ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 10, 2016

TBL MWANZA YALAMBA TUZO NYINGINE.

TBL,Mawnza yashinda Tuzo ya teknolojia ya kisasa Duniani.
Kiwanda cha bia cha TBL mwanza kimejishindi tuzo ya teknolojia ya kisasa ya kuzalisha mvuke unaotumika katika upishi wa bia ,tuzo hiyo imetolewa huko nchini London  na  kampuni ya ushindani  na utafiti  ya SIB Miller kutoka nchini humo  viwanda vingi hushindanishwa ili kupata kiwanda ambacho kinao uwezo wa kukidhi vigezo.

 Tuzo hiyo ya Uvumbuzi wa Teknolojia mpya  iliandaliwa na Thomas Bruwer  ambaye ndiye alikuwa anaendesha mradi wa DDH  ( dry dehiscing)  na kushirikisha viwanda takribani vyote  Duniani.

Akizungumza na Vyombo vya habri  jijini Mwanza  Mkurugenzi wa ufundi  wa TBL Bwana  Gavin Van Wisk   amesema tuzo hiyo wameipokea siku chache kutoka nchini London, amewashukuru sana wafanyakazi wote wa TBL  Mwanza kwa kuhakikisha wamejishindia tuzo hiyo na hiyo ni kutokana na juhudi zao kama wafanyakazi.

Aidha Bwana Pitso amesema hivi sasa kwa uzalishaji wa bia katika ushindani wa kidunia wamekuwa ndani ya washindi kumi bora  wa kimataifa wa uzalishaji,wakati kwa Africa wamekuwa wazalishaji wa bia yenye ubora yenye ubora kuliko kiwanda chochote.
Akizungumza na G sengo Blog  Bwana Osca Kilasi  ambaye ni meneja wa Ubishi kutoka Mwanza amesema mradi umesaidia kupumguza matumizi ya dizeli , umeongeza uwezo wa kiwanda kuzalisha,hata katika mazingira mradi huo unapunguza uharibifu wa mazingira, lakini mzunguko wa wa wapishi umekuwa mfupi kutoka  masaa mawili na dakika sabini hadi  masaa mawili na  dakika hamsini,hata  katika eneo la gharama  za umeme umepunguzo kwa kiasi kikubwa matumizi ya Umeme,

“ Hii ni  teknologia ambayo itaenda viwanda vingine  na teknolojia hii unachukua shairi unatoa maganda na yale maganda   yanatumika kwenye boiler kwa ajili ya kuzalisha mvuke,hii inasadia bia kuwa nzuri,inakaa zaidi sokoni na inachujika kirahisi  baada ya kutumia mafuta wanatumia maganda ,hii hufanya bia kukaa kwa muda mrefu sokoni” Alisema Oscar
Hata hivyo wakati akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Wafanyakazi bwana  Pitso Gabriel  (plant Manager) amesema  Wao kama timu ya Mwanza wamefurahi hasa kwa uzinduzi wa teknolojia na namna ilivyoleta matunda  katika uzalishaji.
“ Zawadi hii itawafanya hata kuongeza nguvu ya uzalishaji na hata hivyo ushindi huu umetuongezea ujasiri wa kufanya kazi kwa juhudi na kujituma ili kuhakikisha hata mwakani tunaongeza tuzo nyingine nyingi” alisema Pitso  


Teknolojia hii ili kiwanda kiweze kutuitumia ni lazima waombe kibali kutoka TBL Mwanza na taarifa zinasema kuwa baadhi ya viwanda kutoka Nigeria na Nampula  tayari wameomba kutumia teknolojia hii ya kisasa na kipekee duniani.





Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.