ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 18, 2015

DADA ANTU MANDOZA ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE WA VITI MAALUM,VIJANA - BUKOBA LEO

Mgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Bi. Antu Mandoza(Kulia) akirejesha Fomu ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana Bukoba katika ofisi za umoja huo Mjini Bukoba, ahaidi kuinua Vijana Kiuchumi endapo atapata nafasi ya kuwa Mbunge wa Vijana.(Habari Picha na Faustine Ruta/bukobasports).
Mcheza kwao hutunzwa, Vijana wazidi kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi. Binti Antu Mandoza mwenye kuonekana kuwa na umri miaka 22-25 Amerudisha Fomu za kuwania nafasi ya Ubunge Vijana Viti Maalumu kupitia CCM. 

Kwa Mahojiano mafupi ameongelea jinsi anavyopanga kuinua Maisha ya Vijana kwa kuwatengenezea Fursa na mbinu mbalimbali za kujiajiri pia kuwaonya kutokukubali kutumika vibaya na MAKUNDI ya Kisiasa tunapoelekea Uchaguzi kwani ni wajibu wetu Vijana kuilinda Amani yetu. 

Mgombea huyo pia amesema kuwa shauku yake kubwa ni kuwatumikia Vijana kwa kutatua changamoto ya Ajira na pia ametoa ahadi ya kushirikiana na Vijana bega kwa bega kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kagera.

Binti Antu Mandoza akiweka sawa Kumbukumbu zake katika kitabu mbele ya karani Bi. Jasinta Benedicto wa Umoja wa Vijana Kagera.

Dada Antu Mandoza akiwa kwenye Ofisi za Umoja wa Vijana Bukoba.
Mgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Dada Antu Mandoza (kulia) akiptia Fomu yake ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana. Kushoto ni Bi. Jasinta Benedicto karani wa Umoja wa Vijana Kagera.

Mgombea Ubunge viti maalumu kupitia chama cha Mapinduzi dada Antu Mandoza akitoka katika ofisi za umoja wa vijana wa ccm Mkoa wa Kagera baada ya kuchukua fomu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.