ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 13, 2014

Friday, December 12, 2014

PICHA ZA KUELEKEA HITIMISHO LA KAMPENI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA MWIGULU ALIVYO UNGURUMA HII LEO JIJINI MWANZA

Kampeni za serikali za mitaa jijini Mwanza zikiwa zinaelekea ukingoni Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Fedha leo majira ya saa 10 alasili amehudhuria mikutano kadha ya hitimisho na hapa alikuwa akishuka kwenye helkopta uwanja wa Magomeni Kirumba.
Kuelekea jukwaa la kuhutubia.
Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Fedha akihutubia wananchi katika uwanja wa Magomeni Kirumba katika kampeni za hitimisho kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo hii leo kwa kutummia usafiri rahisishi ameweza kupiga mikutano 10 katika maeneo tofauti tofauti ya mkoa wa Mwanza na mkoa wa Simiyu.
Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Fedha akikazia neno.
Wananchi katika viwanja vya Magomeni Kirumba.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Joseph Msukuma akihutubia wananchi wa Magomeni Kirumba jijini Mwanza.
Oyeeee....!!
Utulivu wa wananchi wakisikiliza sera.
Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Fedha akiwaaga wananchi uwanja wa Magomeni Kirumba mara baada ya kumaliza kuchagiza kampeni kuelekea uchaguzi serikali za Mitaa na mara baada ya hapo alielekea kwenye kusanyiko jingine lililofanyika viwanja vya mabatini.
Bye...bye....!!
Mkutano wa hitimisho viwanja vya Magomeni Kirumba Mwanza
PICHA NA ZEPHANIA MANDIA WA GSENGO BLOG.

MWANZA KUFIKIA MALENGO YA MILENIA KUKABILIANA NA AFYA YA MAMA NA MTOTO IFIKAPO DISEMBA 2015

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akifungua Mkutano huo.
Mratibu wa Afya ya mama na Mtoto mkoani Mwanza Secilia Mrema akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Drt. James Kengia akitoa ufafanuzi wa maswali ya wadau waliokutana.
Bw. Stanley Matowo, mataalam wa maji kutoka sekretarieti ya mkoa wa mwanza akichangia katika kikao hicho.
Shekhe wa Mkoa wa Mwanza Hassan Fereji akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Seleman Mzee wakifatilia kwa karibu mtoa mada katika kikao hicho
Na: Atley Kuni-(Afisa habari Mwanza).
MKOA wa Mwanza umejiwekea malengo makubwa ili kukabiliana na afya ya uzazi na malezi bora kwa mtoto ili kuweza kufikia malengo ya milennia ifikiapo Desemba 2015.

Hayo yamesemwa na bibi Secilia Mrema wakati akiwasilisha mada kwenye kikao cha pamoja kilichokutana katika ofisi ya mkuu wa mkoa na wadau wa masuala ya afya mkoani hapa kwa ajili yakupitia mipango waliojiwekea lakini pia kupeana majukumu ili kuweza kufikia azma yao hiyo.

Mrema amesena, kutokana na hali ya uzazi salama kuwa chini ukilinganisha na mikoa jirani kama vile Kagera ndio maana wameamua kukaa pamoja ili waone kwa namna gani wanaweza kutoka mahali walipo na kufikia malengo waliojiwekea ifikiapo  mwishoni mwa 2015.

Amesema kutokana na Uelewa mdogo juu ya njia za uzazi salama kwa watoa huduma na kwa jamii, Mila na desturi zinazofanya utumiaji mdogo  wa huduma za afya ya uzazi na uzazi wa mpango, ushiriki mdogo wanaume ni  baadhi sababu kubwa iliyo wasukuma kuja na mikakati hiyo, lakini pia kutokana na mpango wa Tekeleza sasa kwa matokeo makubwa (BRN) ni njia moja wapo ya visababishi vilivyo wafanya kuja na mikakati hiyo “ Tunajua suala la afya ya uzazi ni jukumu la jamii nzima ndio maana tumeona ni vema tuka kaa wadau wote tunao husika ili tuweze kuangalia kiunaga ubaga mikakati hii tuliojiwekea.

