ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 9, 2015

SABABISHA MAPINDUZI YA UCHUMI NA POSO KUPITIA MWONGOZO NA KUWA MTAYARISHAJI KWANZA

King Majuto aka Mzee Majuto akiwa ni mmoja wa wajumbe wa POSO (Point of Servise Office) Ofisi ya Huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, akiwasilisha uzoefu wake wa kupambana na changamoto za ajira na kukuza kipato kwa baadhi ya wanahabari waliohudhuria Semina ya Siku moja iliyofanyika katika ukumbi wa G&G jijini Mwanza.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Bega kwa Bega Microfinance Co. Ltd BKB Bw. Albert P. Girenga akitoa taarifa kuhusu kampeni ya Sababisha Mapinduzi ya Uchumi na POSO kupitia Mwongozo wa kuwa Mtayarishaji kwanza.
Bwana Girenga amesema kuwa huduma wanayoitoa ni jitihada ya makusudi ya kuleta Mapinduzi makubwa ya Uchumi nchini Tanzania, ikiwa na dhana yenye fikra za kina na taswira pana ya mustakabali wa Watanzania kwa lengo la kumkomboa kiadilifu kila raia na vizazi vyake kutoka katika umasikini.

"Mafanikio ya mapinduzi haya yanategemea mshikamano wa walengwa, tunatumaini yatachangia kwa ujumla wamapinduzi haya na kuwafungulia jia ya kushiriki, wale watakaohamasika"

"Sababisha Mapinduzi ya Uchumi na POSO" ni kampeni ya kitaifa ya kufikisha kwa wananchi fursa za uwekezaji na uwezeshaji silisowekwa na sera hii kwa wananchi ili wazitumie kujitajirisha kiadilifu.

Kampeni hii inakusudia kujenga uelewa wa Watanzania walio wengi ili kushiriki kikamilifu katika ujenzi, umiliki, usimamizi na uendelezaji wa mitaji, vitegauchumi, soko, biashara na ajira.

Kupitia Kampeni hii kila Mtanzania atawezeshwa kuwa Mtajirishaji anayefanikisha ujenzi wa Nguvukazi Bora inayowajibika kutoa huduma, kuzalisha na kusambaza bidhaa bora zinazohimili ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi.
Kwa kifupi, Mtajirishaji ni mtu mwadilifu, mwenye werevu wa kiwangocha juu cha kutumia mazingira yanayomzunguka na ya utandawazi kufungamana  katika ubia unaofanikisha uwekezaji unaoibua na kuendeleza Ubunifu, uvumbuzi na Ujuzi (UUU)unaobadili Wazo, taaluma na Rasilimali kuwa Huduma, Bidhaa na Mali Bora zinazouzika kwa Faida inayotengeneza Hazina ya kutajirisha vizazi vyote.
Kampeni hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa ajira zinazowezesha wananchikufungamana na kujitajirisha kiadilifu, chini ya MILIKI mfumo wa UTAJIRISHAJI, unaoinua uwezo wa Watanzania, wa kubuni, kuanzisha, kuendeleza na kusimamia vitegauchumi nabiashara, kujenga na kumiliki mitaji ya uwekezaji, pamoja na kuhimili ushindani wa soko kwa kutumia rasilimali chache kati ya nyingi zinazotuzunguka.
Wabia wakuu katika utekelezaji wa mpango huu nikampunizilizoanzishwa na wananchi chini ya ushirikiano wa GODTEC (T) CO. LTD na Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, utamaduni na Michezo.
Meza ya wadau wa SUSO.
Wanahabari washiriki wa mkutano.








YAYA TOURE NDIYE MCHEZAJI BORA

KIUNGO wa timu ya Manchester City Yaya Toure amekuwa mchezaji wa kwanza kutajwa na shirikisho la soka barani Afrika kuwa mchezaji bora wa mwaka kwa mwaka wanne mfululizo.
Toure ana umri wa miaka 31,aliteuliwa baada ya kucheza kwa kujitoa na kuleta ushindi katika Premier League na League Cup, na pia alijitoa kuisaidia Ivory Coast kuingia katika kombe la mataifa ya Africa yatakayo fanyika baadaye mwaka huu.
Toure amewapiku mshambuliaji kutoka Gabon, Pierre Emerick Aubameyang na golikipa mnigeria Vicent Enyeama.Toure pia alikwaa tuzo ya FIfa ya Ballon D'Or mwezi wa kumi mwaka wa jana..

Thursday, January 8, 2015

YANGA OUT KOMBE LA MAPINDUZI


NA SALEH JEMBE
YANGA imeng'oka katika michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kufungwa bao 1-0 na JKU.

