ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 11, 2015

KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI ATEMBELEA KAMBI YA WAKIMBIZI NYARUGUSU ILIYOKO WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA NA KUWATAKA WAKIMBIZI HAO WADUMISHE AMANI NA UTULIVU

Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke (kushoto) akizungumza na watumishi wa mashirika mbalimbali yaliyoko katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kulia) aliyetembelea kambi hiyo jana.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kulia), akizungumza na watumishi mbalimbali (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kutembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Kambi hiyo inahifadhi wakimbizi kutoka nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
Daktari wa Hospitali ya Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu, Florence Mshana (aliyeshika karatasi), akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kushoto), alipotembelea hospitali hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Kambi hiyo inahifadhi wakimbizi kutoka nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
Mkuu wa Ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) Kasulu, Amah Assiama - Hillgartner( kushoto), akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizaraya Mambo ya Ndani, Mbarak Abdulwakil (katikati), aliye tembelea hospitali hiyo wakati waziara yake katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, MbarakAbdulwakil(katikati), akiongozana na Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu (B),Fredrick Nisajile (kulia) na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) Ofisi ya Kasulu, Amah Assiama –Hillgartner(kushoto) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu kambini hapo jana. Kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma inahifadhi wa kimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (katikati), akiongozana na Mkuu wa Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu (B),Fredrick Nisajile (kulia) na Mkuu waShirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) ofisi ya Kasulu, Amah Assiama –Hillgartner (kushoto) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu katika makazi ya wakimbizi yaliyopo Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, akimsikiliza mmoja wa maofisa waShirika la Chakula Duniani (WFP) alipotembelea ndani ya mahema wanakoishi wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.