Kutokana na changamoto hizi mkoa kwa kupitia halmashauri za wilaya umejiwekea malengo yafuatayo:-
Kupiga vita mila na desturi zinazofanya utumiaji mdogo  wa huduma za afya ya  uzazi kama  vile, uzazi wa mpango, ushirikishwaji wa wanaume, Kuongeza kiwango cha wajawazito kujifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya  kutoka 68%-80% ifikapo desemba 2015, kuongeza  kiwango cha huduma baada ya kujifungua ndani ya siku 7 kutoka 21% mpaka 62% ifikapo  Decemba  2015, kuongeza kiwango cha watoto wanaozaliwa na kina mama wenye maambukizi ya VVU kutumia  ARV (prophylaxis) kutoka 45% to 65% ifikapo Decemba 2015 kuongeza namba ya vituo vinavyotoaa huduma ya IMCI kutoka 69%-80% ifikapo Desemba 2015, mbali ya mikakati hiyo vilevile mkoa umedhamiria Kuboresha utoaji wa taarifa kwa wakati kutoka 66%-100% ifikapo Decemba 2015. 

Mrema amekwenda mbali zaidi nakusema ili waweze kufikia malengo waliojiwekea watatoa mafunzo kwa watoa huduma kuhusu (njia za kisasa za uzazi wa mpango, huduma za dharura wakati wa uchungu na kujifungua, huduma ya kumsaidia mtoto mchanga kupumua baada ya kuzaliwa, IMCI, mtuha). Aidha kupitia vyombo vya habari watatumia mwanya wakutoa elimu kwa umma ili wajue umuhimu wa afya ya uzazi lakini pia kufanya mikutano mingi ya uraghabishaji kwa umma ili ufahamu umuhimu wa masuala ya afya ya uzazi kwa mama na mtoto.

Mkoa wa Mwanza ni mojawapo ya  mikoa 6 inayo unda kanda ya Ziwa ambao una wilaya ziapatazo saba  zenye visiwa 68. Huku mkoa huo kwa mujibu wa sensa ya watu na  makaazi ya mwaka 2012 ikiwa jumla ya watu wapatao 2,772,509, idadi ya watoto chini ya mwaka mmoja ikiwa ni 104,507, na watoto  watoto chini ya miaka 5 ikiwa ni 516,998 huku  wanawake wenye umri wa kuzaa kwa maana ya umri kati ya miaka (14-49yrs)  ni 677,100. 

Mrema amesema, wastani wa watoto katika familia ni 5.4 (Fertility rate), na ukuaji wa wakazi kwa maana ongezeko la watu kimkoa ikiwa ni 3.2% kwa mujibu wa sense ya 2012, aidha mkoa pia  una jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya 360 kati ya hivyo vituo 263 (73) % vinatoa huduma za afya ya uzazi na mtoto. 

Awali akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilya ya Nyamagana alisema ni jukumu la kila mmoja wetu “kujihoji ni kwa vipi mama apoteze maisha ili hali kila mmoja wetu anajua kuwa mama ndiye anaye tengeneza maisha”? aidha  amesema kuwa kutokana na lengo la nne la millennia kugusa suala nyeti kama hili ndio maana kama taifa tayari tathimini ilifanyika ambapo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara, Makatibu Tawala na Waganga Wakuu wa Mikoa Tanzania walikutana na Mheshimiwa Rais tarehe 15 Mei, 2014 na kupewa taarifa ya tathimini hiyo na kujadili mkakati mpya ulioboreshwa wa kitaifa katika kufikia lengo la 4 na la 5. 

Ifikapo mwishoni mwa mwaka 2015, “Pamoja na mengine tuliyokubaliana mbele ya Mheshimiwa Rais, suala la uwajibikaji lilipewa kipaumbele ambapo kila mmoja wetu aliweza  kupata uzoefu wa mikoa mingine, mfano Singida na Mara jinsi walivyofaulu katika suala la afya ya uzazi.