Muuaji wa Yanga alikuwa Amour Mohammed ambaye alifunga bao katika dakika ya 72 na kuwapa Yanga wakati mzuri wa kusawazisha bila ya mafanikio.

JKU inayomilikiwa na Jeshi la Zanzibar imefanikiwa kuing'oa Yanga kwa bao hilo moja katika mechi kali na ya kuvutia kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Kutokana na ushindi huo, sasa JKU itacheza nusu fainali dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo iliing'oa Azam FC leo mchana.

Yanga ilipoteza nafasi kadhaa za kufunga katika kipindi cha kwanza.

Lakini JKU walionekana kuwa tofauti na kucheza soka la kuvutia tokea mwanzo wa kipindi cha kwanza huku wakichezaji wake wakionana kwa pasi za uhakika zilizoonyesha kuna kitu wanatafuta.

MAMBO YA BURUDANI ZA JEMBE BEACH MWANZA.

Wanamuziki wa JJ Band January (kulia) ambaye ni kiongozi akipiga show ya majibizano na Charz ambaye usajili wake rasmi kutambulishwa kesho katika ukumbi huu wa Jembe Beach, Bata Lounge jijini Mwanza.
Charz hapa aliongoza mmoja ya nyimbo.
This is JJ Band.
Guitallist.
Vijana wa JJ Band.
Pamekolea.
Hatariii...
Selebuka.
Poze na style.
Utambulisho kwa mara ya kwanza ikiwa ni jukwaa ambalo lilikuwa siyo,  rasmi haya ni wachache wakuenda story  watu ambao watafurux.
Dunda eeee


BILL GATES ANYWA MAJI YA KINYESI


Mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates amekunywa maji yaliotengenezwa kutokana na kinyesi cha binaadamu kama maonyesho ya teknolojia mpya itakayoweza kutoa maji safi katika mataifa yanayoendelea.
Mwanzilishi huyo wa Microsoft amesema kuwa ataisambaza mitambo ya teknolojia hiyo mpya kote duniani baada ya kuifanyia majaribio mwishoni mwa mwaka huu.
Teknolojia hiyo imeungwa mkono na shirika la WaterAid ambalo limesema kuwa itasaidia sana katika maeneo ya miji.
Kulingana na shirika hilo la hisani takriban watu millioni 748 hawana maji safi ya kunywa.
katika kanda ya video iliyowekwa katika blogu yake,Bwana Bill Gates alishuhudia kinyesi cha Binaadamu kikiingizwa katika mtambo huo kabla ya kunywa maji yaliokuwa yakitoka kutoka kwa kikombe.
''Maji hayo ni mazuri sana ikilinganishwa na maji yoyote yale niliokunywa,na baada ya kusomea teknolojia hii nitayanywa kila siku.
Maji haya ni salama kabisa'',aliandika katika blogu yake.Kulingana na mtengenezaji wa mtambo huo Peter Janicki,maji taka hayo huchemshwa kabla ya mvuke wa maji hayo kutengwa na taka ngumu.
Taka hizo ngumu baadaye huwekwa katika moto na kutoa mvuke unaoendesha mashine zinazotoa nguvu za umeme kwa mtambo huo na pia kwa wakazi wa eneo hilo.
Maji hayo baadaye hutiwa ndani ya mtambo wa kusafisha maji ili kutoa maji safi ya kunywa.
''lakini kwa nini mtu awe na wazo la kubadilisha uchafu kuwa maji ya kunywa na umeme'',aliuliza Gates.
Jibu aliloandika ni kwamba kwa sababu magonjwa yanayosababishwa na mazingira machafu huwaua watoto 700,000 kila mwaka na huwakinga wengine wengi dhidi ya kuathirika kiakili na kimwili. CHANZO BBC.

"I ain't" By Beez Boyz (Official Music Video)

Here is a brand new video from the hit maker Beez Boyz for the song " I AIN'T" 
Directed by YOUNG PDK at PDK FILMS STUDIOS
© PDK ENTERTAINMENT 

MADA MAUGO NA KALAMA NYILAWILA WASAIDI KUZIPIGA MARCH 8 P.T.A SABASABA

Mabondia Mada Maugo kushoto na Kalama Nyilawila wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika March 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba.
Katibu mkuu wa chama cha ngumi za kulipwa nchini Antoni Rutta katikati akiwainua mikono juu mabondia Mada Maugo na Kalama Nyilawila wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika march 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba. 

