ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 31, 2016

WAKALI KUTOKA MWANZA WAANZA KUFYATUA TRAXX MAALUM KWA JEMBEKA FESTIVAL.

Ikiwa imesalia miezi miwili tu kwa wasanii mbalimbali na wapenzi wa burudani nchini Tanzania wapate kushuhudia Tamasha kubwa la burudani linalofanyika kwa mwaka wa pili jijini Mwanza nazungumzia Jembeka Festival 2016 Tamasha linalotarajiwa kufanyika mnamo mwezi Mei tarehe 22 mwaka huu.

Tayari baadhi ya wasanii kutoka Mwanza wameshaanza kuonyesha moto wao jinsi ya namna vipi watakavyokwenda kulipamba tamasha hilo ambalo ndani ya kipindi kifupi limeweza kuteka hisia za wengi kutokana na either vihusishi vinavyotajwa kuwako tamashani mwaka hadi mwaka ima mahusiano mazuri ya kampuni husika JEMBE NI JEMBE na MASHABIKI WAKE kwamba kwa kila wanacho ahidiwa ndicho ambacho huwa kinafanyika tena kwa ubora.

Kupiti mstakabar huo wasanii kutoka mji wa waasisi wa Tamasha hilo  unaotambulika zaidi kama Rock City, tayari msanii mmoja mmoja na wengine kwa makundi wameanza kuachia ngoma zao za uhamasishaji wa burudani kwa tamasha hilo, ukijikita kwenye maaudhui, amshaamsha zake pamoja na kauli mbiu ya mwaka wa tamasha husika.

Biznea na Coyo Mc ni wasanii wa Hip-hop toka Mwanza waliojizolea heshima sasa kutokana na kuwa na kazi nzuri zinazo bang kwa hewa anga za radio stesheni mbalimbali Kanda ya Ziwa na kote nchini, nao wametinga studio za Update Record chini ya mtayarishaji Dee Classic na kufyatua mpini uliokwenda skuli walioubatiza jina la Gusa Nikuguse Tugusane.

Najua unahamu ya kuonja ladha ya mpini huo (BOFYA PLAY) 

Msanii maarufu wa muziki wa R&B kutoka nchini marekani Neyo na Diamond Platnumz kutoka nchini Tanzania ni moja kati ya wakali watakao ungana na wengine wakali kutoka pande mbalimbali wenye uwezo watakao tosha kukisanukisha siku hiyo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege amesema kuwa yuko kwenye mazungumzo ya mwishoni na Makampuni mbalimbali ambayo yameonyesha nia ya kuwa sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo na hadi sasa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi Vodacom Tanzania tayari imeweka miguu yote miwili na kuwa mdamini mkuu wa JEMBEKA FESTIVAL 2016 KAZI NI KWAKO.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.