ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 29, 2014

NDANI YA YATCH CLUB MUDA HUU NI ZAIDI YA NYAMA CHOMA...!! NJOO!!

Toka Jembe Club one the one and two ni Dj K Flip.
'Down' Prince Mashiku (L) na G.
C The area...DJ K Flip is Banging the Music.
Samaki choma, nyama choma, kuku banika na mavimbwanga vyose.
The area.
Frienndz wakipata ....Nyam Nyam 
Brothers.
Girls
Brothers with them charting.
Artiste Zalli in the house.
Like.
Moja.
Zimebali siku chache sana.....
Meza yangu.
Jembe ...
Go down.
The area na utuliiivu hapa ilikuwa mapeema....

SUUZIKA NA MUZIKI MTAaaaamu!


Mo Music - Basi Nenda.Official Video) 
Mzigo umepikwa: K Recods Mwanza
Producer: Lolpop.

Friday, March 28, 2014

MAHAFARI YA 3 CHUO CHA IQRA WASOMI WAASWA KUTOIGA TAMADUNI MBAYA ZA NCHI ZA MAGHARIBI.

Mkuu wa Chuo Cha IQRA Hamza Juma akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukamilika kwa maafali ya tatu ya chuo hicho, wasomi 98 wamehitimu Astashahada na Shahada katika kozi mbalimbali za Utawala wa Biashara, Teknohama, Uhasibu, Manunuzi na Ugavi, Utenguzi mizigo Bandarini na usafirishaji, Mahusiano na Masoko.
Meza kuu.
Tunuku.
Unastahili.
Wahitimu.
Na vyeti vyao. 
Naibu Meya wa jiji la Mwanza, John Minja akikabidhi cheti kwa mmoja kati ya wahitimu wakati wa mahafali ya tatu ya Chuo cha Utawala wa Biashara na Teknohama cha IQRA, kilichopo Mabatini wilayani Nyamagana, jijini Mwanza.

MWANZA.
WASOMI hapa, wametakiwa kuacha kuiga tamaduni mbaya za mataifa ya Magharibi, ikiwemo ndoa za jinsia moja, ambazo ni kinyume cha maadili yetu na mila za kiafrika.

Wito huo ulitolewa juzi na Naibu Meya wa jiji la Mwanza, John Minja wakati wa mahafali ya tatu ya Chuo cha Utawala wa Biashara na Teknohama cha IQRA, kilichopo Mabatini wilayani Nyamagana, jijini Mwanza.

Hivi karibuni kumekuwepo tetesi kwamba, baadhi ya wanafunzi wanaume wa vyuo mbalimbali jijini Mwanza, tofauti na IQRA, wamekuwa wakijihusisha na Ushoga.

Naibu Meya huyo alisema, wasomi wakiwemo wahitimu wa chuo hicho, wanapaswa kuwa na tabia njema popote wawapo ikiwa pamoja na kufata maadili na tamaduni za kiafrika, wakiiga mambo yasiyofaa ya mataifa ya magharibi, watapotoka na kuongeza mmommonyoko wa maadili.

“Epukaneni sana na tabia za ushoga na ndoa za jinsia moja, mambo hayo hata Marekani hayapo sana na Afrika hatuyahitaji kabisa, Uganda wameyakataa sisi hapa ni kinyume cha sheria kabisa. Nyie mnaohitumu leo msiende kubweteka, kajiendelezeni kielimu.” Alieleza Minja na kuwataka waliohitimu taaluma ya Ugavi na Manunuzi wabishe hodi katika Halmashauri ya jiji la Mwanza, waajiliwe.

Awali akimkaribisha Minja, Mkuu wa Chuo hicho Hamza Juma alieleza kwamba,  katika mahafali hayo ya tatu, wasomi 98 wamehitimu Astashahada na Shahada katika kozi mbalimbali za Utawala wa Biashara, Teknohama, Uhasibu, Manunuzi na Ugavi, Utenguzi mizigo Bandarini na usafirishaji, Mahusiano na Masoko.

