ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 6, 2015

WADAU WA VUNJO WAMTAKIA HAPPY BETHDAY KAMANDA WAO INNOCENT

Naibu kamanda wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi wilaya ya moshi vijijini ambae pia anatajwa kutakiwa kuwania ubunge jimbo la vunjo Innocent Melleck shirima leo 06/02/2015 ni siku yake ya kuzaliwa. Kwa niaba ya vijana na wananchi wa jimbo la vunjo tunamtakia afya njema na Mwenyezi Mungu ambariki kuwa na umri mkubwa mara dufu.Tupo nae katika kutekeleza ndoto za maisha yake mwaka huu 2015.

JESHI LA POLISI NCHINI LASHIRIKI KUZINDUA MAGARI MAPYA YA KAMPUNI YA ULINZI YA SECURITY GROUP JIJINIDAR LEO.

 Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la polisi nchini Kamishina wa Polisi Mussa Ally Mussa akiwa na mkuu wa jeshi la polisi mstaafu Philimon Mgaya akikata utepe wa kuashiria kuzindua magari mapya Zaidi ya ishirini ya kampuni ya ulinzi ya Security Group Africa ambayo yataanza kutumika katika kazi mbalimbali za kampuni hiyo hivi karibuni.Katikati yao ni mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Eric Sambu.
 Mwakilishi wa Mkuu wa jeshi la polisi nchini Kamishina wa Polisi Mussa Ally Mussa  akipokea msaada wa pikipiki mbili aina ya Boxer toka kwa mwenyekiti wa bodi wa kampuni ya Security Group Africa ambae pia ni mkuu wa  jeshi la polisi mstaafu Philimon Mgaya kwaajili ya kusaidia jeshi hilo katika oparasheni mbalimbali za kupambana na uhalifu,Katikati yao ni mkurugenzi mkuu wa kampuni ya SGA nchini  Eric Sambu.
 Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya SGA nchini  Eric Sambu akizungumza kwenye hafla ya kuzindua magari mapya Zaidi ya ishirini ya kampuni ya ulinzi ya Security Group Africa ambayo yataanza kutumika katika kazi mbalimbali za kampuni hiyo hivi karibuni.Hafla hiyo imefanyika katika ofisi za kampuni hiyo Mbezi Beach jijini Dar Es Salaam.
 Mwakilishi wa Mkuu wa jeshi la polisi nchini Kamishina wa Polisi Mussa Ally Mussa  akikagua gwaride maalum la kuashiria kuanza kwa shuguli ya kuzindua magari mapya Zaidi ya ishirini ya kampuni ya ulinzi ya Security Group Africa ambayo yataanza kutumika katika kazi mbalimbali za kampuni hiyo hivi karibuni.Kulia kwake ni mkuu wa kitengo cha mafunzo cha SGA bwana Rogers Lumwaji.
 Mwakilishi wa Mkuu wa jeshi la polisi nchini Kamishina wa Polisi Mussa Ally Mussa  akipeperusha bendera kuashiria kuanza kutumika kwa magari magari mapya Zaidi ya ishirini ya kampuni ya ulinzi ya Security Group Africa ambayo yataanza kutumika katika kazi mbalimbali za kampuni hiyo hivi karibuni.Katikati yao ni mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Eric Sambu.

SKYLIGHT BAND WAENDELEA KUTOA BURUDANI YA NGUVU JIJI DAR, NI IJUMAA HII TENA

Binti mwenye sauti ya kumtoa Nyoka pangoni, Ashura Kitenge akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita huku akipewa sapoti na Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 pamoja na Kisura mwingine wa Skylight Band anayefamika kwa jina la Baby.
Tukutane baadae tupunguze stress za wiki nzima kwa burudani iliyoenda shule na sehemu ya watu wastaarabu kama kawaida na mtonyo wetu ule ule getini.
Msanii wa Skylight Band Joniko akiendelea kutoa burudani huku vijana wa Skylight Band wakitimua vumbi jukwaani wakiongozwa na Sony Masamba ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar
Binti mwenye sauti ya kumtoa Nyoka pangoni, Ashura Kitenge akiimba kwa hisia kali mbele ya mashabiki wa Skylight Band(hawapo pichani) ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 akiimba uku akipewa support ya nguvu na Binti mwenye sauti ya kumtoa Nyoka pangoni, Ashura Kitenge( wa kwanza kushoto), Sam Mapenzi (wa pili kutoka kulia) pamoja na John Music ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar
Sony Masamba akiendelea kuimba masebene ya nguvu huku akipewa support na Majembe ya Skylight Band yaliyojimwaga kwenye stage
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 akiimba kwa hisia kali wakati akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar
Waimbaji wa Skylight Band yakijimwaga na sebene jukwaani kwenye show za bendi hiyo zinazofanyika kila Ijumaa ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.
Msanii wa Skylight Band John Music akitoa burudani ya nguvu ndani ya kiota cha Thai Village Ijumaa iliyopita.
Idrisa Drums akifanya yake.

