ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, July 5, 2015

KAMATI MAALUM YA CCM ZANZIBAR YAPITISHA JINA LA DKT. SHEIN KUGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CCM UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 2015.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, ambaye pia ni  Mjumbe wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar, akisalimiana na Rais wa Zanzibar, ambaye pia ni Makamu  Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Ali Shein, wakati walipowasili kwenye Ukumbi wa Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria katika kikao cha Kamati Maalum ya CCM Zanzibar, ambacho leo kilipitisha jina la Dkt. Shein kuwania nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM. Picha na OMR
Makamu  Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Ali Shein, akizungumza na Wajumbe wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar (hawapo pichani) wakati wa kikao cha Kamati Maalum ya CCM kilichofanyika leo Julai 5, 2015 kwenye Ukumbi wa Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar kwa ajili ya kujadili na kupitisha jina la Mgombea Urais wa Zanziba kwa Tiketi ya CCM. (katikati) ni Mjumbe wa Kamati hiyo, ambaye aliongoza kikao baada ya kuteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti, Dkt.Mohammed Gharib Bilal na Mjumbe, Balozi Iddi. Picha na OMR
Kiti cha Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Shein, kikiwa wazi baada ya kukabidhi madaraka kwa wajumbe ili kujadili na kuteua jina la mgombea Urais wakati wa Kikao Maalum cha CCM, leo. Picha na OMR
Kaimu Mwenyekiti wa CCM, Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akiendesha Kikao hicho maalum cha Kamati Maalum, baada ya kuteuliwa na Wajumbe wa Kamati hiyo. Kushoto) ni Balozi Seif Iddi. Picha na OMR
 Dkt.Bilal na Balozi Iddi,wakifurahia baada ya Wajumbe kupitisha Jina la mgombea.

Mjumbe, Dkt.Bilal, akimpongeza Dkt. Shein baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe katika Kikao cha Kamati Maalum ili kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali. Picha na OMR
Mjumbe, Dkt.Bilal, akimpongeza Dkt. Shein baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe katika Kikao cha Kamati Maalum ili kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali. Picha na OMR
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt.  Ali Mohammed Shein, akizungumza na Wajumbe wa Kikao cha Kamati Malum, akiwashukuru baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe hao kugombea Urais wa Zanzibar, katika Kikao kilichofanyika leo Julai 5, 2015 kwenye Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar. Picha na OMR
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt.  Ali Mohammed Shein, akizungumza na Wajumbe wa Kikao cha Kamati Malum, akiwashukuru baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe hao kugombea Urais wa Zanzibar, katika Kikao kilichofanyika leo Julai 5, 2015 kwenye Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar. Picha na OMR
Wajumbe walioshiriki katika Kikao hicho.
Wajumbe walioshiriki katika Kikao hicho.
Wajumbe walioshiriki katika Kikao hicho.
Picha ya pamoja baada ya kikao hicho.
Picha ya pamoja baada ya kikao hicho.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.