ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 17, 2015

MWANZA YAAHIDI KUMPA KURA ZA NDIYO MAGUFULI :- AWANADI VYEMA WAGOMBEA UBUNGE ILEMELA NA NYAMAGANA.

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt.John Pombe Magufuli akimwaga sera kwa wananchi waliofurika kwa wingi kwenye mapokezi yake jijini Mwanza, na hapa alikuwa akitokea uwanja wa ndege wa Mwanza kuelekea viwanja vya furahisha ambako ndiko shughuli nzima ilifanyika.
Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kwa wananchi waliojitokeza kumpokea.
Watu na mtu wao.....
Sasa ni safari kutoka airport Mwanza hadi viwanja vya Furahisha vilivyoko Kirumba jijini Mwanza.
Barabara ya Makongoro jijini Mwanza.
Watu wamefurika hapa.
Ni upenyo almuradi kupata kuona kile kilichokuwa kikifanyika.
Katika mkutano huo Dkt.Magufuli alipata mapokezi makubwa kiasi cha kuuufanya Uwanja wa Furahisha kuelemewa na idadi ya wananchi na Makada wa CCM waliofika uwanjani hapo.
Katika mkutano huo Dkt.Magufuli alipata mapokezi makubwa kiasi cha kuuufanya Uwanja wa Furahisha kuelemewa na idadi ya wananchi na Makada wa CCM waliofika uwanjani hapo.
Akizungumza katika Mkutano huo,Dkt. Magufuli alishindwa kuficha hisia zake na kueleza kuwa Mwanza wamejitokeza kwa wingi sana kiasi cha kufanya idadi ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kutofikiwa na idadi yoyote ya wananchi waliojitokeza katika mikutano ya kisiasa barani Afrika.
Katika hotuba yake Dkt.Magufuli alisisitiza kwamba hatawaangusha watanzania ikiwa watampa ridhaa ya kuwa rais wao katika Uchaguzi Mkuu ujao unaotarajia kufanyika Octoba 25 mwaka huu na kuongeza kuwa atahakikisha anasimamia vyema shughuli za maendeleo ikiwemo kufufua viwanda vilivyobinafsishwa na havifanyi kazi, kutoa elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne pamoja na kuondoa kero ya ushuru inayowakabiri watanzania hivi sasa
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza Dkt.Antony Diallo akizungumza katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza kwenye mkutano wa hadhara wa kuomba kura kwa wananchi katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu nchini.
Ikiwa ni kwa ajili ya maendeleo yao, dkt.Magufuli aliwaomba watanzania kuwachagua viongozi wanaotokana na CCM Kuanzia ngazi ya Madiwani, Wabunge na Rais ambapo aliwatambulisha wagombea mbalimbali Mkoani Mwanza akiwemo Stanslaus Mabula ambae ni mgombea ubunge Jimbo la Nyamagana (kulia) pamoja na Angelina Mabula ambe ni Mgombea ubunge jimbo la Ilemela (kushoto)
Magufuli ameomba ridhaa ya kuwatumikia wananchi huku akiahidi kuwa iwapo wananchi wakimchagua kuwa rais wa awamu ya tano atakuwa kufuli la kufunga milango na upenyo wa mianya yote ya rushwa na ufisadi katika idara mbalimbali za serikali.
Angelina Mabula ambe ni Mgombea ubunge jimbo la Ilemela.
Stanslaus Mabula ambae ni mgombea ubunge Jimbo la Nyamagana.
Bango lasomeka hivi.
Wananchi wakipunga mikono hewani kuashiria maridhiano na kile kilichokuwa kikiendelea jukwaa kuu.
Wananchi wakisikiliza sera katika Uwanja wa Furahisha kwenye mkutano wa hadhara wa Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli wa kuomba kura kwa wananchi katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu nchini.
Watu na vyama vyao....watu na watu wao.
Ni katika Uwanja wa Furahisha kwenye mkutano wa hadhara wa Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli wa kuomba kura kwa wananchi katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu nchini
Wananchi waliofurika kusikiliza sera kwenye mkutano wa hadhara wa Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli wa kuomba kura kwa wananchi katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu nchini.
Wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM zilizohudhuriwa na Maelfu ya watu.