Kikao hicho cha siku moja kimewakutanisha Viongozi wa dini, wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa halmashauri, wenyeviti wa halmashauri, waganga wakuu wa wilaya na waratibu wa afya ya uzazi wa wilaya pamoja na wataalam kutoka sekretarieti ya mkoa wa Mwanza.

POLISI KANDA YA TARIME RORYA YAMNASA NGALIBA AKIKEKETA WASICHANA

Kuanzia kushoto ni Ngariba (Wankyo Mwikwabe - 65+), watoto wanne walioathiriwa na ukeketaji, Mzazi wa Mtoto Anna na mwisho kulia ni Bibi Rhobi Chacha bibi yao na Ghati.
Wakati wanapakiwa katika gari la polisi.
Ngariba akiwa nje ya jengo polisi kinesi
Vinembe vilivyokatwa pamoja na vifaa ya ngariba.

NA IGENGA MTATIRO, MARA.

MRADI wa kutokomeza ukatili wa kijinsia na ukeketaji kwa watoto wa kike na akina mama ulioanzishwa na mwaka 2010 na Jumuiya ya Kikiristo [CCT] Tanzania, wilaya ya Rorya, umeendelea kuzaa matunda.

Waratibu wa mradi huo katika maeneo ya wilaya hiyo yanayoendekeza ukatili wa kijinsia na ukeketaji kwa watoto wa kike Isack Salasala na Ilibariki Raphael wanaendelea kuibua vitendo vya ukatili huo wakishirikiana na madawati ya Polisi katika vituo vikuu vya Rorya [Utegi], Kinesi na Shirati.

Mbali na uibuaji wa vitendo hivyo na kufikishwa katika vyaombo vya sheria kuchukuliwa hatua za kisheria kwa lengo la kuomesha hali hiyo, pia kunaendeshwa mafunzo kwa jamii ya uelewa wa madhala ya kuendekeza ukeketaji huo kwa watoto wa kike.

Desemba 3, mwaka huu usiku wa Alfajiri, saa 11.00 Ngaliba Wankyo Mwikwabe [65-70] alitiwa mikononi mwa Askari polisi wa kituo cha Kinesi alipokutwa akiwakeketa watoto wa kike katika maficho ya nyumba Anna Magoigwa [14] na Ghati Mwita [15].

Ngaliba huyo alifanya tendo hilo katika nyumba ya mji wa Magoigwa Matiku majira hayo katika kitongoji cha Mlimani Kijiji cha Marasibora kata ya Kisumwa, ambapo alipatwa na viungo vya vipande vya miili ya sehemu za siri zilizonyofolewa vya watoto hao wa kike akiwa tayari amevihifadhi na miti shamba kwa pamoja.

'' Tulimkuta akiwakeketa watoto hao wa kike tukiwa na Askari Polisi wa kituo cha Kinesi usiku wa Alfajiri saa 11.00, desemba 3, mwaka huu katika nyumba moja ya mji wa mzee Magoigwa Matiku katika Kitongoji cha Mlimani kijiji cha Marasibora, Wankyo Mwikwabe alipotushutikia tumeingia ndani alikimbilia uvunguni kujificha na vifaa vyake na wale watoto aliokuwa akiwakeketa'' alisema Mratibu Isack Salasala.

Aidha oparesheni hiyo pia ilifanikiwa kuwapata watoto waliokeketwa na ngaliba huyo siku hiyo waliokuwa wamekeketwa siku ya desemba 2 mwaka huu waliofahamika kwa majina yao kuwa ni Veronica Msangya [14] na Bhoke Msangya [12] ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano [v] katika shule ya msingi ya Marasibora wote wakaazi Kitongoji cha Senta  kijiji cha Marasibora.

Watoto hao walifanyiwa tohara hiyo kwa siri na ngaliba huyo katika nyumba moja ya mji wa Msangya Nyabange mbinu ambayo iliyopo ailiyogunduliwa na kuibuliwa na waratibu wa CCT na kuwasilisha katika Jeshi la Polisi chini ya kamanda wake Lazaro Mambosasa.

