ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 14, 2016

POLISI YACHUNGUZA SUMU OFISINI KWA MEYA WA JIJI LA MWANZA.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi 

Jeshi la polisi limeanzisha uchunguzi kubaini dhidi ya madai ya kupuliziwa hewa ya sumu ofisini kwa Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza, James Bwire.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema leo kuwa jeshi hilo tayari limewahoji watu kadhaa kuhusiana na tukio hilo lililotokea Juni 13, mwaka huu.
Ofisi za Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Juhudi za kumpata Meya Bwire kuzungumzia suala hilo hazikufanikiwa tangu juzi na jana baada ya mtu aliyepokea simu yake ya kiganjani kujibu kuwa amepumzika na madaktari wameagiza asisumbuliwe.

Madai ya sumu kupulizwa ofisini kwa Meya huyo yaliibuka muda mfupi baada ya kiongozi huyo kuingia ofisini akitoka kwenye ziara ya kukagua maeneo yalitotengwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo eneo la Sinai.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.