3 kwa uongozi wa Kampuni hiyo kushindwa kutekeleza maelekezo yaliyotolewa awali. BOFYA PLAY KUMSIKILIZA
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.