Uchaguzi Guinea:Alpha Conde aongoza


Image copyrightAFP
Image captionAlpha Conde
Matokeo ya duru ya kwanza ya uchaguzi wa urais nchini Guinea yanaonyesha kuwa rais wa sasa Alpha Conde ameshinda kura za kutosha kuzuia kuwepo duru ya pili ya uchaguzi.
Huku asilimia 90 ya kura zikiwa zimehesabiwa tume ya uchaguzi ya nchi hiyo inasema kuwa bwana Conde yuko mbele ya mshindani wake mkuu Cellou Dalein Diallo.
Image copyrightAFP
Image captionCellou Dalein Diallo.
Kiongozi huyo wa upinzani alisema wiki iliyopita kuwa alikuwa anajiondoa kwenye uchaguzi huo akidai kuwepo udanganyifu.
Uchaguzi huo ulifanyika licha ya janga la hivi majuzi la ugonjwa wa ebola ambalo liliwaua maelfu ya watu. CHANZO BBC SWAHILI.

MAMIA WAMUAGA MBUNGE WA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE NA NDUGU ZAKE NYUMBANI KWAKE KIJICHI JIJINI DAR ES SALAAM

 Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe enzi za Uhai wake.
 Msaidizi wa Mbunge huyo, Casablanga Haule enzi za Uhai wake.
 Padri Plasdus Ngabuma enzi za Uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe wakati wa ibada ya kuuaga iliyofanyika nyumbani kwake Kijichi Dar es Salaam leo mchana.
 Majeneza yenye miili ya aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe na ndugu zake, Plasdus Ngabuma na Casablanga Haule yakiwa yamewekwa mbele wakati wa ibada ya kuiombea iliyofanyika nyumbani kwa mbunge huyo Kijichi Dar es Salaam leo, kabla ya kusafirishwa kwenda Ludewa kwa mazishi.
 Mjane wa Deo Filikunjombe, Sarah (katikati) akisaidiwa na jamaa zake wakati wa ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Padri Maxmillian Wambura kutoka Parokia ya Mtakatifu Wote Kiluvya akiyamwagia mafuta ya baraka majeneza hayo.
 Waombolezaji wakiwa katika ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza la Plasdus Haule.

 Jamilia ya Filikunjombe ikiwa katika ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
Nyumba ya Filikunjombe ambayo inadaiwa amekaa wiki mbili tangu ahamie baada ya kukamilika ujenzi wake 'Hakika tumuache mungu aitwe mungu"

BARAZA KUU LA WAISLAMU MKOA WA MWANZA LAMUONYA ASKOFU GWAJIMA

Jana Ijumaa ya Octoba 16,2015 Baraza Kuu la Waislamu Mkoa wa Mwanza liliungana na Waislamu wengine kuadhimisha mwaka mpya wa Kiislamu ambao ni 1437. 
Kwa kalenda ya Kiislamu sherehe hizo zilifanyika jana tarehe mbili, mwezi Muharamu mwaka wa 1437 (02.01.1437) ikiwa maadhimisho yanayoambatana na kumbukumbu ya Kuhama kwa Mtume Muhammad kutoka Mji wa Macca kwenda Madina.

Katika kuadhimisha sherehe hizo, Baraza hilo kupitia kwa Katibu wake Mkoani Mwanza Sheikh Mohamed Balla (Kulia Pichani) alitoa tamko kwa niaba ya Waislamu wote Mkoani Mwanza kutokana na kauli inayoelezwa kutolewa na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima kwamba ana ndoto ya Misikiti yote nchini kugezwa kuwa Sunday School na Masheikh watakwenda kuangukia katika misalaba. 

Alisema kauli za namna hiyo si njema kwa mstakabali wa Taifa ambapo alisema kuwa Waislamu wote Mkoani Mwanza wanalaani na kukemea kauli hiyo na nyingine zote za aina hiyo na wale wanaozitoa.

Aliwataka Watanzania kuungana kwa pamoja hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu na kwamba Wamchague kiongozi muadilifu, Mchapakazi na anaechukia rushwa ambae ataendelea kuwaunganisha watanania wote. 
Imam wa Msikiti Khadija Jijini Mwanza Mohammed Awadhi akisoma Ibada ya Quran katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Sheikh Mahamood Khasan akisoma ibada ya kuliombea taifa amani katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Imam wa Msikiti wa Ibadhi Jijini Mwanza Nouh Othman akisoma mada juu ya mwaka mpya wa kiislamu wa 1437 katika Sherehe zilizofanyika jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Mwanza na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kuendeleza Quran na Sunna nchini JUQUSUTA Sheikh Hassan Kabeke akiwasilisha mada juu ya amani katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Qaswida
Qaswida
Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika Sherehe za Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.
Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya Sherehe ya Mwaka mpya wa Kiislamu (1437) ulioadhimishwa jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza na kuambatana na ibada mbalimbali ikiwemo kuliombea taifa amani.