ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 4, 2014

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA COMPASSION LILIVYO FANIKIWA KUBORESHA MAISHA YA AKINAMAMA NA WATOTO MKOANI MWANZA

Mwalimu wa kituo cha Huduma ya Mtoto kanisa la Babtist lililopo Kona ya Bwiru Mwanza akizungumza na wageni wa UN waliotembelea kituo hicho kujionea utekelezaji wa huduma wanazozitolewa, ziara iliyolenga kukagua utendaji katika miradi iliyolenga kutekeleza malengo ya maendeleo ya millennia (MDG) na dira ya taifa 2025.    
BOFYA PLAY KUMSIKILIZA

 “Imekuwa kasumba ya watanzania waliowengi kulalamika bila kufanya kazi kwa bidii, maarifa na uadilifu hivyo ni lazima tuwe na mkakati na tunataka tuwe na kizazi sio cha wanung’unikaji na walalamikaji tunataka tuwe na kizazi chenye kutafuta suluhisho ufumbuzi wa matatizo na suala ya kuwasaidia watoto yatima ni jukumu letu sote kuanzia ngazi ya familia hadi taifa” 
 Pichani ni baadhi ya watoto walionufaika na mpango wa maendeleo wa Compassion Mwanza.
 Picha za ukutani.
 Alisema kuwa mkazo mkubwa umewekwa katika kuwatoa na kuwakomboa watoto waishio mazingira magumu, kuwasaidia kutoka kwenye hali za umasikini wa Kiuchumi, kiroho, Kijamii, na Kimwili na hatimaye kuwawezesha kuwa watu wazima wanaoujua wajibu wao, na wanaojitosheleza.
Moja kati ya malengo  yaliyowekwa na Kituo cha Huduma ya Mtoto ni pamoja na kuendelea kutoa huduma kwa kushirikiana na makanisa yenye ushirika wenza katika misingi ya uadilifu, utu na kuwa mawakili wema wa rasilimali za watoto na jamii na kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa katika vituo vyao vyote. 
Kutoka eneo moja kwenda jingine.
Bi hawa athumani akihadithia jinsi maisha yake yalivyo badilika mara baada kusota kwa kipindi kirefu akiishi kaika kibanda ambapo sasa anamiliki nyumba yake nzuri ya kisasa.
Pamoja na kusaidia watoto waishio mazingira magumu pia shirika la Compassion limewasaidia baadhi ya akina mama katika kuwapa elimu ya Ujasiriamali , Elimu isiyokuwa rasmi, Elimu kwa Wazazi,  Maji, Usafi na kuboresha mazingira yao kama jinsi lilivyomsaidia Bi. Hawa ambaye alikuwa amekata tamaa ya maisha kutokana na kuishi katika hali duni bila msaada. BOFYA PLAY MSIKILIZE 
Wadau wa UN wakiwa katika picha ya pamoja na Bi. Hawa Athumani, na aliye keti ni mume wa Bi. Hawa.
Wadau wa UN na Shirika la Compassion wakiagana na familia ya Bi. Hawa Athumani
SHIRIKA la Compassion International Tanzania limekuwa na mahusiano mazuri na kushirikiana na Serikali, makanisa na jamii ya watu wote wanaotuzunguka na kushirikiana nao katika malezi, makuzi na maendeleo ya kiujumla ya watoto na vijana.

Katika Afrika Mashariki ukiondoa Tanzania shirika hilo lipo Rwanda, Kenya, Uganda na Ethiopia na tayari limezalisha wasomi wengi wakiwemo madaktari na wauguzi wahasibu, wanasheria na askari ambao kwa sasa wamekuwa tegemeo kubwa kutokana na ufadhili unaotolewa na shirika hilo.

Shirika hilo la compassion internation Tanzania lilianzishwa rasmi tarehe 30/4/1999 lengo ikiwa ni kuhudumia watoto wahitaji ili kuwatoa katika umasikini wa kiroho,kiuchumi,kijamii na kimwili na baadae lilianzisha ushirika wenza na baadhi ya makanisa ya kiinjili katika mikoa ya lindi ,mtwara,Iringa  na Arusha ambapo ndio makao makuu.