Wararibu hao walifanikiwa pia kukamatwa kwa wazazi wa watoto hao waliofanyiwa tohara na Askari polisi wa kituo hicho siku hiyo waliofahamika majina yao ni Nchagwa Magoigwa [35] na Robi Chacha [60] waliofikishwa katika kituo cha Polisi na kufunguliwa majalada ya jinai hiyo.

Gazeti hili lilifanikiwa kulinyaka tukio hilo, na kuweka picha zake za kuhusiana na tukio hilo wakati zoezi hilo likifanyika chini ya Askari polisi hao muda mfupi, aliposika ngaliba akisema kuwa hawezi kuacha kukeketa watoto wa kike hadi hapo akipata kazi nyingine ya kumpatia ujira.

'' Siwezi kaucha kazi hii hadi hapo nikipata kazi ya kunipatia ujira kwani hapa ninafanya kazi hii ninajipatia fedha kutoka kwa wazazi wa watoto hawa'' alisema Ngaliba Bibi Wankyo Mwikwabe.

Bi Wankyo alisema kuwa yeye anafanya kazi hiyo kwa kukubaliwa na wazazi ama walezi wa watoto wanaofikishwa kwake na kuwakeketa na yeye anafurahia wakifishwa na kazi hiyo kuendelea kuwepo ajipatie riziki.

Wazazi wa watoto hao walikiri kuwahusisha watoto wao kwa hiali yao kufanyiwa mila hiyo ili kutekeleza jadi hiyo bila kujali kutokwa baadae na madhala watoto wao hao.

Watoto hao walipoulizwa juu ya hilo walidai kuwa wanafurahishwa na kutendewa na mila hiyo kupitia wazazi na walezi wao na kwamba wao hawana mamlaka ya kuonga kufanyiwa hivyo na hawajui madhala yake.

'' Sisi wazazi na walezi wetu ndio walituhamasisha kufanyiwa ukeketaji kwa kurejea mifano ya wakubwa waliofanyiwa mila hiyo na aliyetufanyia ukeketaji huu ni huyu bibi Wankyo na tuliletwa usiku na kuingizwa kwenye nyumba kwa siri bila watu kujua'' walisikika wakisema watoto hao walipohojiwa na Askari Polisi.

Watoto hao baada ya kuchukuliwa maelezo yao katika kituo cha Polisi cha Kinesi baada ya kumalizika uchunguzi wa kitabibu katika kituo cha Afya cha Kinesi na kubaini kuondolewa sehemu zao a siri kwa kukatwa, waliachiwa mikononi mwa Askari Polisi walipowasafirisha na kuwarusisha majumbani kwao katika Kijiji cha Marasibora.

Tukio hilo ni moja ya matukio yanayopingwa na mradi huo ukikumbwa na changamoto mbali mbali katika jamii kushindwa kubadilika na kuachana na mila hiyo kwa visingizo mbali mbali visivyo na msingi.

Waratibu hao katika msimu huu wa tohala wanaendelea kuibua na kufikishwa katika vituo vya polisi kuchukuliwa hatua za kisheria yaliyoshamili na kutukuzwa katika makabila na koo zinazotekeleza mila hiyo muda wote.

Isacka Salasala na Ilibariki Raphael mapema mwaka huu waliibua tukio la kunyanyaswa mjane Pili Samwel Elphas [24] wa Kijiji cha Omuga wilayani Rorya, aliyepigwa na shemeji yake Isaya Elphas Mei 19, mwaka huu na kumuingizia mti sehemu za siri.

M,jane huyo alifanyiwa hayo na shemeji yake huyo majira ya saa 5.00 asubuhi alipotetea haki yake na mume wake marehemu Samwel Elphas aliponyang'anywa Ardhi [mashamba] na kutimuliwa kutoka nyumbani kwake alipokwenda kuishi na mikononi mwa baba yake mzee Alex Allal.

Waratibu hao katika kumsaidia mjane huyo waliungana na baba mzazi wa mjane huyo na babu yake Mzee Alselemus Raphael Ondieki na kufanikiwa kukamatwa na mtu huyo aliyemfanyia kitendo hicho.