Msanii wa Skylight Band Joniko (wa kwanza kushoto) akiendelea kutoa burudani akisaidiwa na John Music(wa kwanza kulia) pamoja na Ashura Kitenge pamoja na Baby.
Ulifika muda wa sugua sugua mpaka utakate ........ilikuwa noma sanaaaaa!!!!!
DSC_0141
DSC_0148
Mashabiki wa Skylight Band wakijiachia kwa raha zao ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.

WAHANDISI WA SEIKALI ZA MITAA KIJITAFAKALI ILI KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

 
NA PETER FABIAN, MWANZA.
WAHANDISI walioko katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, wametakiwa kujitafakari kwa kina ili kutekeleza majukumu yao yatakayosaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa jamii kutokana na miradi mingi kutumia gharama kubwa katika utekelezaji wake.
Akifungua mkutano mkuu wa mwaka waWahandisi wa Serikali za Mitaa jana jijini Mwanza, Mgeni rasmi katika mkutano huo, KatibuTawalawaMkoawaMwanza, Faizal Issa, hotuba yake iliyosomwa na mwakirishi wake, NdaloKulwijira, alisema kwamba wahandisi wazingatie taaluma yao katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa jamii.
“Taaluma ina umuhimu mkubwa kwa taifa na jamii, hivyo ni vyema mkatekeleza majukumu yenu kwa weledi mkubwa wakati wa kutekeleza maradi ya maendeleo inayotumia gharama kubwa ilikuwezesha kutoa huduma kwa jamii kwa muda mrefu na kwa ubora unaotakiwa,”alisema.
KwilwijiraalisemakuwaAssociatin of Local Government Enginners in Tanzania (ALGETA) ni Jumuiya ambayo kazi zake niza kitaalamu zaidi hivyo ni vyema mkajadiliana kwa kina  na kubadilishana uzoe na kuwa ma mfumo bora na  kutimiza wajibu wenu na dhamana mliyonayo katika taifa na halmashauri zenu ilikukabilia na changamoto za utekelezaji miradi mbalimbali ya jamii.
Kwilijira nimeeleza kwamba Wahandisi wanaoshiriki mkutano huu wote wanatoka Serikali za mitaa (TAMISEMI),ambao nimamizi wanaosimami utekelezaji wa miradi ya miundombinu inayotekelezwa na wananchi katika ngazi ya mamlaka za serikali za mitaa vikiwa ni vyombo vilivyo karibu na wananchi
“Taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali imekuwa ikionyesha mojawapo ya sababu za Halmashauri kupata Hati zisizoridhisha na chafu kutokana na miradi kutosimamiwa kikamilifu ikiwa ni i ile miradi ya maji, miundombinu ya majengo na barabara hali hii imeanza kudhibitiwa kila mwaka,”alisema.
Serikali inawataka watumishi wote ikiwemo wahandisi kuweka mikakati inayotekelezeka  na isiyokinzana na sheria na maadili ya utumishi ambapo serikali imejipanga kuwasaidia kadiri inavyowezekana ili kufanikisha azima yake ya Serikali  ya awamu ya nne ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.
“Nawaasa Wahandisi wote kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretalieti za Mikoa na Hata Wizara kuwatumikia wananchi kwa uadilifu wa hali ya juu kwa taratibu za maadili ya utumishi wa umma pamoja na kuwa na jukumu la kuhamasisha na kuwawezesha wananchi kujiletea maendeleo kwa ustawi wao binafs kwenye maeneo yao,”alisisitiza.
Awali Rais wa ALGETA Taifa, Mhandisi Ezekiel Kunyaranyara, kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano huo, alisema mkutano huo wa kikatiba wa Jumuiya hiyo utajadili “Utoaji Huduma Bora za Kihandisi Kwa Maendeleo ya Jamii” katika Sekta ya maji, barabara na majengo ikiwemo mitambo ya umeme.
Mhandisi Kunyaranyara, alisema kuwa mkutano huo ni halali kutokana na Jumuiya hiyo ya ALGETA kusajiliwa mwaka 2007 na kupata usajili Na 14878 na kuwa na wanachama 453 ambao ni wahandisi na wafundi wasanifu 531 ikiwa lengo kuu ni kuwaleta pamoja wataalamu wote wanaofanya kazi chini ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Sekretalieti za Mikoa na Wizara ya TAMISEMI.
“Mkutano huu umelenga pia kusaidia wanafunzi wasichana katika shule za sekondari kusoma masomo ya Sayansi kwa kutoa msaada wa vitabu, pia kutoa msaada wa madawati 100 katika shule mojawapo ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza na wajumbe kupata fursa ya kutembelea mradi wa barabara za Mawe iliyokamilika,”alisema.
Mkutano huo wa siku mbili pia utajadiliana jinsi ya kuongeza ushiriki wa watoto wa kike kupenda kusoma masomo ya Sayansi yatakayo pelekea wao kuwa wahandisi baaada ya kuhitimu ili kuongeza wahandisi wakike na kutekeleza majukumu ya kulijenga taifa bora lenye kasi ya maendeleo.