Mabondia Mada Maugo kushoto na Kalama Nyilawila wakitunishiana misuli wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika March 8 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba

mabondia wakiwa katika picha ya pamoja kushoton ni Emilio Norfat,Nassibu Ramaradhani,Mohamed Matumla na Amosi Mwamakula.
Picha na SUPER D BOXING NEWS

AIRTEL KUZINDUA UNI255 JUMAMOSI HII

Afisa Masoko wa Airtel Henrick Bruno akionyesha moja kati ya vocha za Airtel UNI255 maalum kwa vyuo vikuu nchini tayari kwa uzinduzi jumamosi hii.

 Airtel kuzindua Airtel UNI 255 J-mosi maalum kwa vyuo vikuu Dar es salaam

·                Ney wa Mitego, Roma Mkatoliki, Shilole kupamba uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel UDSM
                                                                                                             
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imebainisha kuwa mwishoni mwa wiki hii itazindua rasmi huduma mpya maalum kwaajili ya kutoa huduma nafuu za mawasiliano kwa wanafunzi walioko vyuoni katika chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM ambapo hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo inayojulikana kama Airtel UNI 255 kwa vyuo vikuu vilivyopo Dar es salaam itafanyika katika viwanja vya Mabibo hostel

Jackson Mbando.
Akiongea kuhusiana na uzinduzi wa huduma hiyo Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando amesema “Airtel Uni 255 ni huduma pekee yakibunifu toka Airtel Maalum kwa wanafunzi wa vyuo yenye kuwapa unafuu wa kuwasiliana wawapo chuoni, sasa wanafunzi wote wa chuo wanapotaka kupata nyongeza ya vile wanavyosoma kwenye mtandao huduma  hiii  ndio jibu sahihi kwao kutokana na unafuu wake kwenye inteneti, kupiga simu na hata sms. Huduma hii tayari tumeshaizindua kwa vyuo vikuu vingine vya Dodoma, Mbeya, Iringa, Mwanza na imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa watumiaji wakiwemo wanafunzi na wale wote wanaotumia huduma hii maeneo ya vyuo”

“Airtel tumeona ni vyema tuizindua hapa katika vyuo vya Dar es salaam wiki hii siku ya Jumamosi pale mabibo hostel ambapo mbali na uzinduzi kutakuwa na tamasha kubwa litakalopambwa na watoa burudani nguli akiwemo Ney wa Mitego, Roma Mkatoliki, Shilole pmaoja na DJ maarufu jiji Dj Zero aliongeza kusema Mmbando

Nae meneja wa huduma hiyo ya UNI 255 Anethy Muga alisema “Airtel tumeoana hii ni huduma maalum kwa wanafunzi na ndio maana tukaona ni vyema kuizindulia katika Hostel zao pale mabibo ambapo tunaamini wanafunzi wengi wa chuo kikuu hapa jijini wanaifahamu na wanaishi mabibo hivyo wanakaribishwa katika uzinduzi huo ambapo kiingilo chake ni BURE”

Burudani zitakuwa zakutosha kupitia Airtel UNI 255  siku hiyo.

Kampuni ya simu za mkononi ya airtel ilianzisha huduma ya UNI255 ili kuendana sambamba na mkakati wao wa kusaidia vyuo vikuu nchini kutumia ipasavyo huduma za mtandao ili kuboresha sekta ya elimu kwa lengo la kusaidia wateja wake walioko vyuoni kufikia malengo yao.

Wednesday, January 7, 2015

MAGUFULI AAGIZA KUFUNGWA MFUMO MPYA WA KIELEKTRONIKI KATIKA VIVUKO VYOTE NCHINI


Na JOHN DOTTO  Mwanza
 
WAZIRI wa Ujenzi Dk. John Magufuli ameagiza kufungwa kwa mfumo mpya wa kielektroniki katika vivuko vyote nchini ili kukabiana na wajanja wachache wanahujumu mapato katika vivuko hivyo.
 
Mbali ya hilo, ameagiza kufanywa kwa utaratibu utakaowezesha huduma katika vivuko zinatolewa kwa saa 24 ili kukidhi mahitaji ya wananchi.
 
Dk. Magufuli alitoa maagizo hayo jana katika uzinduzi wa mfumo mpya wa kielektroniki katika kivuko cha Kigongo -busisi mkoani hapa uliowekwa na Kampuni ya Africom Tanzania.
 
"Tulianze pale Kigamboni na tukaona mafanikio, tulipokuja hapa (Kigongo) tukaboresha na mafanikio yameonekana kwa kiasi kikubwa. Vivuko vyote sasa vifungwe mfumo mpya wa kielektroniki...vivuko vyote nchini," aliagiza Magufuli.
 
Alisema mfumo huo una faida kubwa ikiwemo kudhibiti upotevu wa mapato ambapo katika kivuko cha kigongo - Busisi alisema mapato yameongezeka kwa takribani asilimia 40 baada ya kufungwa kwa mfumo huo.
 