'' Sisi waratibu wa CCT wilayani hapa tuliibua tukio la mjane Pili Samwel Elphas aliyepigwa na shemeji yake  hadi kuingiziwa mti katika sehemu zake za siri zilizopata vidonda Mei mwaka huu na mtuhumiwa Isaya Elphas alifikishwa mahakama ya wilaya ya Tarime'' alisema Salasala.

Tukio hilo lilinukuliwa RB yake UTE/RB/256/2014 katika kituo cha Polisi Utegi ilifunguliwa kesi yake ya jinai CC191/2014 ambapo bado inaendelea na hatua zake changamoto ambayo ilidaiwa na wararibu hao kuwa ipo katika jamii kuchukua muda mrefu kuelewa na kubadilika.

Salasala ambaye ni mchungaji wa kanisa la AIC wilayani Rorya, anasema kuwa licha ya k,utumia mafunzo ya kiroho kwa waumini wake kupinga matendo hayo bado ni kazi ngumu.

'' Kwa mfano bibi Wankyo,muda wote tumekuwa tukimwambia aachane na kukeketa watoto wa kike tukimuelimisha zaidi bado alisimamia msimamo wake wa kuendelea na kukeketa watoto wa kike, kisa eti hana kazi nyingine labda tumpatie kazi nyingine ya kumuwezesha kupata fedha 200, 0000 kwa mwezi sio vinginevyo'' alisema Salasala.

Ukatili wa kijinsia na ukeketaji wa watoto wa kike katika makabila yanayotekeleza mila hiyo hadi sasa nchini licha ya kudaiwa kupungua kutokana na juhudi za kubadilishwa na mashirika ya kijamii ya TAMWA, KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU [LHRC] na TGNP MTANDAO, bado unaendekezwa na jamii.

Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na watoto anayo kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuyawezesha mashirika hayo binafsi ruzuku na k,uacha kutegemea fedha za wafadhili wa ndani na nje kutekeleza miradi hiyo ili kuharakisha kukomesha ukatili katika jamii wanaofanyiwa watoto, akina mama.

'' Ipo haja kazi hii serikali itambue kuwa ni ngumu kufanikiwa hili, kwani ni mila na ni utamaduni ulioshamili muda mrefu tusiachiwe tu mashirika tu, serikali kuanzia ngazi ya kitongoji [ mtaa] hadi ngazi ya kitaifa, wizara yake kutengwa bajeti ya kutosha katika kufanikiwa haya'' alisema Salasala.

Ukatili wa kijinsia na ukeketaji wa watoto wa kike na akina mama wilaya za mkoa wa mara, kwa makabila yaliyoendekeza tabia hizo, umekuwa sugu na kuwafanya wanajamii wakae kando na wengine wanashiriki moja kwa maoja wakitambua wengine kutotambua madhala yake kiafya na kiuchumi wakiacha mashirika ya kijamii na viongozi wa serikali kupata changamoto zake.