“WAKATI WA KUIBUKA NA USHINDI MNONO KAMPENI YA ‘TUTOKE NA SERENGETI’ NDIO HUU"

“YOUR CHANCE TO WIN BIG IN TUTOKE NA SERENGETI IS NOW”….SAYS SBL
Dar es Salaam, Tanzania: 04th February, 2015. Tanzania’s second largest brewing company has revealed that the ongoing Tutoke na Serengeti campaign is about to mark its end. As that is the case the company plans to end the campaign in style and make sure that more lucky winners stand a chance of walking away with various prizes that are still up for grabs.

Speaking to journalists at SBL’s main offices-Chang’ombe, Serengeti Premium Lager’s brand manager Mr. Rugambo Rodney mentioned some of the prizes that are still up for grabs as;- The Limo Bajaj, Free trip to Serengeti national park dubbed…“Mtoko wa mbugani”, Instant cash, free beers that can be redeemed instantly at an outlet and the 300Tsh beer discount.

“I’m very happy that the promotion has had a good response so far and as a company we are proud that we have rewarded various prizes to a good number of Tanzanians…. I’m glad that the rewards have had a positive impact in the lives of most of winners. I also know there are so many Tanzanians who would wish to visit Serengeti national park, own a Limo Bajaj or even walk away with instant cash.”
Rodney added that the time is now as the clock is now ticking faster and louder for  two weeks that are remaining on the calendar for customers to grab the awards.

He went ahead to remind customers that time is limited and to win these prizes is very simple all one has to do is buy a Serengeti Premium Lager the brand which sponsors the campaign and look under the crown where you will find unique codes to be sent to an SMS number 15317 and there one automatically enters into the draw while standing a chance of winning the above mentioned prizes.
SBL also confirmed to journalists that so far they have awarded 5 Limo Bajaj to various winners 2 from Kilimanjaro region, 1 from Morogoro and 2 others from Dar es Salaam. They have also rewarded free trips to the Serengeti national park for two, Tshs. 100,000/= weekly cash to more than 15 people and free beers to various winners during all this time. Statistics further confirmed that most of “Tutoke na Serengeti” winners came from upcountry concluding that the campaign has had a good response from all over the country.

The countrywide promotion was officially launched by SBL together with BPESA 3 months ago and the trend has been to reward consumers every week in the lucky draws conducted by SBL under the supervision of the Gaming Board of Tanzania. The secret behind winners of this promotion has been to send the codes to the number 15317 as much as possible so as to create higher chances of winning the Limo Bajaj and other prizes. However one has to be 18+ years in order to participate and only buy a Serengeti Premium Lager which is the beer that sponsors the campaign

FOR MORE INFORMATION:-

Please visit Serengeti Premium Lager’s Face book and Twitter pages.