KAMA ULIPITWA NA PICHA ZA BIRTHDAY YA DIAMOND PLATNUMZ

Platnumz's birthday.
IMG_6274
Mama Diamond na Diamond na Wema.
Staa wa Bongo Fleva anayefanya vizuri duniani Diamond Platnumz au Nasibu Abdul Juma aliyezaliwa October 2 1989 hivi majuzi ya tarehe 2oct alifanya bonge la party kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. 
Kwenye hilo party ambalo lilifanyika Golden Jubilee Towers Dar es Salaam Kilimanjaro Hall lilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa Tanzania wakiwemo waigizaji, watangazaji wa redio na tv, wasanii wa bongo fleva na wengine. PICHA ZOTE NA TAARIFA NEWS
IMG_6214
Mwanamuziki wa muziki wa Bongo Fleva Shilole (R), Mziwanda (C) na Friendz (L)
IMG_6281
Mimina mimina...
IMG_6285
The Platnumz na shampaigne.
IMG_6312
Wema akishiriki kucheza ngoma.
IMG_6313
Hapo vipi...?
IMG_6330
Yamoto Band wakitoa burudani.
IMG_6339
Ze keki...!
IMG_6368
Make a wish...!!
IMG_6373
Diamond alipo muita Dada yake Queen Darleen kula keki.
IMG_6387
Zamu ya Ommy Dimpoz...!
IMG_6401
Flowers.
IMG_6399
Frendz
VIDEO KWA HISANI YA BONGO FIVE. 

MISS UNIVERSE TANZANIA 2011 NELLY KAMWELU ENROLLS AT THE NEW YORK FILM ACADEMY

MISS UNIVERSE TANZANIA 2011 NELLY KAMWELU ENROLLS AT THE NEW YORK FILM ACADEMY

Miss Universe Tanzania 2011 Nelly Kamwelu is in New York and has started her studied in acting at the New York Film Academy . New York Film Academy-School of Film and Acting (NYFA) is a for-profit film school and acting school based in New York City. Nelly’s enrollment is part of her scholarship to the institution that she was awarded when she won the Miss Universe Tanzania title.
Nelly  Kamwelu won the Miss Universe Tanzania and Miss Southern Africa International titles in 2011. She represented Tanzania in Miss Universe 2011 in São Paulo, Brazil, Miss International 2011 in China, Miss Earth 2011 in Manila, Philippines, and Miss Tourism Queen International in China. 
Nelly is the only beauty queen who has competed in four Grand Slam Pagents (Miss Universe, Miss International, Miss Earth and Miss Tourism Queen International) in a single year. Nelly has featured in Music Videos of Tanzanian Musicians and also recorded a song Say it to my face before her departure for Miss Universe 2011. The song was released on YouTube while she was participating in the beauty contest in São Paulo, Brazil 2011.
New York Film Academy's programs include film directing, film producing, screenwriting,  cinematography, film editing,  documentary filmmaking and courses in acting. Since 2010, Miss Universe Tanzania has been sponsored by NYFA and all winners (Hellen Dausen, Nelly Kamwelu and Winfrida Dominic) have attended the Academy. Betty  Omara, Miss Universe Tanzania 2013 will get her chance to attend the Academy once she hands over her crown this October.

For more information:
Mwanakombo Salim – National Coordinator
0655441165


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA KONGAMANO LA BIASHARA LA KIMATAIFA KWA NCHI ZA AFRICA JIJINI DUBAI FALME ZA KIARABU

Mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa Afrika Aliko Dangote katika mazungumzo na Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal kuhusu uwekezaji wake katika kiwanda cha simenti mkoani Mtwara. Dangote alisema kazi ya ujenzi inakwenda kama ilivyopangwa na kwamba kiwanda hicho kitakuwa kikubwa kabisa kwa uzalishaji simenti katika ukanda wa Afrika Mashariki. Picha na OMR

Friday, October 3, 2014

KURA MBILI ZAIPITISHA RASIMU YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA

CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI
Dodoma/Dar. Licha ya upinzani kutoka makundi kadhaa ya wananchi, Bunge la Katiba jana lilihitimisha kazi yake kwa kupitisha Katiba inayopendekezwa baada ya kupata theluthi mbili za wajumbe wa kila upande wa Muungano.
Matokeo hayo yaliyohitimisha mchakato huo, yalifanikishwa kwa tofauti ya kura mbili za wajumbe katika baadhi ya ibara na nyingine kwa kura moja tu, ikimaanisha kuwa iwapo kura hizo mbili zingekosekana hadithi ingekuwa tofauti.
 Kutangazwa kwa matokeo hayo kuliwafanya wajumbe walioshiriki mchakato hadi hatua ya mwisho baada ya wenzao wa kundi la Ukawa kususia, kulipuka kwa furaha, nyimbo, tambo, vijembe na vigelegele huku wakijimwaga ukumbini kusakata dansi.
Akitangaza matokeo hayo, Naibu Katibu wa Bunge hilo, Dk Thomas Kashililah alisema hali ya upigaji kura ilikuwa ni nzuri na kila kura za kila upande zilitosheleza na kutoa uhalali wa Katiba inayopendekezwa kupelekwa kwa wananchi.
Katibu huyo alianza kutoa matokeo ya upande wa Zanzibar ambako wajumbe wengi walikuwa na wasiwasi kuwa huenda usipate akidi ya kura 146 iliyotakiwa.
Kwa jumla, kura za ‘ndiyo’ za Zanzibar zilikuwa ama 147 au 148 na ‘hapana’ ama saba au nane; wakati kwa matokeo ya Tanzania, wajumbe waliopiga kura walikuwa 335 na kura moja tu ndiyo ilikataa ibara zote na kura mbili zilichomoza kukataa baadhi ya ibara.
Matokeo hayo yalithibitishwa na mawakala Amina Makilagi na Waziri Rajabu Salum ambao walisimama na kueleza namna ambavyo kura hizo zilihesabiwa kwa uhuru mpana.
Kuserebuka bungeni
Baada ya matokeo hayo, Ukumbi wa Bunge ulihanikizwa kwa nyimbo za mipasho na mafumbo zikiambatana na kuwashwa vipaza sauti bila ya utaratibu na wajumbe kurukaruka na kukumbatiana kwa furaha.
Hali hiyo, iliwalazimu walinzi wa viongozi kuingia ndani ya ukumbi kwa kuweka hali ya amani kwani wajumbe walianza kuvamia viti vyao kwa nia ya kuwapongeza.
Hali ilipozidi, walinzi wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda walimwondoa haraka na kumweka katika chumba maalumu hadi hali ilipotulia huku idadi kubwa ya walinzi ikisogea kwa Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta.

TOA DAKIKA MOJA TU YA MAISHA YAKO - DONATE 1 MINUTE OF YOUR LIFE

SUBJECT: donate 1 minute of your life

Dear Family & Friends,

It will take less than 1 minute of your life to vote for Under The Same Sun (UTSS).

Please ask your family and friends to do the same.

UTSS has become eligible for a One Hundred Thousand Euro grant from the Netherlands. Every year, the Dutch Ministry of Foreign Affairs awards the Human Rights Tulip to a human rights defender who promotes and supports human rights in innovative ways.

UTSS has been shortlisted to 1 of 30 charities from the original 1 of 160. The next phase of shortlisting will bring us to 1 of 3 charities who become eligible for the grant. This next phase of shortlisting will occur through a website voting system.

Please vote for UTSS.

FIRST – click here

THEN – follow these INSTRUCTIONS:

-        Click on the pink VOTE icon on the right side of the page to proceed to the voting ballot

-        Then enter your email address

-        Then click on the VOTE icon again

-        Within a few seconds you should receive a confirmation email – MAKE SURE YOU CONFIRM YOUR VOTE.

DONE

Thanks so much for your vote,

Thursday, October 2, 2014

DJ STEVE JUNIOR KUTOKA KENYA ATINGA TZ KUKISANUKISHA KESHO IJUMAA VILLA PARK JIJINI MWANZA

Dj Maarufu wa muziki wa Reggae kutoka nchini Kenya Dj Steve Junior akitizama maadhari ya jiji la Mwanza baada ya kuwasili leo mchana kwaajili ya Tamasha la REGGAE BRING BACK LOVE litakalo fanyika kesho Ijumaa (3/oct/2014) Villa Park Mwanza.
Dj Maarufu wa muziki wa Reggae kutoka nchini Kenya Dj Steve Junior (katikati) akifanya mahojiano na G. Sengo (kushoto) katika hoteli ya JB Belmonte baada ya kuwasili leo mchana kwaajili ya Tamasha la REGGAE BRING BACK LOVE litakalo fanyika kesho Ijumaa (3/oct/2014) Villa Park Mwanza. Kulia ni Meneja wa Dj Huyo.
WAFANYABIASHARA wanao miliki vituo vya radio, television pamoja na kumbi za burudani nchini wameaswa kuwekeza katika muziki wa reggae kwa kuanzisha vituo maalum vya kupiga muziki huo na kumbi maalum za muziki huo kwani ni sekta ambayo ni fursa iliyo wazi kwa kuwa soko lake lipo si kwa vijana tu bali hata kwa watu wazima.