Juma alieleza kwamba, chuo chake kinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kukosa eneo la kujenga Chuo (wamepanga katika jengo la mtu binafsi), vifaa vya kujifunzia kama Compiyuta na kumshukuru Minja ambaye aliahidi kushghulikia kwa haraka wapate eneo la kujenga Chuo hicho.

MWANAMKE BORA WA MWAKA 2014

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda kesho atakuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Tuzo ya Mwanamke Bora wa Mwaka 2013-14, itakayowakutanisha wanawake wanne itakayofanyika kesho katika Ukumbi wa The African Dream mjini Dodoma.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ndiye atakuwa mgeni rasmi katika utoaji tuzo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers, ambayo ndiyo iliyoratibu zoezi hilo, Eric Shigongo, alisema jana kwamba shughuli hiyo itakuwa ni hitimisho la kazi kubwa ya kupokea na kuchuja kura zilizotumwa na wasomaji kumtafuta mwanamke bora ambaye ni nembo kwa taifa.
Prof. Anna Tibaijuka.
“Zoezi hili lilifanyika kwa muda wa miezi tisa, kuanzia Juni mwaka jana hadi Machi mwaka huu. Awali kabisa watu walitakiwa kutuma majina ya wanawake wanaowaona ni bora ili wapigiwe kura, watu waliitikia vizuri sana, kwani jumla ya majina 150 yalitumwa katika kipindi cha miezi miwili.
Dk. Asha Rose Migiro.
“Baada ya hapo majina hayo yakaandikwa katika magazeti na watu wakatakiwa kupiga kura ili kuwatoa wanawake ambao wanadhani hawakustahili tuzo hizo,” alisema Shigongo, ambaye kampuni yake inatoa magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Amani, Risasi na Championi.
Alisema katika awamu ya kwanza ya miezi hiyo miwili, majina ya wanawake 20 yaling’ara na hivyo kuingia katika awamu nyingine ya kupigiwa kura, ambapo baada ya muda kama huo pia, wanawake kumi walipata alama nyingi na hivyo kuingia katika awamu ya tatu na ya mwisho.
Mh. Anne Kilango Malechela.
Alisema kwenye hatua hiyo ya mwisho, wanawake watano walipita ambao ni Ananilea Nkya, Anna Tibaijuka, Anna Kilango Malecela, Asha Rose Migiro na mama Maria Kham. Katika zoezi hilo, wanawake hao wenye mvuto katika jamii walichuana na mmoja wao, Nkya, kuondolewa baada ya kura zake kutotosha kwa ajili ya fainali,” alisema Shigongo.
Dk. Maria Kamm.
Kwa upande wake, mratibu wa Tuzo hizo, Luqman Maloto, alisema tukio hilo la kihistoria ambalo pia litashuhudiwa na wabunge wa Bunge la Katiba walio mjini Dodoma, litaambatana na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali, akiwemo Linah,” alisema Maloto.

WATEJA WA AIRTEL KULIPA MIKOPO YA MASOMO KUPITIA HUDUMA YA AIRTEL MONEY.

Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu Bwana Juma Chagonja akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma itakayowawezesha wahitimu wa vyuo mbalimbali nchini kurejesha mikopo yao kupitia huduma ya Airtel Money, kushoto ni Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma itakayowawezesha wahitimu wa vyuo mbalimbali nchini kurejesha mikopo yao kupitia huduma ya Airtel Money kulia pichani ni  Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu Bwana Juma Chagonja
Wateja wa Airtel kulipa mikopo ya masomo kupitia huduma ya Airtel Money

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) imeanzisha mapinduzi ya malipo ya kielectoniki kwa kuwawezesha watumiaji wa huduma ya Airtel Money kulipia mikopo ya elimu ya juu  kupitia huduma ya Airtel money