Hata hivyo, Dk. Magufuli alikataa kutaja ni kwa shilingi ngapi mapato hayo yameongezeka kwa hofu kuwa watu wenye dhmira mbaya wakisikia wanaweza kwenda na kufanya uhalifu.
 
Pia, aliagiza Kivuko kwa Kigamboni nacho kiboreshwe mfumo wake kama ilivyokuwa kwa Kigongo - Busisi. 
 
Waziri huyo wa Ujenzi, alisema kutokana na mafanikio yanayopatikana katika kudhibiti upotevu wa mapato na kurahisisha huduma kwa wananchi, wafanyakazi husika kwa maana ya wale wa TEMESA maslahi yao yanapaswa kuangaliwa upya na kuboreshwa.
 
"Kama mapato ni mazuri, wafanyakazi nao walipwe vizuri, wasikae kimasikini kwani wanapaswa kuona mwaka 2015 ni ukombozi katika maisha yao.
 
Alisema serikali chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete imefanikiwa kujenga madaraja yote makubwa nchini ambapo kwa sasa kuna madaraja 4880 nchini na kuwa wakati inapata uhuru kulikuwa na madaraja mawili ambayo yalikuwa ya kuvutwa.
 
 
Mfumo wa kielektroniki katika vivuko vya Kigamboni na Kigongo Busisi ulifungwa na Kampuni ya Africom Tanzania ambaye Mkurugenzi Mtendaji wake Juma Rajabu alisema watahakikisha wanafunga mifumo ambayo itadhibiti upotevu wa mapato na kurahisisha huduma kwa wananchi ambao ndiyo watumiaji.

MKAZI WA DAR AIBUKA NA USHINDI MNONO KWENYE KAMPENI YA TUTOKE NA SERENGETI

Meneja bia chapa Serengeti Primium Lager, Rugambo Rodney akiongea kwa njia ya simu na mshindi wa Limo bajaj na fedha taslim Tsh 100,000/= katika Shindano la Tutoke na Serengeti linaloendeshwa na kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kushirikiana na BPESA kushoto ni  msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Bw. Bakari Majjid , ambapo Godfrey Longino Mpiruka mkazi wa Dar ameibuka na ushindi mnono. Droo hiyo ilifanyika makao makuu ya Serengeti-Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
Meneja bia chapa Serengeti Primium Lager, Rugambo Rodney akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kuchezesha droo ya Shindano la Tutoke na Serengeti linaloendeshwa na kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kushirikiana na BPESA. Kushoto ni  msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Bw. Bakari Majjid na kulia ni Meneja Vipoozeo na mwonekano, Baraka Mandara,  ambapo Bw.Godfrey Longino Mpiruka mkazi wa Bunyokwa, Segerea Dar es salaam ameibuka mshindi wa Limo Bajaj yenye uwezo wa kubeba watu 7 na fedha taslim Tsh. 100,000/=. Droo hiyo ilifanyika makao makuu ya Serengeti-Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
Meneja bia chapa Serengeti Primium Lager, Rugambo Rodney akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kuchezesha droo ya Shindano la Tutoke na Serengeti linaloendeshwa na kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kushirikiana na BPESA
RE: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MKAZI WA DAR AIBUKA NA USHINDI MNONO KWENYE KAMPENI YA TUTOKE NA SERENGETI
7th Dec 2015, Dar-Es-Salaam
Mwaka 2015 umeanza vizuri kwa Bwana Godfrey Longino Mpiruka  baada ya kutangazwa mshindi wa nne wa bajaji mpya aina ya Limo sambamba na fedha taslim Tsh. 100,000/= zinazotolewa kila wiki katika kampeni  inayoendelea ya  “Tutoke na Serengeti” .

Godfrey mwenye umri wa miaka 47 na mkazi wa Bunyokwa Segerea-Dar es salaam ameibuka na ushindi huo mnono baada ya kuwashinda washiriki kutoka mikoa ya Moshi na Morogoro ambayo mpaka sasa  imeongoza kwa kutoa washindi mbalimbali katika kampeni hii ya miezi mitatu inayodhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Serengeti Premium lager kwa kushirikiana na BPESA.
“Wakati nashiriki katika kampeni hii, lengo langu lilikuwa ni kushinda shilingi 100,000/= bila kujua kwamba ushiriki wangu ungenipelekea kushinda pia Limo Bajaj mpya..ninashukuru sana Serengeti” alisema Bw.Godfrey kwa njia ya simu mara baada ya kuibuka mshindi wa nne wa Limo Bajaj. Godfrey aliongeza kwamba, Bajaji hiyo yenye uwezo wa kubeba watu 7 ambayo imeigharimu SBL kiasi cha Tsh. 9,000,000/= itamsaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza kipato katika maisha yake na pia kukabiliana na changamoto mbalimbali za kifedha ambazo amekua akikabiliana nazo.

