ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 28, 2015

MSHITUKO: KAPTENI JOHN KOMBA AFARIKI DUNIA

Mara zote aliimba kwa hisia.... enzi za uhai wake Kapteni John Komba.

Habari zilizotufikia muda mchache uliopita, zinasema kuwa aliyekuwa Mkurugenzi wa TOT na Mbunge wa Mbinga Magharibi (CCM) Kapteni John Komba amefariki dunia katika Hospitali ya TMJ.

Hivi sasa juhudi zinafanyika kuhamisha mwili wa marehemu kutoka TMJ kwenda Hospitali ya Lugalo.

Aidha imeelezwa kuwa KOmba amefariki baada ya kufikishwa Hospitalini hapo akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari ambapo ilikuwa imepanda hadi kufikia 30 majuzi na kufanikiwa kupunguza hadi kufikia 9 jana.


Pia ikumbukwe kuwa marehemu Komba ameacha kazi kubwa aliyokuwa tayari ameianza ya kutunga na kurekodi nyimbo za kampeni akishirikiana na baadhi ya wanamuziki wake wa zamani kama Thabiti Abdul, Jerry Juma na wengineo.

Taarifa zaidi tutazidi kupashana kupitia hapa GSENGO blog.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.