ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 15, 2016

KUELEKEA JEMBEKA NA VODACOM HIVI NDIVYO 'VIPAJI FRESH' VILIVYOIBULIWA MWANZA.

Mmoja kati ya majaji wa mchakato wa kusaka vipaji Mwanza, wakuitwa  Mwaka Mzima kutoka Jembe Fm akitoa maksi zake kwa mmoja wa washiriki wa 'Vipaji Fresh' ambapo washiriki hao watakwenda kushindanishwa katika fainali itakayofanyika katika Tamasha la Jembeka Festival  uwanja wa CCM Kirumba jumamosi ya tarehe 21 Mei 2016.  Chini ya Udhamini wa Vodacom.
Hapa ilikuwa shughuli.
Maufundi katika 'VIPAJI FRESH'
Pia 'VIPAJI FRESH' ilisaka ma-Dj na hapa mmoja kati ya wakali akionyesha maujuzi yake kwenye mashine zilizofungwa Jembe Beach Mwanza.
Jimmy Kagaruki ni mtangazaji wa kipindi cha Mchakamchaka kupitia 93.7 Jembe Fm naye alishiriki kubaini 'VIPAJI FRESH' vilivyojitokeza Jembe BeachMwanza kuelekea Tamasha kubwa la Burudani la kila mwaka lijulikanalo kama JEMBEKA FESTIVAL linalidhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Nani aliibuka kuwa mkali zaidi yao ambaye atapanda jukwaa lile lile atakalopanda mwanamuziki mahiri kutoka nchini Marekani Neyo? Basi hapa Chief Judge wa 'VIPAJI FRESH' Deejay K-Flip alikuwa akitangaza washindi.
SwagZ nazo zilihusishwa.
'VIPAJI FRESH' Kupitia uchekeshaji ni Balaaaa.......
Majaji mezani.
Watu na watu  wao.
Dj katika 'VIPAJI FRESH'
Mwanza inavipaji ......imagine wote hawa  walikuwa wanasaka nafasi.
Si haba mmoja mmoja kupitia vipaji tofauti tofauti, iwe ni Dj, Mchekeshaji, Mtangazaji, Mkali katika kucheza au kipaji chochote kati ya hawa ataibuka kuwa mshindi katika 'VIPAJI FRESH' kwa tamasha kubwa la Burudani JEMBEKA FESTIVAL litakalo ungurumishwa uwanja wa CCM Kirumba jijini  Mwanza Jumamosi ya Tarehe 21 Mei 2016, chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.