Baadhi ya washindi waliofaidika na kampeni hii na kupata zawadi zao ni pamoja na: - Bi. Rukia Almasi ambaye ni mama wa nyumbani na mkazi wa Kihonda aliyeshinda bajaji ya kwanza, wakati  Peter Emmanuel, dereva wa  bodaboda aliibuka mshindi wa pili, na Isaack Edward Maro mwalimu wa shule ya awali kutoka mkoa wa Kilimanjaro aliibuka mshindi wa tatu. Kwa upande mwingine, Hassan Mfaume na Deogratias Masenga kwa pamoja walishinda safari ya siku mbili na wenza wao ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Serengeti National park na zaidi ya washindi saba walijinyakulia kitita cha shilingi  100,000/= kila mmoja zilizokuwa zikitolewa kila wiki baada ya droo.

Akiongea na waandishi wa habari Bw. Rugambo Rodney, Meneja wa bia chapa Serengeti Premium Lager alisema….“ Promosheni ya Tutoke na Serengeti bado inaendelea na kama ilivyo ada, SBL kwa kushirikiana na BPESA wanaendelea kuwazawadia wateja wao zawadi mbalimbali zikiwemo Limo Bajaj, safari za bure za kutembelea mbuga za wanyama, fedha za papo kwa hapo kiasi cha shilingi  100,000/= kila wiki, punguzo la bei la shilingi 300/= katika bei halisi ya bia aina ya Serengeti, pamoja na bia za bure ambazo zinatolewa nchi nzima.” Rodney aliendelea kueleza kuwa promosheni imeendelea kufanya vizuri tangu kuanza kwake kwa muda wa miezi miwili iliyopita na hivyo basi uongozi umeona ni vema kuongeza mwezi mmoja wa promosheni ili wateja waendelee kujinyakulia zawadi mbalimbali.

Promosheni hii ya nchi nzima ilizinduliwa na SBL pamoja na B-Pesa miezi miwili iliyopita ikiwa na lengo la kuwazawadia wateja wake katika kila droo itakayokuwa ikifanywa kila wiki na SBL chini ya uangalizi wa bodi ya michezo ya bahati nasibu Tanzania.

Ili kushiriki katika promosheni hii, mteja anatakiwa awe na umri wa zaidi ya miaka 18, na anunue bia ya Serengeti Premium Lager na kuangalia chini ya kizibo ambapo atakuta namba zinazotakiwa kutumwa  kwa njia ya SMS kwenda 15317. Kadiri mteja anavyoshiriki zaidi ndivyo anavyojiweka katika nafasi nzuri ya kushinda zaidi.

Tuesday, January 6, 2015

SOKA LATINGA GEREZANI.

Diwani wa Kata ya Nyamagana Jimbo la Nyamagana, Bikhu Kotecha (wa pili kushoto) akikabidhi mipira 10 na Kombe dogo kwa Mkuu wa Gereza la Butimba, ACP Jail Mwangunda ili vitumike katika michuano ya soka kwa wafungwa na askari wa Gereza Kuu la Butimba lililopo Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza
 Na Albert G Sengo, Mwanza.
DIWANI wa Kata ya Nyamagana Jimbo la Nyamagana, Bikhu Kotecha leo amekabidhi mipira 10 na Kombe dogo kwa wafungwa na askari wa Gereza Kuu la Butimba lililopo Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.

Hatua hiyo ya Diwani Kotecha (CCM) kukabidhi mipira kunafatia ombi la viongozi wa wafungwa na mahabusu kupitia uongozi wa Gereza la Butimba ili kuwasaidia kuburudika, kuimalisha afya zao kupitia michezo na kudumisha mahusiano baina ya mahabusu na wafungwa na kuendeleza vipaji na ushabiki wa timu za Simba na Yanga na vilabu vingine vikiwemo vya Ulaya.
Picha ya pamoja.
Kotecha akikabidhi alisema ametekeleza ahadi aliyoitoa mwaka jana alipowatembelea wafungwa hao katika ziara aliyoifanya akiwa na baadhi ya viongozi wengine wa kiserikali hivyo ametekeleza ikiwa ni sehemu ya jamii ambayo inawajibu ya kushiriki na kuendeleza vipaji japokuwa wako chini ya utaratibu maalumu wa Gereza, Pia kutokana na mahusiano ambayo Kata yake imekuwa ikisaidiwa na wafungwa katika ujenzi wa miradi ya kijamii ikiwemo Sekondari ya Kata hiyo.