Wednesday, February 4, 2015

NDEGE YA TAIWAN YAANGUKIA MTONI

Ndege inayoimilikiwa na Shirika la Ndege la Taiwan, la TransAsia imepata ajali na kuangukia kwenye mto katika mji mkuu, Taipei.
Vyombo vya habari vya Taiwan vimesema watu zaidi ya 50 walikuwa ndani ya ndege hiyo, wakati ajali ilipotokea na idadi kubwa ya watu wameripotiwa kujeruhiwa.
Shirika la Habari la Taiwan limeonesha picha ya ndege hiyo ikiwa imezama kwa kiasi kikubwa katika mto Keelung.
Chanzo cha ajali bado hakijajulikana.
Watu kadhaa wameokolewa na kupelekwa hospitali na wengine 10 bado wamenasa katika ndege hiyo.
Ndege hiyo ilikuwa ikiruka kutoka uwanja wa ndege wa Songdshan Taipei kuelekea uwanja wa ndege wa Kinmen nje ya Taiwan.
Picha ya ndege hiyo ikiwa imezama kwa kiasi kikubwa katika mto Keelung.
Mwezi Julai mwaka uliopita watu 48 walikufa baada ya ndege ya shirika hilo la TransAsia kupata ajali kutokana na hali mbaya ya hewa katika kisiwa cha Penghu.

WAHANDISI WAKUTANA KUJADILI MAFANIKIO, UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MEENDELEO NCHINI

RAIS wa Association of Local Government Engineers Tanzania (ALGETA) nchini, Mhandisi Ezekiel Kunyaranyara (Katikati) akizungumza leo na waandishi wa Habari (hapapo pichani), kuhusu kufanyika mkutano wao wa mwaka utakaofanyika kesho jijini Mwanza, kushoto ni Makamu wa Rais wa ALGETA, Mhandisi Gerald Matindi na kushoto ni Katibu Mkuu wa Jumuia hiyo, Mhandisi Lusekelo Mwakyami. 
NA PETER FABIAN,
GSENGO BLOG/MWANZA.
WAHANDISI 350 wa Halmashauri kutoka Mikoa 25 nchini wanachama wa Association of Local Government Engineers Tanzania (ALGETA) wanakutana kesho jijini Mwanza kwa siku mbili kujadili utoaji bora wa huduma kwa jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Mwanza, Rais wa ALGETA nchini, Mhandisi Ezekiel Kunyaranyara alisema kuwa mkutano huo wa mwaka wa wahandisi wanachama pia utajadili utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri zao za sekta ya maji, barabara na majengo.

Mhandisi Kunyaranyara alisema kuwa pia mkutano huo utajadili mfumo wa watumishi wa taaluma ya Uhandisi wa serikali wa Mitaa ili kuona kama lengo la kuwa na wahandisi wanne kila Halmashauri limefikiwa katika Idara ya Uhandisi ikiwemo wasaidizi katika Idara za maji, barabara na majengo.

“Mkutano huu utawashirikisha pia wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Bodi ya Usajili ya Wakandarasi na Bodi ya Wasanifu na Wakadiriaji wa Majengo ili kuwezesha kujadili na kusaidia miradi ya inayotekelezwa kwenye Halmashauri kutoharibika kwa muda mfupi baada ya kukamilika kwake pamoja na kuangalia mafanikio ya miaka 8 toka kuanzishwa kwake rasmi mwaka 2007,”alisema.

Rais, Kunyaranyara alieleza kuwa katika mkutano huo wajumbe watapata fursa ya kujadili kwa kina na kushauri juu ya utekelezaji wa miradi ya maji, majengo ikiwemo ujenzi wa Vyumba vya maabara, utumiaji wa mitambo ya umeme na vifaa vya kudrufu, kusaidia wanafunzi wa kike wa sekondari kusoma masomo ya Sayansi kusaidia vitabu.