MAKARBISHO YA LEO FRIDAY NDANI YA 'THAI VILLAGE NA SKYLIGHT BAND' NI USIKU WA MSIMU WA MAPUMZIKO YA MWEZI DISEMBA

Divas wa Skylight Band wakitoa burudani kwa mashabiki wao Ijumaa iliyopita ndani ya viunga vya Thai Village Masaki wakiongozwa na Meneja wa Band Aneth Kushaba AK47 (katikati), Digna Mbepera (kulia) pamoja na Bela Kombo.
DSC_0016
Aneth Kushaba AK47 sambamba na Bela Kombo wakiwapa raha mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar es Salaam.
DSC_0025
Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa bongo akifanya yake jukwaani kwa mashabiki wa Skylight Band huku akisindikizwa na Sam Mapenzi (kulia) pamoja na Joniko Flower.
DSC_0186
Sam Mapenzi na Sony Masamba wakifanya ya jukwaani huku wakitega kwa ukodak.
DSC_0183
Backstage nako walishindwa kujizuia nakuamua kupasha misuli moto huku wengine wakiendelea na kutoa burudani.
DSC_0184
Backstage nako walishindwa kujizuia nakuamua kupasha misuli moto huku wengine wakiendelea na kutoa burudani.
DSC_0026
Diva Digna Mbepera akitoa burudani kwa wapenzi wa Skylight Band Ijumaa iliyopita kwenye kiota Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0038
Bela Kombo katika hisia kali akiwapa raha wapenzi wa bendi ya Skylight Ijumaa iliyopita ndani ya viunga vya Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0067
Aneth Kushaba na Sam Mapenzi kwenye Kolabo kali ya Utake (nyimbo za Afrika mashariki) huku wakisindikizwa na Digna Mbepera sambamba na Bela Kombo.
DSC_0070
SAM MAPENZI;...Kuna Watu Hatari, Wenye Mapenzi Zenye Siri Kali,...Letu Nalo Lina Jua Kali, Penzi Letu Serikali,....Wajua Nakupenda, Malaika......ANETH KUSHABA; ...I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I, Love You,(Aiyayaaaaa)…I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I Love You,..(Aiyayaaaaa)..I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I Love You, (Aiyayaaaaa)..I'm Going Koo Koo, Na Sijishuku I, I Love You.
DSC_0092
Hashim Donode akipiga vocal kwa hisia kali mpaka mishipa ya damu ikimsimama kichwani, hii yote ni kuhakikisha mashabiki wa Skylight Band wanapa ladha ya kitu roho inapenda.
DSC_0106
Nakupenda pia pia aha....Nakupenda pia...You make me wanna say....Nakupenda pia pia ahaa......Kolabo ya UTAKE matata sana inayowabamba mashabiki wa Skylight Band kati ya Bela Kombo na Hashim Dononde huku wakisindikizwa na Digna Mbepera.
DSC_0117
Mkongwe wa muziki wa dansi Joniko Flower akiwapigishwa ligwaride Sony Masamba, Aneth Kushaba pamoja na Sam Mapenzi Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0114
Mdogo mdogo twende kazi sasa....Majembe ya Skylight Band yakiwajibika jukwaani.
DSC_0209
Shabiki alipoamua kupanda jukwaani nakuoyesha ufundi wake wa kucheza nyimbo ya "SHAKE BODY" aliyokuwa akiporomosha Sam Mapenzi.
DSC_0212
Pale wapenzi wa Skylight Band wanapokunwa na nyimbo hivi ndio muonekano wao mwingine kama analia, mwingine kashika moyo, mwingine kashika kichwa basi raha tupu tukutane leo jioni Thai Village.
DSC_0214
Oya shake body...Oya move body...Make you ring alarm o....Oya shake body burudani na iendeleeeeeeee!
DSC_0148
Hashim Donode aliposhuka jukwaa na kuwafuata mashabiki wa Skylight Band na kucheza nao Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0153
Aicha, Aicha, écoute-moi...Aicha, Aicha, t'en va pas..Aicha, Aicha, regarde-moi...Aicha, Aicha, réponds-moi...Si mwingine ni Hashim Donode akikonga nyoyo za mashabiki wa Skylight Band, njoo leo ushuhudie nyimbo mbalimbali kutoka Skylight Band.
DSC_0150
Hashim Donode wa Skylight Band akimwimbia mtoto mzuri aliyenogewa na uimbaji wake.
DSC_0158
DSC_0161
Kutoka kushoto ni Mkongwe wa muziki wa dansi Joniko Flower, Aneth Kushaba AK47 a.k.a KOMANDO KIPENSI, Sam Mapenzi pamoja na Sony Masamba wakipiga mavocal ndani ya kiota cha Thai Village Ijumaa iliyopita.
DSC_0204
Mashabiki wakijiachia na sebene kutoka Skylight Band.
DSC_0164
Mashabiki wakijiachia na sebene kutoka Skylight Band.
DSC_0193
Mashabiki na style ya 'chuma chuma'
DSC_0175
Bela Kombo akiongoza mashambulizi jukwaani huku Aneth Kushaba na Hashim Donode wakicheza swagga za KIDUKU.
DSC_0178
Le Manager her self Aneth Kushaba AK47 na vijana wake Bela Kombo na Hashim Donode.
DSC_0189
Bela Kombo na Digna Mbepera wakipata Ukodak.