Hayo yamesemwa na Dj Maarufu wa muziki wa Reggae kutoka nchini Kenya Dj Steve Junior ambaye yuko jijini Mwanza katika ziara yake ya kuzitembelea nchi kadhaa barani Afrika akitoa burudani ya muziki huo na kuutambulisha uzuri wake kwa jamii kizazi na kizazi ambapo kesho (Ijumaa) kwa mara ya kwanza atakutana na mashabiki wake pale Villa Park kwenye Tamasha lake linalojulikana kama REGGAE BRING BACK LOVE.

Dj Steve Junior anasema kuwa ni kwa takribani miaka kumi sasa amewekeza katika muziki huo akiburudisha na kuufanya muziki huo kuwa sehemu ya kuendesha maisha yake, familia na jamii yake. ZAIDI BOFYA PLAY KUSIKILIZA MAHOJIANO.

Dj Maarufu wa muziki wa Reggae kutoka nchini Kenya Dj Steve Junior (katikati), Kutoka Clouds Fm G. Sengo (kushoto) katika hoteli ya JB Belmonte baada ya kumaliza mahojiano leo mchana ikiwa ni matayarisho kwaajili ya Tamasha la REGGAE BRING BACK LOVE litakalo fanyika kesho Ijumaa (3/oct/2014) Villa Park Mwanza. Kulia ni Meneja wa Dj Huyo.
Dj Maarufu wa muziki wa Reggae kutoka nchini Kenya Dj Steve Junior amefurahia sana mapokezi aliyoyapata toka kwa watanzania wakarimu.
Ni wakati wa ku-Enjoy mazingira safi na tulivu ya jiji la Mwanza yanayo nakshiwa na muonekano wa ziwa Victoria. 
100 usikose Tamasha la REGGAE BRING BACK LOVE litakalo fanyika kesho Ijumaa (3/oct/2014) Villa Park Mwanza. 
Swimming pool iliyo juu ya ghorofa...
With FrendZ...!!
Mpango mzima wa Ijumaa hii tarehe 3/oct/2014

'SIJAFA' ASEMA KIONGOZI WA B.HARAM

Kiongozi wa Boko Haram Aboubakar Shekau.
Kanda ya video inayomuonyesha mtu anayedaiwa kuwa kiongozi wa kundi la Boko Haram imetolewa akikana madai ya jeshi kwamba amefariki.
Katika kanda hiyo,Abubakr Shekau anasema kuwa wapiganaji wake waliitungua ndege ya wanajeshi wa angani iliotoweka wiki tatu zilizopita.
Wiki iliopita jeshi lilidai kuwa mtu anayejionyesha katika kanda ya video ya Boko Haram aliuawa na mwezi Agosti 2013 likadai kwamba huenda Shekue amefariki.
Wachanganuzi wametilia shaka kuhusu uthabiti wa madai hayo ya jeshi.
Wapiganaji wa Boko Haram.
Mwandishi wa Nigeria Ahmad Salkida ,ambaye ana mawasiliano mazuri na Boko Haram alisema kuwa katika mtandao wake wa Twitter wiki iliopita ana hakika kwamba Shekue yu buheri wa afya na kwamba hajafariki.
Haijabainika ni lini ama wapi kanda hiyo iliopatikana na shirika la habari la AFP ilitengezwa.
Lakini muhariri wa Idhaa ya BBC ya Hausa, Mansur Liman ,amesema kuwa mtu aliyezungumza katika kanda hiyo ya video alikuwa Abubakr Shekue yule yule anayeonekana katika kanda nyengine za video za kundi la Boko Haram.
CHANZO: BBC SWAHILI.

UTALII SIYO MBUGA ZA WANYAMA TU!

Mwananchi kitaani kauchapa tulii na wanyama..
Barabara za Kabuholo zama hizi za mvua.
Tafakari mwisho wa barabara.
Basi inasemekana ndani ya mjengo huu kuna bONGe la msusi atakaye kusuka mitindo yote duniani.
Kitaa.
Barabara zinazosubiri ujenzi wa mawe.
Kutoka Rock City taswira kando kando mwa barabara kuu iendayo Musoma. 
Mama zangu na dada zangu wachakarikaji.
Katika majira haya upanuzi wa barabara unaoendelea kwa kipande cha Mabatini hadi buzuruga kina kwamishwa na mvua sijui hali itakuwaje hapo baadaye.
Msaada kwenye tuta.
Ze daraja.
Msongamano nao ni sehemu ya utalii...ha...ha...haaaa!!