Ushirikiano huo kati ya Airtel na HESLB unawawezesha wahitimu wa masomo ya juu katika vyuo mbalimbali nchini kuweza kulipia mikopo yao kwa urahisi kupitia huduma ya Airtel Money na hivyo kuongeza ufanisi katika  ukusanyaji wa mikopo hiyo

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde alisema” tumewawezesha kupitia huduma yetu ya Airtel money wateja wetu kuweza kulipia mikopo yao ya elimu ya juu inayotolewa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu kirahisi wakiwa majumbani mwao. Tunawahakikishia wateja wetu huduma bora, salama, ya uhakika yenye viwango vya gharama nafuu  na inayopatikana mahali pote nchini kupitia mawakala zaidi ya elfu 35,000 walionea nchini.

 Huduma hii ni ya haraka na nirahisi kutumia, sasa wateja hawana haja ya kusubiri kwenye mistari muda mrefu kufanya malipo, wanachotakiwa ni kufanya muamala rahisi kwa kupitia simu zao  kulipa na kupata uthibithisho wa malipo ndani ya sekunde chache

Ili kupata huduma hii mteja anatakiwa kupiga *150*60#  na kuunganishwa na orodha ya Airtel Money kasha kuchagua namba 5 kufanya malipo, alafu chagua namba 8  kupata huduma zinginezo kisha kuandika neno HESLB , ingiza kiasi cha pesa, kumbukumbu namba na namba ya siri kufanya malipo  aliongeza mmbando

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu Bwana Juma Chagonja alisema”hii imekuja wakati muafaka ambapo baadhi ya waliofaidika na mikopo hii muda wao wa kurejesha malipo ya mikopo yao umekwisha,  kwa kupitia huduma hii ya kulipia kwa Airtel Money hakutakuwa na haja ya watu kutembea umbali mrefu na kupanga foleni katika mabenki ili kulipia, tunaleta kwa wateja wetu urahisi wa malipo na njia mbadala ya kurejesha mikopo yao kwa wakati na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mikopo hiyo.

Chagonja aliongeza kwa kusema kwa kupitia huduma hii ya Airtel Money sasa wateja wetu wataweza kulipa mikopo yao kirahisi wakati wowote mahali popote masaa  24 siku 7 kwa wiki.

Thursday, March 27, 2014

UCHAGUZI CBE MWANZA 2014 NI ZAIDI YA URAIS.

Huu ni msafara wa mmoja kati ya wagombea uchaguzi wa Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo cha Biashara CBE Mwanza. 
Hapatoshi.
Mazingira ya Chuo.
Kama kuna viashiria fulani hivi... au macho yangu?
Wagombea Mashariki.
Wagombea Magharibi.
MATOKEO TUTAYAANIKA HAPA HAPA
@gsengo.

KAMATI YA UCHUMI NA FEDHA YA HALMASHAURI YA MJI KOROGWE, TANGA YAPITISHA MPANGO WA TIBA KWA KADI (TIKA)

Mwenyekiti wa Hamashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello Bendera akiendesha kikao cha Kamati ya Uchumi na Fedha cha Halmashauri ya Mji kujadili mchakato wa kubadilisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha tatu kimefanyika leo Machi 27, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Pembeni ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtonga, Mheshimiwa Francis Komba (kushoto), anayefuatia ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Dokta Jerry Mwakanyamale (kulia) na Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto).
Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto) akieleza umuhimu wa matumizi ya Tiba kwa Kadi (TIKA) kikao cha Kamati ya Uchumi na Fedha cha Halmashauri ya Mji kujadili mchakato wa kubadilisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha tatu kimefanyika leo Machi 27, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Pembeni ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Dokata Jerry Mwakanyamale (kulia), Mwenyekiti wa Hamashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello Bendera na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtonga, Mheshimiwa Francis Komba.
Wajumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha ya Halmashauri ya Mji Korogwe, Tanga wajadiliana jambo wakati wa kikao.
Diwani wa Kata ya Kwamdolwa, Mheshimiwa Hillary Ngonyani akijadili jambo.
Mchumi wa Halmashauri ya Mji Korogwe, Bw. Kikonge Jeremiah akitoa tathimini zake juu ya matumizi ya Tiba Kwa Kadi (TIKA) kwa wananchi wa halmashauri yao.
Diwani wa Kata ya Ngombezi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya, Maji na Uchumi, Mheshimiwa Omari Chafesi akitoa mwongozo na mtazamo wake katika mchakato wa kubadilisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA).
Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Korogwe, Rabeca Balisidya (wa kwanza kulia) kitoa ufafanuzi wa vifungo vya sheria katika mchakato wa kubadilisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Pembeni yake ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Dokta Jerry Mwakanyamale na Mwenyekiti wa Hamashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello Bendera.
Afisa Muuguzi Kitengo Cha Afya ya Akili, Ayubu Mwakalila nae hakuwa nyuma kutoa mtazamo wake juu ya mada iliyokuwa ikijadiliwa. Picha zoe na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.

