ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 20, 2016

COPY AND PASTE YA MKE WA TRUMP TOKA KWA BI. OBAMA YAZUA MAMBO!!!


CHANZO:- BBC SWAHILI
Sherehe ya ufunguzi wa kongamano kuu la wajumbe wa chama cha Republican nchini Marekani imegubikwa na utata baada ya hotuba iliyotolewa na mke wa Donald Trump.
Hotuba hiyo ya Melania inadaiwa kuwa na maandishi yaliyotolewa kutoka kwenye hotuba ya mke wa Rais Barack Obama, Michelle, aliyoitoa miaka minane iliyopita.

Mke huyo wa Trump, ambaye ni mzaliwa wa Slovenia, amesema alipata usaidizi mdogo sana wakati wa kuandika hotuba hiyo, ambayo imesisitiza sana maadili ya kifamilia na kujumuishwa kwa watu wa matabaka yote.

Hotuba ya Bi Obama mwaka 2008 ilisema: "Mimi na Barack tulilelewa na maadili karibu sawa, kwamba unatia bidii kutafuta unachotaka maishani; kwamba neno lako linaweka uhusiano na kwamba unafaa kutenda unachosema utatenda; kwamba lazima uwaheshimu watu, hata kama huwafahamu, na hata kama haukubaliani nao.”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.