“Kupitia mkutano huu utatoa msaada wa madawati 100 kwa shule moja ya Msingi zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, kutembelea ujenzi wa miradi ya barabara za mawe za halmashauri ya Jiji la Mwanza na mgeni rasmi atakayefungua mkutano wetu wa mwaka ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Faizal Issa,”alisema.

Naye Makamu wa Rais wa ALGETA, Mhandisi Gerald Matindi, alisema mkutano huo utahudhuliwa na Wahandisi wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Wilaya, Sekretarieti za Mikoa na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ambapo pia utekelezaji wa rasilimali watu na fedha zinavyofanikiwa.

“Mkutano huu utaishauri serikali kuhusu taratibu za manunuzi ya umma ambao umekuwa na changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kuchelewa kukamilika kwa wakati kutokana na sheria na taratibu za manunuzi ya umma kuwa katika Idara nyingine badala ya kuwa Uhandisi,”alisisitiza.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa ALGETA, Mhandisi Lusekelo Mwakyami, alisema kuwa mkutano huo utatoa mapendekezo kwa serikali ili kuanzisha mchakato wa ujenzi wa maabara za Kanda za Uhandisi kama ilivyo kwa Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) ili kuwezesha kufanyia vipimo sampuli na malighafi za ujenzi wa miradi ili kuwa na ubora na iweze kudumu kwa muda mrefu baada.

ametoa wito kwa wanachama wote kuhudhulia mkutano huo ambao umelenga kuboresha utoaji huduma na utekelezaji bora utakaoendana na thamani ya fedha katika miradi hiyo kwenye Halmashauri zao na kuhusisha wajumbe wa ERB na CRB kutawezesha kudhibiti kwa wenye fedha kufanya ujenzi wa majengo kwa kufuata taratibu na sheria ili kutoharibu sifa ya wahandisi.

BENKI YA I&M YAZINDUA HUDUMA YA KWANZA YA MFUMO WA KIELEKTRONIKI YA MASAA 25 KATIKA JENGO LA VIVA TOUR,POSTA JIJINI DAR

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha  (kushoto) akiongea na wadau wa benki hiyo hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa tawi  na mfumo mpya wa kielektroniki uliovumbuliwa na Smart Banking Solutions Ltd ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa pesa  sambamba na kupata huduma nyingine za kibenki kama kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mashine za kielektroniki masaa 24 ya siku.Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam, Kulia ni Meneja wa I&M wa tawi hilo Bi. Shabina Manji.
Baadhi ya wadau wa benki ya I&M na waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo Bw. Anurag Doreha , hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la kielektroniki , ambapo wateja wake wataweza kuweka na kutoa pesa kwa kutumia ATMs sambamba na huduma ya kubadili fedha za kigeni kwa masaa 24. Hafla hiyo ilifanyika katika tawi jipya la I&M, Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam. Benki hiyo imeungana na kampuni ya Smart Banking Solutions kuwaletea wateja wake huduma hii
Mkurugenzi Mkuu wa VIVA Tower Viral Manek, akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa tawi jipya la Benki ya I&M katika jengo hilo litakalotoa huduma masaa 24, kwa kuweka na kutoa fedha na kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mfumo mpya wa mashine za kieletroniki (ATMs). Kushoto ni mkurugenzi mkuu wa benki hiyo, Bw. Anurag Doreha, Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha (katikati) akifafanua jambo baada ya uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo kufanyika katika jengo la Viva Tower ambapo huduma za kuweka, kutoa na kubadilisha fedha za kigeni zitakua zikifanyika masaa 24 kutumia mashine za kielektroniki(ATMs) kulia ni Mkurugenzi mkuu wa VIVA Tower Viral Manek na kushoto ni Meneja Masoko wa Smart Banking Solutions Limited, Salil Abbas Sadik. Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi mkuu wa VIVA Tower Viral Manek, akionesha kwa vitendo jinsi ya kuweka fedha katika moja ya mashine za kielektroniki ndani ya tawi jipya lililozinduliwa la benki ya I&M ikishirikiana na Smart Banking Solutions-Viva Tower-Posta jijini Dar es salaam ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa fedha masaa 24 sambamba na kupata huduma ya kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mashine za kielektroniki(ATMs).
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha akiwaonyesha waandishi wa habari moja ya mashine inayotumika kubadili fedha za kigeni, baada ya kuzindua tawi jipya la benki hiyo maalum kwa shughuli za kuweka na kutoa fedha kwa kutumia mfumo mpya wa kielektroniki kupitia mashine za (ATMs). Hafla hiyo ilifanyika katika jengo la Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam ambapo benki hiyo imeshirikiana na kampuni ya Smart Banking Solutions Ltd.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha akionyesha mfano wa kutoa fedha katika moja ya mashine inayotumika kubadili fedha za kigeni. Mare baada ya kuzindua tawi na mfumo mpya ulioanzishwa na Smart Banking Solutions wa kuweka na kutoa fedha kupitia ATMs sambamba na kubadili fedha za kigeni ambapo mteja atapata huduma hii ndani ya masaa 24 ya siku. Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar.
Meneja Masoko wa Smart Banking Solutions Limited  Bw. Salil Abbas Sadik akiwaeleza waandishi wa habari kwa undani jinsi mfumo huo  wa kielektroniki unavyofanya kazi ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa fedha kupitia mashine za (ATMs) sambamba na kubadili fedha za kigeni masaa 24. Smart Banking solutions Ltd ndio waanzilishi wa teknolojia hiyo ambayo bado haijatumiwa na benki nyingine yeyote. Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar.
Meneja Masoko wa Smart Solution limited, Salil Abbas Sadik. Akiongea  na wadau wa Benki ya I & M hawapo pichani , wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo lililo katika Jengo la Viva Tower ambapo huduma zitatolewa masaa 24, ikiwemo kutoa ,kuchukua na kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mashine za kisasa za kielektroniki za ATM, Uzinduzi huo ulifanyika katika jengo hilo la Viva Tower Jijini Dar es Salaam