SERIKALI YAIPONGEZA AIRTEL KWA KUCHANGIA MAENDELEO YA ELIMU.

Meneja biashara wa Airtel kanda ya kaskazini Brighton Majwala akimkabidhi vitabu vya sayansi kwa mkuu wa wilaya Arusha John Mongela kwa ajili ya shule ya sekondari Naura ya jijini Arusha vilivyotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya airtel chini ya mpango wake wa Shule Yetu.
Wanafunzi wa shule ya sekondari naura ya jijini Arusha wakiangalia vitabu mara baada ya kukabidhiwa vitabu hivyo na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania.
Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela akimkabidhi vitabu mbalimbali mkuu wa shule ya sekondari Naura Sunday Mushobozi  vilivyotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania  katika hafla iliyofanyika shuleni hapo.
Press Release
Serikali yaipongeza Airtel kwa kuchangia maendeleo ya elimu.
Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela aliwashukuru Airtel kwa msaada wa vitabu kwa shule ya sekondari ya Naura na kusema kuwa  licha ya kuwa ni jukumu la Serikali kutoa vitabu kwa shule lakini imekuwa ikizidiwa  na majukumu mengi hivyo kwa msaada huo Airtel wanapaswa kupongezwa kwa kutimiza wajibu wao kwa jamii.
Kauli hiyo imetolewa wakati Airtel ilipotoa msaada wa vitabu kwa Shule ya sekondari ya Naura mkoani Arusha chini ya mpango wake maalumu wa “shule yetu” ambapo Mkuu wa wilaya ya Arusha Bwana John Mongela alikuwa mgeni rasmi.
Bwana Mongela alisema “Vitabu ndio nyenzo ya msingi ya kupata maarifa hivyo kwa Airtel kujikita katika kusaidia jamii kupitia vitabu kwa shule za sekondari kutawawezesha wanafunzi na jamii kupata hazina kubwa ya maarifa na mbinu za kujikwamua kiuchumi kupitia vitabu hivi. Napongeza sana jitihada hizi na mpango huu ambao ni endelevu na yenye kugusa shule nyingi na jamii kubwa ya watanzania kwa ujumla”.
Meneja biashara wa Airtel kanda ya kaskazini Brightone Majwala  akizungumzia msaada huo amesema mpango huo unaolenga kutoa vifaa vya kufundishia mashuleni yaani vitabu vya hisabati, physikia, chemia na biologia  una lengo la kupunguza changamoto za uhaba wa vitabu mashuleni,   tunayofuraha  kutoa msaada wa vitabu kwa shule ya sekondari Naura kwani tunaamini wanafunzi wengi  zaidi watanufaika na kuhamasika kujiunga na kusoma masomo ya sayansi
Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo Gasper Mushobozi aliwashukuru Airtel kwa msaada huu wa vitabu vya sayansi shuleni hapa , lakini alibainisha kuwa msaada huu pia uendelezwe kwa kutuboreshea maabara ya shuleni hapo ili kuweza kupata tecknologia ya sayansi kikamilifu.