ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 22, 2015

TAIFA STARS V/S AMAVUBI NGOMA DROO 1-1 CCM KIRUMBA MWANZA.

Nahodha wa Taifa Stars Simon Msuva (kushoto) akibadilishana bendera na nahodha wa timuya taifa la Rwanda 'Amavubi' Haruna Niyonzima (kulia) kabla ya mpambano wa kirafiki uwanja wa CCM Kirumba Mwanza. Hadi mwisho wa mchezo timu zinatoka sare ya kufungana bao 1-1.

KUSIKIA KILICHOJIRI BOFYA PLAY
Kikosi cha Taifa Stars 'Maboresho' kilichoshuka leo dimba la CCM Kirumba kukiputa na Amavubi.
Timu ya taifa la Rwanda aka 'Amavubi'
Rais wa TFF Malinzi (wa tano toka kushoto) akiwa na safu ya wakuu meza kuu wakati wimbo wa taifa la Rwanda ukipigwa.
Rwanda.
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa MWAUWASA Anthony Sanga akipata utambulisho toka kwa nahodha wa Taifa Stars Simon Msuva (kulia) ambaye hapa akimtambulisha golikipa wa Stars Manyika Peter.
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa MWAUWASA Anthony Sanga akipata utambulisho toka kwa nahodha wa Rwanda Haruna Niyonzima (kulia) ambaye hapa akimtambulisha golikipa wa Amavubi Oliver Kwizera.
Nahodha wa Stars Simon Msuva (kushoto) akiukokota mpira kulia mwa uwanja kuelekea goli la Rwanda mbele ya Mugeraneza Batist ambaye ndiyo mfungaji wa bao la Rwanda katika mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki ulio katika Kalenda ya FIFA ukifanyika dimba la CCM Kirumba Mwanza. Hadi mwisho Tanzania na Rwanda zinatoka sare ya 1-1.  
Simon Msuva akihaha winga ya kushoto kuelekea lango la Amavubi Rwanda nyuma yake ni beki namba mbili Baysenga Emiry (15) na kwa umakini golikipa wa Rwanda Oliver Kwizera (18) akifuatilia mwenendo wa ulinzi. 
Hili ndili goli la kuongoza la Rwanda likifungwa kwa kichwa dakika ya 9 ya mchezo na Mugeraneza Batist, golikipa kupitia mpira wa kona, naye golikipa wa Stars Manyika akiwa ametoka kuuokoa mpira huo alirudi golini kinyumenyume akiushuhudia ukitikisa nyavu zake .
Mpira unazama kimiani ....Rwanda inapata bao la kuongoza.......
Kutoka kushoto ni Sibomana Patrick (Rwanda), katikati ni Shiza Rama (Tanzania), Mugeraneza Batist, Bigirimana Issa na Ismail Nshatyamagara wote wa Rwanda.
Patashika langoni mwa Rwanda toka winga ya kushoto.
Aaaah mzigo wa Selfie..... Kutoka kushoto ni G.Sengo, Haruna Niyonzima na Ladilaus Mbogo wa Toto Africans ya Mwanza.
Tanzania:- Peter Manyika, Miraj Adam, Gabriel Michael, AndrewVicent, Joram Mgeveke, Salim Mbonde, Said Ndemla, Hassan Dilunga, Kevin Friday/Rashid mandawa dk70, Simon Msuva na ShizaRamadhani/Salum Telela dk 45.

Rwanda:- Oliver Kwizera, Emery Bayisenga, Ismail Nshyutamagara, Maxime sekamana/Yanick Mukunzi dk75, Michael Rusheshangonga, Jean Baptiste Mugiraneza, Haruna Niyonzima, Issa Bigiramana/Andrew Buteera dk61, Betrand Iradukunda/Justin Mico dk90, PatrickSibomana na Janvier Mutuima.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.