TIC YAKUTANA NA UJUMBE WA WAFANYABIASHARA KUTOKA NCHINI UJERUMANI

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (wa pili kushoto) akizungumza katika mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo hicho,jijini Dar es salaam.Ujumbe huo unaongozwa na Waziri wa Masuala ya Kiuchumi na Nishati wa nchini Ujerumani,Mh. Matthias Machnig (wa pili kulia). Picha zote na Othman Michuzi.
Mratibu wa Uwekezaji wa Kimataifa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Zacharia Kingu akifafanua jambo wakati akiwasilisha taarifa ya uwekezaji katika maeneo mbali mbali nchini wakati wa mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo hicho,jijini Dar es salaam.
Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani pamoja uongozi wa TIC ukifatikia kwa makini taarifa ya uwekezaji iliyokuwa ikitolewa na Mratibu wa Uwekezaji wa Kimataifa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Zacharia Kingu (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (katikati) akitoa ufafanuzi wa maswala mbali mbali ya uwekezaji kwa ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani waliotembelea kituo hicho jana jioni,jijini Dar es salaam.
Kiongozi wa Msafara wa Wafanyabiara hao ambaye ni Waziri wa Masuala ya Kiuchumi na Nishati wa nchini Ujerumani,Mh. Matthias Machnig akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki. 
Meneja wa Kitengo cha Uratibu Miradi ya Ubia (Sekta ya Umma na Binafsi) wa TIC,Said Amir akitoa ufafanuzi juu ya maswala ya ubia katika miradi,wakati wa mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo hicho,jijini Dar es salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Ushirika wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Revocatus Arbogust akichangia jambo katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (katikati) akifafanua jambo katika mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo hicho,jijini Dar es salaam.
Kiongozi wa Msafara wa Wafanyabiara hao ambaye ni Waziri wa Masuala ya Kiuchumi na Nishati wa nchini Ujerumani,Mh. Matthias Machnig akizungumza na mmoja wa wafanyabiashara aliofatana nao.
Sehemu ya Wafanyabiashara hao wakifatilia kwa makini taarifa ya uwekezaji.
Sehemu ya Ujumbe wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ukifatilia kwa makini mkutano huo.
Sehemu ya Ujumbe wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ukifatilia kwa makini mkutano huo.
Sehemu ya Ujumbe wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ukifatilia kwa makini mkutano huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (wa pili kushoto) akiongea na ujumbe huo wakati akiwaonyesha moja ya Jengo lilalotumiwa Kituo hicho lililojengwa na Wajerumani.