Mmoja wa viongozi wa wafungwa na mahabusu waliopo katika gereza hilo alimshukuru Diwani Kotecha kwa kuwakumbuka na kutekeleza ombi lao , kwa kueleza kuwa pamoja na kuwa gerezani kwa makosa mbalimbali bado ni sehemu ya jamii na inayohitaji kubadirika na kupata burudani ikiwemo ya soka na kulinda vipaji vyao kupitia timu tisa zilizopo ndani ya Gereza hilo zikiundwa na mahabusu na wafungwa.

Shukurani.
Naye Mkuu wa Gereza la Butimba, ACP Jail Mwangunda , amepongeza utekelezaji wa ombi la watu ambao ni sehemu ya jamii wanaotumikia adhabu ya makosa mbalimbali lakini pia uamuzi wa Diwani Kotecha wa kuthubutu umeonyesha ungwana na upendo wa hali ya juu na kuonyesha mahusiano yake na uongozi wa Gereza hilo.

Msaada huo wa mipira kumi uliotolewa na kukabidhiwa na Diwani Kotecha kwa uongozi wa Gereza, wafungwa na mahabusu,  ambapo  viongozi wa wafungwa na mahabusu wamekabidhiwa mipira sita na kombe dogo watakaloshindania, timu ya askari wa Gereza hilo mipira miwili na timu ya askari ya wanawake mipira miwili ya netiboli.

SAFARI LAGER WEZESHWA

Meneja wa Bia ya Safari Lager, Edith Bebwa(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani ) wakati  kutangaza upatikanaji wa fomu za kuomba ruzuku za wajasiliama kwa msimu wan ne wa program ya Safari Lager Wezeshwa  uliofanyika Dar es Salaam jana.Kulia ni Jaji wa Programu hiyo, Joseph Migunda.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Toleo la Leo

SAFARI LAGER YATANGAZA RASMI UPATIKANAJI WA FOMU ZA PROGAMU YA SAFARI LAGER WEZESHWA MSIMU IV.
Dar es Salaam, Jumanne  Januari 6, 2015: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza rasmi upatikanaji wa fomu za programu yake ya Safari  Lager Wezeshwa kwa msimu wa nne kwa wajasiriamali wadogo wadogo  na wa kati  Nchini.  

Akizungumza  na waandishi wa habari, Meneja wa bia ya Safari Lager Bi. Edith Bebwa  alifafanuwa ya kwamba “ Fomu za ushiriki zitapatikana kwenye mabohari ya TBL, Mawakali wa kusambaza bia, kwenye mtandao wa www.wezeshwa.co.tz . Fomu hizo zichukuliwe, zijazwe na kurejeshwa kwenye vituo vilivyotajwa hapo juu au kwa njia ya posta kwa sanduku la posta (Safari Lager Wezeshwa msimu wa nne,Tbl Dar es Salaam,P.o Box 9393 DSM).
Alisema Bi Edith, hii ni hazina tosha kwa wajasiriamali wadogowadogo nchini kwani itarahisisha kazi  kwa kuwepo na vitendea kazi bila ya kutumia nguvu nyingi”.
Programu hii ni msimu wa nne   tangu kuanzishwa kwake na  imeleta mafanikio makubwa kwa wajasiriamali waliopata uthubutu wa kujaribu kujiunga na hatimae kuongeza uchumi wa nchi.

Programu hii itafanyika takribani mikoa yote ambapo itawapa fursa wajasiriamali wa aina zote bila kujali fani,kabila wala jinsia  kujaza fomu kwa usahihi na kamilifu   kisha kuzirudisha mahala husika na baadae waliokidhi nafasi zinazohitajika kuchaguliwa kisha kupewa mafunzo mafupi  pamoja na kukabidhiwa ruzuku  zao alisema Bi Edith.

Meneja wa bia ya Safari Lager, Edith Bebwa alimaliza kwa kutaja tarehe ya mwisho wa kurejesha fomu kuwa ni 20,Februari 2015 hivyo wajasiliamali wanapochukua fomu wakumbuke pia muda wa kuzirejesha walipozitoa.

Nae kiongozi wa wataalamu wa ushauri wa biashara kutoka kampuni ya TAPBDS, Bwana Joseph Migunda alisema kuwa  “Zoezi hili linahusisha wataalamu wenye uwezo na uzoefu mkubwa katika kushauri na kusaidia ukuzaji wa sekta ya biashara ndogo na kubwa. Hivyo aliomba wajasiriamali wote kuitumia fursa hii kushiriki kwa kuzingatia vigezo vilivyoainishwa kwenye fomu ya ushiriki. Wenye nia ya kufika mbali kibiashara na wenye  malengo ya kuisaidia jamii inayowazunguka wasisite kuchangamkia fursa hii”.

