ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 3, 2016

MASHAUZI, SNURA, ROMA MKATOLIKI NA WAZEE WA SINGELI KUISHIKA DAR LIVE JUMAMOSI HII


Jumamosi hii ya Juni 4 mbona ‘kitanuka’ Dar Live! Ni usiku wa nani mkali kutoka kwa mastaa wataarab, bongo fleva na singeli. Ni onyesho kubwa la na mwisho kabla kuelekea mapumziko ya mwezi mtufu wa Ramadhan ambapo Isha Mashauzi akiwa na kundi zima la Mashauzi Classic ataumanajukwaanaSnura, Roma Mkatoliki, Sholo Mwamba na Man Fongo. Msemaji wa ukumbi wa Dar Live, Juma Mbizo amesema onyesho hilo la kipekee limezingatia muziki wakila nyanja ilikuleta ladha isiyochuja mwanzo hadi mwisho wa show. 

Mbizo amesema kupitia onyesho hilo mashabiki watajionea wenyewe nimzuki upi wenye nguvu zaidi kati ya taarab, bongo fleva, singeli na hata rumba kutokana na ukweli kuwa Isha Mashauzi mbali na taarab lakini pia anangoma zake kali zamuziki wa rumba.

Naye Isha Mashauzi amesema atalitendea haki onyesho hilo hasa kutokana na ukweli kuwa hajapanda jukwaa la Dar Live kwa takriban miaka miwili na hivyo hiyo ni nafasi pekee ya kuka ta kiu ya mashabiki wake watakaofika kwenye ukumbi huo mkubwa zaidi wa burudani ulioko maeneo ya Mbagala jijini Dar es Salaam.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.