ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 7, 2015

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA MWANZA STANSLAUS MABULA AFUNGA MAFUNZO YA AIRTEL FURSA.

Meya Stanslaus Mabula akiongea na vijana Mwanza wakati wa uzinduzi  wa warsha maalum kwa vijana  ya'Airtel Fursa'  kutoka Airtel Tanzania yenye lengo la kuwawezesha Vijana wajasiliamali nchini iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji Mwanza.
Baadhi ya vijana wa mwanza wakifuatilia kwa makini mafunzo alikuwa yakiendeshwa na Airtel Fursa yenye lengo la kuwawezesha vijana kupata mafunzo kwenye usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mikopo, kufungua akaunti ya benki na mambo muhimu katika kuendesha biashara. Warsha hiyo ilifanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji Mwanza.

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiongea na vijana wa Mwanza wakati wa uzinduzi  wa warsha maalum kwa vijana  ya'Airtel Fursa'  kutoka Airtel Tanzania yenye lengo la kuwawezesha Vijana wajasiliamali nchini iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji Mwanza.
Mtaalamu wa maswala ya kijamii na ujasiliamali bw, Fidelis Madaha akifundisha mada ya Masoko katika warsha ya Airtel fursa iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya jiji jana. Airtel inaendesha warsha hizo kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata mafunzo kwenye usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mikopo, kufungua akaunti ya benki na mambo muhimu katika kuendesha biashara.
Airtel Fursa yazinduliwa na warsha mkoani Mwanza Jijini Mwanza Tarehe 7 July Meya Stanslaus Mabula amezindua warsha maalum kwa vijana  ya 'Airtel Fursa'  kutoka Airtel Tanzania wenye lengo la kuwawezesha Vijana.

Akiongea katika ufunguzi wa warsha hiyo na uzinduzi wake alisema, mpango huu wa Airtel Fursa ni mzuri na umekuja kwa wakati sahihi na kuwawezesha vijana kwa kuwapa vifaa ili kuboresha biashara zao "Wote tunajua tatizo kubwa linalowasumbua vijana kwa sasa. 


Wengine wanaelimu nzuri lakini bado hawajapata ajira hivyo Airtel Fursa imekuja kusaidia. Najua si rahisi kufikia vijana wote kwa wakato mmoja lakini warsha tunayoanza leo ni mwanzo mzuri hivyo nawasihi vijana wengi iwezekanavyo kuomba kujiunga na mpango wa 'Airtel Fursa' na kama wakichaguliwa wawe miongoni mwa walionufaika na mpango huu na kuupa sifa mkoa wetu kwa kuleta mabadiliko", alisema Amewasihi vijana wa jiji hilo kuitumia nafasi hiyo kwa kuonyesha ubunifu na kuhakikisha wanakua kwenye hali ya kupongeza Airtel kwa
nafasi waliopata.


"Tunajisikia heshima kwa kuteuliwa kuwa mkoa wa pili baada ya Dar Es Salaam ambapo ulifanyika mwezi uliopita na  kunufaika na mradi huu wa Airtel Fursa na hiyo inaonyesha jinsi Airtel inavyojitolea kwa ajili ya kuhudumia jamii. Tunawashukuru kwa kuiunga mkono serikali kwa kutengeneza ajira na kupunguza umasikini", alisema Meya Mabula


Alisema Mwanza kunavipaji vingi hivyo vijana wanaweza kutumia nafasi hiyo kuboresha maisha yao na kukuza uchumi wa Mwanza. "Huu sio wakati wa kusubiri wakati kunanafasi nyingi, vijana wetu wanatakiwa kujihusisha na shughulu mbalimbali zitakazowafanya wanufaike na mpango huu wa Airtel Fursa" alisema


Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema, "Airtel Fursa ni moja ya huduma za jamii kutoka Airtel na kuwataka vijana kujiunga na mradi huo".


Alisisitizia vijana kuwa sio  tu wanaojiunga ndio watakaonufaika na Airtel Fursa bali pia mpango huo utatoa mafunzo kwa vijana zaidi ya 1500 kila mwaka nchi nzima kupitia warsha kama hii iliyofanyika Mwanza katika Ukumbi wa Jiji (City Hall)  kwa lengo la kuwawezesha vijana kujijenga na kujitegemea kwa kupatiwa mafunzo kwenye usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mikopo, kufungua akaunti ya benki na mambo muhimu katika kuendesha biashara.


Airtel Tanzania imedhamiria kufanya kazi na Serikali ili kuhakikisha vijana wanaangaliwa na wanaamini mpango huu utaleta mabadiliko makubwa na yakushangaza kwa vijana wa Mwanza na maeneo mengine yatakayofikiwa na mpango huu wa Airtel Fursa.


Mmoja wa vijana  washiriki wa 'Airtel Fursa'  Emmanuel Benjamin akifunguka.
Mtaalamu wa maswala ya kijamii na ujasiliamali bw, Fidelis Madaha akifundisha mada ya Masoko katika warsha ya Airtel fursa iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya jiji jana. Airtel inaendesha warsha hizo kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata mafunzo kwenye usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mikopo, kufungua akaunti ya benki na mambo muhimu katika kuendesha biashara.
Darasa la 'Airtel Fursa' 
Wadau toka Airtel Tanzania
Mmoja wa vijana washiriki wa 'Airtel Fursa' Elina Elikana akichangia.
Mambo ya kuzingatia.
Kwa umakini.
Vijana  ya'Airtel Fursa'  Mwanza.
Meya Stanslaus Mabula akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Airtel mara baada ya kuzindua warsha maalum kwa vijana  ya'Airtel Fursa'  kutoka Airtel Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.