ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 18, 2016

MMALIM SEIF AIONDOA FAMILIA YAKE ZANZIBAR NA KUIPELEKA MUSCAT OMAN.

Pichani ni mkewe Seif Shariff Hamad, Bi Awena Sinani Masoud akiwa chumba cha VIP uwanja wa ndege na tiketi yake ya Oman Air, muda mfupi kabla ya kuondoka.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad ameondosha familia yake katika Kisiwa cha Unguja na kuipeleka Muscat-Oman.

Familia hiyo ya Maalim Seif Shariff Hamad wameondoka jana jioni kwa kutumia ndege ya Shirika la ndege la Oman (Omar Air). Familia hiyo ya Maalim Seif imeondoka katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport saa 5:50 jioni hii.

Haikuweza kufahamika mara moja sababu hasa za Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Seif Shariff Hamad kuiondoa familia yake Zanzibar. Kwa sasa Makamu huyo wa Kwanza wa Rais yupo katika mapumziko katika Hoteli ya Kitalii ya Dar es Salaam Serena.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.