ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 15, 2016

TAANESCO MKOA WA PWANI YAMAKAMATA MMILIKI WA YADI YA MAGARI KWA WIZI WA UMEME

NA MWANDISHI WETU

SHIRIKA la ugavi wa umeme Tanesco Mkoa wa Pwani limefanikiwa kumkamata moja ya mteja wake  ambaye ni  mmiliki wa yadi ya magari ya White star iliyopo kiluvya kwa Komba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kwa kosa la kuhujumu miundombini kwa kufanya wizi baada ya kuamua   kujiunganishia umeme  kinyemela  wa njia tatu kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mteja huyo alikamata baada ya kufanyika kwa msako  mkali kwa wateja ambao wanaiba umeme na kuweza kubaini katika yadi hiyo kuna hujuma ambayo imefanyika ya kujiunganishia umeme bila ya kufuata taratibu zozote za Tanesco.

Akizungumza katika eneo hilo la tukio Afisa Usalama wa Tanesco Mkoa wa Pwani Henry Byarugaba alisema kwamba baada ya kufanya ukaguzi waliweza kukuta mtaja huyo alijulikana  kwa jina la Munila Mbowe ambapo aliweza kukamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi cha Kibaha.


Byarugaba alisema kwamba mteja huyo alikuwa anatumia umeme wa wizi kutokana na kujiunganishia laini tatu za nyaya ambapo kutokana na wizi huo ameseza kulisababishia hasara shirika zaidi ya shilingi milioni 50.

“Kama mnavyoona ndugu waandishi katika kufanya msako wetu wa kawaida tumeweza kumkamata mmiliki wa yadi ya magari ya white star ambayo ipo kiluvya kwa kombo kwa kosa la kuiba umemembila ya kuzingatia sheria zozote na kwamba ameweza kujiunganishia njia tatu ambazo zilikuwa zinapitisha umeme kwa matumizi ambayo sio sahihi katika eneo hilo,”alisema Byarugaba.

Aidha Byarugaba alisema mteja huyo amekuwa akifanya vitendo vya kuhujumu miundombinu yao na kufanya uharibufu mkubwa hali ambayo inaweza kuleta madhara makubwa ya kutokea kwa majanga ya moto kutokana na kujiunganishia umeme  bila ya kuwatumia wafanyakazi wa shirikika la umemem Tanesco.

Pia alisema kuwa mteja huyo amekuwa ni sugu kwa kipindi cha muda mrefu kutokana na kujirudia kwa makosa kama hayo kwani mwaka jana wakati wanafanya msako kwa wateja wao wanaohujumu miundombinu waliweza kumkuta akiiba tena  umeme na walimpeleka polisi na hatua kali za kisheria ikiwemo kumlipisha faini.

“Jamani ndugu waandishi huyo mteja wetu ambaye anajulikana kwa jina la Munira Mbowe amekuwa akifanya matukio haya kwa kipindi cha muda mrefu na kutokana na hali hii amelitia hasara shirika la umeme, maana mwaka jana tulimkamata tena akiifanya vitendo kama hivi na tulimfukisha katika vyombo vya sheria lakini nashangaa amekuja na staili hyingine ya wizi kwa kutumi tena njia tatu  za umeme hii ni hatari sana.

Kwa upande wake mmoja ya wamilii ya yadi hiyo ya Munira Mbowe alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusina na tumuma za wizi huo alisema kwamba yeye afahamu lolote juu ya suala hilo kwani mara nyingi yeye  anafanyia shughuli zake jijini Dar es Salaam.

“Ni kweli tumekutwa na kosa na kuiba umeme lakini jamani waandishi  nataka niwaeleze kuwa mimi siusiki na kingine nawaomba msinitoe katika vyombo vya habari kwani haya ni maisha tu, sio vizuri kunitoa jamani mimi sihusiki kabisa katika wizi huu labda anaweza kuwa ni mlinzi amefanya hivyo au mume  wangu amenificha maana wanaume ni wasiri sana,”alijitetea Munira.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Taneso Mkoa wa Pwani Selemani Mgwila alisema kwamba kitendo alichokifanya mteja wao ni kosa kubwa sana kwani umeme waliokuwa wanatumia katika yadi hiyo ulikuwa unapotea bure na kusababisha upotevu mkubwa wa mapato.


Aidha Mgwila aliwaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani kuepukana na watu ambao wanajifanya ni watumishi halali wa tanesco na endapo wakiwabaini wahakikishe wanatoa taarifa mapema kwa vyombo vya dola ili waweze kuchukuiliwa hatua kali za kesheria kwani baadhi yao ni matapeli.

SHIRIKA la umeme Tanesco Mkoa wa Pwani limekuwa likiingia hasara kubwa kutokana na baadhi ya wateja wake kuamua kujiunganishia umeme kinyemela pasipo kuzingatia sheria na taratibu na wakati mwingine kupelekea kutokea kwa majanga ya moto.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.