ALIBINO ANASAKWA MWANZA , WATU 15 MBARONI

Waandishi wa habari Sheila Sesi na Grace Chilongola walipokuwa wakifanya mahojiano na mama yake Pendo.
Wananchi wa kijiji cha Ndami wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo Mbele kabisa kwenye kusanyiko.
 Walinzi wa jadi wanaojulikana kama 'Sungusungu' wakimsikiliza mkuu wa mkoa.
Bw. Alfred Kapole ni Mwenyekiti wa albino mkoa wa Mwanza na hapa akizungumza na kusanyiko hilo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola alipokuwa akitoa taarifa ya uchunguzi hadi sasa.

Nyumbani kwao Pendo, Mwenyekiti wa albino mkoa wa Mwanza Alfredy na Mwenyekiti wa  CHAWATA mkoa wa mwanza wakiongea na mama Pendo Emmanuel.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Serikali mkoani Mwanza imesema hakuna kulala hadi mtoto Pendo Emmanuel (Albino) apatikane kufatia tukio la kutekwa na watu wasio julikana toka tarehe 27.12.2014 katika kijiji cha Ndami, Tarafa ya Mwamashimba Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza na kisha kutoweka naye kwenda kusiko julikana hadi sasa.

MKUU WA MKOA.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo, alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo na kuwahusisha wananchi wakijiji hicho pamoja na uongozi wa Wilaya na Mkoa huku akitaka kujua hatua iliyofikiwa na wana nchi hao katika kuwabaini walifanya unyama huo.

Mtoto Pendo alitekwa na watu wasiojulikana mnamo usiku wa tarehe 27.12.2014 majira ya saa nne usiku akiwa amelala na wazazi wake huko Nyumbani kwao na kisha watekaji kutoweka naye na kwenda kusiko julikana hadi sasa, huku taarifa za Polisi zikionesha jumla ya watu kumi na watano (15), wakiendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Akihutubia wananchi wa kijiji hicho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, alisema ni tukio la kusikitisha kwani toka mwaka 2007 hakuna tukio la namna hiyo lililo wahi kutokea katika Wilaya hiyo na tukio la mwisho lililotokea lilimkumba mwananchi wa Wilaya hiyo aliyekuwa amesafiri kwenda Mkoani Shinyanga kwa shughuli zake.

Amesema kiburi walicho nacho watekaji hakiwezi kuwa nje ya mipaka ya kijiji hicho cha Ndami bali mpango mzima unajulikana kwa wenyeji na ndio maana ilikuwa rahisi kufanya unyama huo “Kiburi cha watekaji kimo humu humu haiwezekani mtu kutoka mbali aje atekeleze tukio hapa kijijini bila yakuwa na wenyeji lazima kuna mtu au watu walioshirikiana na wahalifu hao”, alisema Mulongo na kuongeza “ kwa mazingira ya Nyumba ya kina Pendo ilipo kule hakuna sehemu yakutokea na kama mliona pikipiki inaranda randa mchana,.. iweje mshindwe kuitilia shaka? Hapana,  hii haikubaliki! mimi nimekuja kuwaambia nataka Pendo apatikane na sio vinginevyo, nawapa siku tano ijumaa nitarudi hapa mniambie Pendo yuko wapi! Alisema mkuu huyo wa Mkoa akionesha kusononeshwa na tukio hilo. 

“Mbona mifugo inapo ibwa inapatikana”? Aliwahoji viongozi wa sungu sungu na kusema haiingii akilini kusema wakati wa tukio la utekaji sungu sungu wote walikuwa wamekwenda kula chakula na ndipo kadhia hiyo ilipotokea, mkuu wa mkoa, alihoji kufatia kauli iliyotolewa na kiongozi wa sungu sungu kuwa wakati wa tukio askari wote wa sungu sungu walikuwa wamekwenda kula majira ya saa tatu na tukio kutokea saa nne.

MWENYEKITI WA ALBINO MWANZA.
Awali akielezea kusikitishwa kwake na tukio hilo, Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu wa Ngozi mkoani hapa Alfred Kapole, alisema inasikitisha kuona wanadamu wakiwauwa binadamu wenzao kama vile wanyama bila hata woga na vyombo vya maamuzi vikishindwa kutoa hukumu kwa wakati huku akielekeza lawama zake kwa mahakama na Mkemia Mkuu.

 “Mh. Mkuu wa mkoa inasikitisha kuona miongoni mwa kesi 72 zilizokuwa mahakamani, ni kesi 3 tu ndizo zilizokwisha kutolewa hukumu” alisema Kapole, na kuongeza ingekuwa ni kesi ya Wabunge wameshindana kwenye masuala ya uchaguzi ingekuwa imekwisha hukumiwa lakini kwakuwa ni mlemavu wa ngozi,  basi kupuuzia kumekuwa kwingi mno. Alisema kapole.

