ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 10, 2015

BARAZA LA HALAMSHAURI YA WILAYA YA MOSHI LAMCHAGUA MICHAEL KILAWILA KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI.

Wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,wakiwa ukumbini hapo kabla ya kuapishwa.
Baadhi ya wajumbe wa baraza hilo kabla ya kuapishwa.
Wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,wakiapishwa kuwa madiwani rasmi.
Katibu tawala wilaya ya Moshi,Remida Ibrahim akiongoza zoezi la upigaji kura kwa ajili yakumpata Mwenyekiti na Makamu wake wa Halmashauri hiyo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akiteta jambo na Diwani wa kata ya Kahe ,Rodrick Mmanyi wakati wa kikao cha baraza hilo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akipiga kura wakazi wa zoezi hilo.
Wajumbe wakishiriki zoezi la upigaji kura.
Diwani wa kata ya Mabogini Emanuel Mzava akimpongeza Diwani wa kata ya Kindi,Michael Kilawila baada ya kutangazwa mshindi kwa kupigiwa kura 36 .
Madiwani wakifurahia mara baada ya kuvaa joho rasmi kwa ajili ya uzinduzi wa baraza hilo.
Mwenyekiti mpya wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila akiongozana na Makamu wake ,Exaud Mamuya wakati wakiingia katika ukumbi wa baraza hilo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji akitoa muongozo wakati wa uzinduzi rasmi wa baraza hilo.
Mwenyekiti wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila akitoa hotuba yake ya kwanza wakati wa uzinduzi rasmi wa baraza hilo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza wakati wa uzinduzi wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi.
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro ,Severine Kahitwa akitoa maelekezo mbalimbali ya uendeshaji wa baraza hilo kwa Madiwani na uongozi mpya wa baraza hilo.
Menyekiti wa Chadema wilaya ya Moshi vijijini Ekarist Kiwia pia alikuwa ni miongoni mwa mashuhuda wa mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi ,Michael Kilawila.
Ndugu wa madiwani wakifurahia nje ya ukumbi wa Hlamshauri ya wilaya ya Moshi mara baada ya Madiwani kuapishwa.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kakskazini (0755659929).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.