ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 19, 2016

ARUSHA WAHAIDI KUTOACHIA TAJI LA MISS TANZANIA

 baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la kumsaka mlibwende wa mkoa wa Arusha wakiwa katika pozi
 warembo hao wakiwa wanacheza hii ikiwa ni moja ya mazoezi yao wanayoyafanya ndani ya ukumbi wa  hoteli  Naura Spring Arusha ambapo wameweka kambi
Na Woinde Shizza,Arusha
Kusimamishwa kwa shindano la umrembo  Tanzania (miss Tanzania ) kwa mwaka mmoja imekuwa ni changamoto kubwa kwa waandaaji wa shindano hilo kwani  warembo wengi wamesahau na shindano kwa ujumla limepungaza motisha.

Hayo yamebainishwa na muaandaaji wa  shindano la kumsaka mrembo wa mkoa wa Arusha kutoka katika kampuni ya  Tour Visual Entertainment Penda Simwita  wakati akiongea na mwaandishi wa habari jana katika kambi ya kumuandaa Miss Arusha.

Alisema kuwa kwa upande wake kumekuwa shindano hili limekuwa gumu kidogo kwani warembo wengi wamejipweteka na walijisahau kuwa kunashindano kama hili kwa mwaka huu hivyo ilimlazimu kutembelea katika vyuo mbalimbali vya hapa mkoani Arusha kwa ajili ya kuwatafuta warembo ambao  watashiriki shindano hili.

"pamoja na kuwa tumewatafuta likini kiukweli tumewapata warembo wazuri wanasifa na naamini wataweza kutetea taji la miss Tanzania likatoka hapa kwani wanauwezo na kizuri zaidi najiamini naweza kuwaandaa maana ata mrembo ambaye anashikilia taji sasa ivi alitoka mkoa wa Arusha, na kipindi kile kulikuwa bado kuna mrembo wa vitongoji kwaiyo alitoka kwangu ambapo niliandaa miss Arusha City Cetre  kwa iyo naamini na uyu atatoka pia kwangu maana najua kuwapika na kuchagua warembo wazuri wenye sifa heshima na uwezo pia wanao"alisema Pendo.

Gazeti hili lilizungumza na mmoja wa warembo hao Maurine Ayubu naye alisema kuwa amefurahi kushiriki shindano hili naanao uwakika kwa kuwa anasifa zote za kuwa mrembo wa Mkoa wa Arusha,mrembo wa kanda ya kaskazini na pia anaamini atatetea taji la miss tanzania libaki Arusha kama linavyoshikiliwa sasa ivi na mrembo wa Tanzania Lilian kamazima.
 
"nasema hivyo kwakuwa najua urembo najiamini na ninauwezo kwaiyo naamini nitachukuwa,pia kuna ili swala watu wengi wamekuwa wakilichukulia na kusema kuwa   kuwa miss ni umalaya nataka niwatoe shaka na niwaambie watu hususa ni wazazi  umiss ni urembo kama urembo mungine na sio umalaya kwani  kila mtu anakuwa na tabia yake ambayo ametoka nayo kwao kwa iyo akifanya kitu anafanya kama yeye na sio kwamba mrembo akiwa malaya  basi shindano hilo ndio linawafundisha la hasha bali ni tabia ya mtu binafsi hivyo ata wazazi wasiwazuie watoto wao kushiriki shindano hili kwa kuwa na dhana ya kuwa shindano hili ni lakimalaya"alisema Maurine.

Jumla ya warembo 17 kutoka katika mitaa mbalimbali  na wilaya mkoani hapa wanatarajiwa kupanda jukwaani mapema May 28 mwaka huu katika ukumbi wa Hotel ya Naura Spirng  kwa ajili ya kumsaka mlibwende wa mkoa wa Arusha ambaye atawakilisha mkoa katika kinyanganyiro cha kumsaka mrembo wa Tanzania na tukumbuke mpaka hivi sasa taji hilo la mrembo wa Tanzania linashikiliwa na mrembo kutoka mkoa wa Arusha Lilian Kamazima .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.