ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 28, 2016

SERIKALI ITATUWE NA HILI LA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA NA MADAWATI.

Lupemba shule ya msingi iliyoko wilayani Magu mkoani Mwanza, wakipata masomo.

SHULE YA MSINGI LUPEMBA ILIYOKO MAGU YAKABILIWA NA UHABA WA MAJENGO NA MADAWATI.
NA Shushu Joel,Magu
TUMEZOEA kusikia shule zilizoko vijijini ndani ndani ndizo zinakabiliwa na tatizo la madawati na majengo,lakini kumbe hata zile za karibu na mijini bado ni shida kwani shule ya msingi Lupemba iliyoko wilayani magu mkoani mwanza inakabiliwa na matatizo hayo

Shule hiyo iliyoko karibu kabisha na ofisi za mji mdogo wa halmashauri ya magu,inapungukiwa madawati zaidi ya 400 na majengo ya madarasa yasiyopungua 5, licha ya kuwa karibu na ofisi hizo, lakini cha kushangaza zaidi hakuna kiongozi wa aina yeyote ile ambaye amefikilia chochote kile juu ya kutatua tatizo hilo linalowakabili wanafunzi hao wanaosomea kwenye mahema na matofali.

Shule hii ya Lupemba ilifunguliwa rasmi miaka michache tu iliyopita,pamoja na upungufu wa madawati na majengo bado pia inakumbwa na tatizo la upungufu wa walimu kwani waliopo ni walimu 8 tu wanawake ni 5 na 3 ni wanaume huku shule ikiwa na jumla ya wanafunzi 620.

Hayo ni baadhi tu ya matatizo yanayoikabili shule hiyo ya msingi Lupemba ambayo idadi kubwa ya wanafunzi wanaishia kukaa chini na kusomea kwenye mahema na huku wakiendelea na shughuli zao zingine za darasani kama ilivyozoeleka kwa wanafunzi wetu.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Daniel Matemi anathibitisha uwepo wa tatizo hilo katika shule yake na kusema kuwa suala hili hata yeye amelikuta katika shule hiyo ingawa amekwisha lifikisha katika sehemu husika ila mpaka sasa bado hakuna lolote lililofanyika.

“Tumewabana sana wazazi wa wanafunzi wetu katika michango mbalimbali japo tuweze kuinusuru shule hii lakini suala hili linakuwa ngumu kwa upande wa wazazi hao nah ii ni kutokana na siasa chafu zilizopo katika kijiji hiki na hili ni kutofautiana kwa vyama kati ya mwenyekiti wa shule na mwenyekiti wa kijiji ndio changamoto kubwa inayochangia kuwaumiza wanafunzi hao.

Mkuu huyo aliongeza kuwa kilichobaki kwa sasa ni kuwaomba wafadhili walio na moyo ili wajitokeze kuweza kuifadhili shule hii na kuweza kuinusuru katika janga hili kwani kipindi hiki cha mvua sijui itakuwaje kwa wale wa darasa la 5,6 na 3 ambao wanasomea kwenye mahema,kwa kusema ukweli watoto hawa wanapata taabu sana.

Shule ya msingi lupemba wilayani Magu inasikitisha.
“Ndugu mwandishi kama unavyojua sisi wenyewe hatuna cha kuwasaidia,kama unavyofahamu kuwa mwanafunzi anayekaa chini unamkosesha mambo mengi sana” alisema mkuu huyo wa shule.

Kwa ujumla hali hii inawafanya wanafunzi hao kupunguza uwezo wao wa kufanya vizuri darasani.

Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi wilaya ya magu Yesse Kanyuma alipohojiwa juu ya shule hiyo alisema kuwa yeye si msemaje juu ya hilo na wala ajui lolote kuhusu shule hiyo ya lupemba.

N kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Ntinika  Paul alipopigiwa simu yake ili kuthibitisha kwa habari ya shule hii simu yake iliiita bila kupokelewa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.