Akinukuu maneno kutoka katika kitabu cha Biblia, Kapole alisema hata kama hukumu zitashindwa kutolewa na wanadamu hapa Duniani, naamini Mungu wa Mbinguni kuna siku haki itatendeka kwa kuwa “Kitabu cha Mika 3.3-7 kinaeleza juu ya hukumu watakayo ipata watu walao nyama za watu bila woga. Kesi zinaendeshwa Polisi wanajitaihidi sana lakini mkemia watendaji wa ofisi ya mkemia mkuu wanatuhujumu kwa kuita nywele zetu albino ni za Midoli, aling’aka Kapole wakati akielezea kusikitishwa na ofisi ya Mkemia mkuu wa serikali pindi inapo pelekewa Nywele.

Mwenyekiti Kapole pia aliomba kwa yeyote aliye na Mtoto huyo kumrejesha na kama wamemdhuru basi warejeshe hata mwili wake ili matanga yaweze kufanyika, akatumia fursa hiyo kumomba Rais wale wote waliohukumiwa kunyongwa wanyongwe ili kuepusha kuendelea kula chakula cha serikali bure.

RC ITIKADI KATIKA KAZI.
Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa aliwataka wanachi kuweka mbali itikadi zao za namna yoyote na kufanya kila linalowezekana  ili kufanikisha zoezi zima la kuwasaka walio husika na utekaji wa mtoto Pendo Emmanuel, ambao unasimuliwa kuleta siamanzi kubwa ndani ya jamii ya wana Kwimba na watanzania  lakini pia kuchafua taswira ya nchi mbele ya mataifa mengine ya Dunia . Huku akiwaonya watu wa haki za binadamu kuacha kupaza sauti za kuwatetea wahalifu. Tanzania inatajwa kuwa kinara cha ukatili huo tangu mauwaji hayo yalipo zuka mwanzoni mwa miaka ya 2006/2007.

TAKWIMU ZA KIMATAIFA.
Kwa Mujibu wa takwimu za kimataifa zinaonesha ni asilimia 2% tu ya watu ambao huzaliwa na ulemavu wa ngozi ndio hufikia na kusherekea miaka 40 ya kuzaliwa kwao, huku pia takwimu zikionesha katika nchi za Afrika mtu mmoja (1) kati ya elfu mbili (2000) huzaliwa wakiwa na ulemavu wa ngozi wakati katika marekani ni mtu mmoja kati ya elfu kumi na saba ndio huishi na ulemavu wa ngozi. 

Mauaji ya Albino katika Tanzania yanaonekana kushamiri katika Mikoa ya kanda ya ziwa, ambapo imani za kishirikina zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha mauwaji ya hayo lakini pia yale yalio wahusu vikongwe yanayo husishwa na  masuala ya kujipatia utajiri wa haraka suala ambalo sio la kweli, ambapo takwimu zinaonesha kuwa mauwaji yalianza  siku nyingi japo kuripotiwa katika mamlaka za serikali na vyombo vya habari ilianza  mwaka 2006/2007.

Hivi sasa zipo asasi za kiraia zinazo jihusisha na harakati za kupinga mauwaji hayo ikiwapo asasi ya Under The Same Sun ya Nchini Canada na kwa Tanzania imeshakuwa na tawi toka mwaka 2008.

KAMANDA WA POLISI.
Awali akitoa taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mulowola alisema tayari watu 15 wanashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoani humo kwa mahojiano zaidi akiwapo baba mzazi wa Pendo, lakini pia jeshi hilo limefanikiwa kuipata piki piki iliyotumika kufanya unyama huo. “Hivi sasa tunawashikilia watu wapatao kumi na watano na wanaendelea kuhojiwa na Polisi” alisema Mlowola na kuongeza kuwa huo sio mwisho kwa kuwa jinai haina mwisho hata miaka ishirini tukio hili litaendelea kuchunguzwa”, na kusema hata kama yeye atahamishwa au kustaafu kijana atakayekuja ataendelea na kesi hiyo, hivyo wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa kile wanacho kifahamu, alisema Mlowola na kusema tayari Jeshi hilo mkoani hapa limetangaza kuto Milioni tatu 3 kwa atakayefanikisha kupatikana kwa mtoto  Pendo.

Mtoto Pendo alikuwa ni miongoni mwa alibino 74 waliopo katika wilaya ya Kwimba na alikuwa namba 9 katika suala la kupatiwa ulizi.
Imeandaliwa na Afisa habari Mwanza- Atley Kuni.