MARIA HEWA AWATAKA WANAINCHI WA KATA YA MAHINA KUWANYIMA KURA WATUMIAO LUGHA ZA MATUSI.









NA PETER FABIAN, MWANZA.

MBUNGE wa Vitimaalum Mkoa wa Mwanza, Maria Hewa (CCM), ameawataka wananchi wa Kata ya Mahina kutowapigia kura wagombea nafasi ya wenyeviti wa Mitaa na wajumbe wao wa vyama ambavyo wamekuwa wakiwatukana matusi na kuwadhalilisha wagombea wenzao jukwaani.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa jana, wakati wa kuwanadi wagombea wa nafasi za wenyeviti wa mitaa 20kupiutia Chama chake, alisema kuwa wakati huu wa kampeni kumeibuka baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakiwatukana hadharani wagombea wenzao na kusema uongo jambo ambalo wananchi mnatakiwa kuwa makini na kutopiga kura za hasira.

“Tunapokuja kwenu na wagombea hawa kuwanadi jambo la busara ni kuwauliza maswali nini watafanya mkiisha wachagua kuwatumikia katika majukumu yao kwenye mitaa yenu, lakini pia watatekeleza sera na ilani za vyama vyao katika kuwaleta maendeleo pamoja kuwahojijinsi gani wamejipanga kuzitafutia ufumbuzi wa haraka kero mbalimbali zilizopo kwa jamii,”alisisitiza.

Hewa aliwahasa wananchi kutopiga kura kwa ushabiki wa kisiasa pia kwa hasira baada ya kuchochewa na baadhi ya wanasiasa badala yake wajitokeze kuwasikiliza kwa makini wagombea wakati huu wa kampeni za kujinadi ndipo mfanye uamuzi sahihi siku ya Desemba 14 mwaka huu ya upigaji kura ili kuwapata viongozi bora watakaowatumikia kwa weredi.

“Pamoja na CCM kupoteza uwakilishi wa Ubunge wa Jimbo la Nyamagana na Udiwani Kata ya Mahina tumeendelea kutekeleza ahadi zetu kwa wananchi, lakini mimi kama Mbunge wa vitimaalum Mkoa wa Mwanza kupitia CCM nimehakikisha utekelezaji wa daraja la Mahina unakamilika ikiwemo kumaliza migogoro ya viwanja katika baadhi ya maeneo ya mitaa ya katani hapa,”alisisitiza.

Naye Rajabu Jumanne anayegombea nafasi ya mwenyekiti wa mtaa wa Ipuli kwa niaba ya wagombea ujumbe wa kamati ya mtaa, akijinadi kwa wananchi alisema kwamba amekuwa mstari wa mbere kushughulikia mgogoro wa viwanja katika maeneo yote ya Ipuli, ambapo hadi sasa malalamiko yameisha na wananchi wamepata haki yao.

Jumanne alisema, wananchi wa mtaa wa Ipuli na mtaa wa jirani wa Mahina wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo nivyema wakawachagua viongozi watakaoshirikiana nao kuhakikisha wanazitafutia ufumbuzi na wananchi wanapata huduma badala ya kuchagua watu ambao wamekuwa wakiwatelekeza wananchi na kuanza visingizio.

“Wananchi tunaomba kura zenu kwa wagombea wote wa mitaa ya Kata ya Mahina kupitia CCM kwani tumekuwa tukishirikiana kwa karibu na wananchi katika matatizo mbalimbali ya kijamii, tumeendelea kuwa wasikivu kwenu na kero zote zilizojitokeza tumezishughulikia kwa kushirikiana na viongozi wa CCM Kata na Wilaya ya Nyamagana,”alisema.

Mkutano huo wa kuwanadi wagombea wa Kata hiyo kutoka mitaa 20 ya Kisiwani, Shigunga, Mandu, Kasota, Maswa Mashariki, Maswa Magharibi, Sokoni, Nyanguruguru, Mahina Kati, Mahango B, Mahango C, Mahango A, Mahango, Temeke, Susuni, Mwananchi, Igelegele, Bugarika, Ipuli na Mahina.