ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 30, 2016

TWANGA PEPETA YAZINDUA ALBUM YAKE YA 13 'USIOGOPE MAISHA' MBELE YA MKUU WA MKOA WA MWANZA NA KUCHANGIA MADAWATI.

Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiwakaribisha wakazi wa Mwanza katika Uzinduzi wa Album ya 13 ya Bendi ya Twanga Pepeta inayojulikana kwa jina la 'Usiyaogope Maisha' uliofanyika Villa Park jumamosi na kuhudhuriwa na mamia ya mashabiki wa burudani ya muziki wa nyumbani akiwemo mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela.
Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa album ya 13 ya Bendi ya Twanga Pepeta Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela (kulia) akizungumza na wadau wa burudani ambapo pia ilikuwa fursa ya kufanya harambee fupi ya kuchangia madawati kwa ya manufaa ya shule zenye uhaba, Kushoto ni Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka mara baada ya kumkaribisha mgeni rasmi, mpango mzima ukifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbiwa Villa Park Resort.
Mikononi mwa mgeni rasmi album 'Usiyaogope Maisha'
Wadau wa burudani  walizichanga kwa njia mbalimbali....
Mkurugenzi wa Semira LTD naye alipata nafasi ya kuchangia katika harambee fupi iliyofanyika ndani ya uzinduzi wa album 'Usiyaogope Maisha' ya Bendi ya Twanga Pepeta.
Afande Abou aka Mzee wa Boma ya Ng'ombe akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela mara baada ya kuchangia harambee ya madawati kwa shule za Mwanza ndani ya uzinduzi wa album Usiyaogope Maisha ya Bendi ya Twanga Pepeta.
Master Plan naye alipata fursa ya kuujazia mfuko wa madawati.
Zamu ya Ashraf.
Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akikabidhi kiasi cha shilingi milioni 1.3 kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela  zilizochangwa na waakazi wa Mwanza kwenye zoezi la 'Changia elimu papo hapo'   katika Uzinduzi wa Album ya 13 ya Bendi ya Twanga Pepeta uliofanyika Villa Park mwishoni mwa wiki siku ya jumamosi na kuhudhuriwa na mamia ya mashabiki wa burudani ya muziki wa nyumbani.
Shukurani za Mkuu wa Mkoa mara baada ya fedha kukabidhiwa kwa Mr. Matia Levi (kulia) ambaye ni Katibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa album ya 13 ya Bendi ya Twanga Pepeta Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela (kulia) akibofya rimoti kwaajili ya wadau wa burudani kujionea kwa mara ya kwanza Video ya album mpya ya Twanga Pepeta iitwayo 'Usiyaogope Maisha'  Kushoto ni Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akishuhudia tukio hilo, mpango mzima ukifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbiwa Villa Park Resort.
Rais wa Bendi ya Twanga Pepeta Ally Choki (kushoto) na Makamu wake Luiza Mbutu (kulia) wakiongoza safu ya mashambulizi jukwaani.
Hapa Kalala Jr, hapa Haji BSS na hapa Luiza Mbutu.
Rogati Hega na sauti yake adimu kwa stage la Twanga.
Makamuzi yaliendelea kwa style yake.
Hatari sana.
Kikazi zaidi.
Mashambulizi ya Twanga.
Mzuka wa bass guitar ulipopanda ilikuwa zaidi ya uchizi.
Zile swaggZ....pale kati.
Shabiki na stage la Twanga Mwanza.
Chekshia.
Keyboardist wa Twanga Pepeta mtamboni huku Luiza Mbutu akichombeza kwa pembe ni balaaa.
Mpigaji wa solo guitar na Twanga Pepeta akifanya mashambulizi.


Kwa hisia zaidi Kalala Jr na Luiza Mbutu.
Twanga Pepeta dadaz....mbeeeeele.
Ally Chiki akiimbisha  mashabiki wake.
Double impact.
Selfie na kamera ya Gsengo.
Drummer boy wa Twanga Pepeta James Kibosho na selfie ya Gsengo blog.
Taswita kutoka juu.
Another selfie.
Meneja wa Villa Park Mwanza Rammadhan akiwa na mkewe Bi Husna.
The last Selfie kwa tukio.
Kama ni nafasi ya kuwaizungumzia Twanga Pepeta ya sasa kauli ninayoweza kuitoa kuhusu onyesho lao la burudani Mwanza , ni kuwa "Onyesho la Jumamosi lilikuwa la aina yake, nidhamu ya jukwaani ilikuwa kubwa kiasi cha kushangaza, uchaguzi wa nyimbo (playlist) ukadhihirisha kuwa Twanga Pepeta ina utajiri wa nyimbo nyingi kali, za zamani hadi za sasa, kwa upande wa ma-vocalisti daah wametulia hawana papara wanajua wanachofanya, wanaimba kwa kupokezana wakipishana kimahesabu sahihi ya muziki....Nashindwa kubaini nani alikuwa nyota wa mchezo kwani hata wanenguaji walikuwa balaaa. 

BIG UP TWANGA PEPETA 'KISIMA CHA BURUDANI' TUTAINUNUA SANA ALBUM YENU 'USIYAOGOPE MAISHA' 
by Gsengo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.