ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 22, 2014

KAMPUNI YA AFRICAN BARRICK GOLD MINING YABUNI NJIA MPYA ZA UFUMBUZI WA TATIZO LA AJIRA NCHINI.

INJINIA EVARIST NDIKILO - Mkuu wa mkoa wa Mwanza akifungua Kongamano la wadau wa sekta ya madini lililo andaliwa na Kampuni ya uchimbaji madini ya African Barrick Gold Mining nakufanyika Malaika Hotel jijini Mwanza.  
BRAD GOLDAN – Afisa mtendaji mkuu African Barrick Gold Mining.
KAMPUNI ya uchimbaji wa madini ya dhahabu African Barrick Gold Mining (ABG),  mwaka huu inatarajia kuwapunguza kazi wataalamu kadhaa wa kigeni kutoka mataifa mbalimbali Duniani ili kufungua milango ya ajira kwa watanzania hususani vijana.

Kampuni hiyo imetangaza uamuzi huo Jijini Mwanza katika mkutano wa wadau wa sekta ya madini, baada ya takwimu za Wizara ya kazi na ajira kuonyesha kuwa zaidi ya asilimia 11% ya vijana, waliohitimu katika vyuo mbalimbali hapa nchini hawana ajira za uhakika.

Katika mkutano huo Afisa mtendaji mkuu wa (ABG) Brad Goldan amewaambia wadau hao kuwa kutokana na uzito wa tatizo hilo tayari kampuni hiyo imeshawapunguza kazi wataalamu 121 kati ya 411 ili kutoa nafasi za ajira kwa watanzania.

  Hadi sasa Takwimu zinaonyesha kuwa vijana walioajiriwa wenye umri kati ya miaka 15 hadi 34 ni 9,056,217 wakati idadi ya vijana wasiokuwa na ajira ikionyesha kuwa 1,398,677 na kusababisha ongezeko la watu wasiokuwa na ajira Duniani kufikia million 74.6.
Ni sehemu ya kusanyiko la wadau wa sekta ya madini walio jitokeza katika mkutano huu ulio fanyika hii leo mchana ukumbi wa Hotel malaika jijini Mwanza.
Wadau wakichukuwa data.
 ANTONY DIALO – Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza.
Ushauri WA WADAU HAO umefuata baada ya taarifa ya Afisa mtendaji mkuu wa Kampuni hiyo Brad Goldan kueleza kuwa Kampuni hiyo imeshindwa kulipa kodi katika kipindi cha mwaka 2002 hadi 2006 baada ya serikali kuchelewa kuwasilisha notisi ya madai.   

Mikakati ya Kampuni ya African Barrick Gold Mining kuwekeza kwa wafanyakazi wazalendo zaidi imekuja wakati Kampuni hiyo ikiwa bado inasuasua katika suala la ulipaji kodi, hivyo kuikosesha serikali mapato ambayo yangeinufaisha katika mikakati yake ya kuboresha huduma za jamii. Nao wadau wa mkutano wa sekta ya madini hawakubaki nyuma kutumia fursa hiyo kuishauri (ABG) kujikita katika shughuli za kijamii na kuzingatia ulipaji wa kodi kwa wakati.
Naye blooger wa blogu ya Maarufu ya Kanda ya ziwa inayojulikana kwa jina la Kijukuu Blog (kulia) naye alikuwa sehemu ya wadau na hapa kwa umakiiiiini akichukuwa data na taarifa mbalimbali.
Meza kuu wadau wa ABG.
ATHUMANI AKARAMA – Mkurugenzi halmashauri ya Manispaa ya Tarime akichangia .
PATRICK KALANGWA – Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Msalala mkoani Shinyanga.
DEO MWANYIKA – Makamu wa Rais African Barrick Gold Mining.
Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo Deo Mwanyika anasema katika kutekeleza azma hiyo tayari asilimia 60% ya watanzania wapo katika mataifa mbalimbali Duniani wakisoma masomo maalumu ya ufundi ili waweze kuziba nafasi hizo. BOFYA PLAY KUMSIKILIZA.

MAMA HUYU APOKEA KICHAPO TOKA KWA MWANAMKE MWENZIE KWA KUPITISHA NG'OMBE KWENYE SHAMBA.

MASIKINI wa Mungu mama huyu wa kijiji cha Buhundwe wilayani Rorya mkoani Mara akitambulika kwa jina la Catherine Benedicto, amepokea kichapo kikali toka kwa mwanamke mwenzie aliyetajwa kwa jina la Bi. Tatu Wambura kwa kosa la eti kupitisha ng'ombe kwenye eneo la shamba linalomilikiwa na Bi. Tatu.  

Inatajwa kuwa jumatano katikati ya wiki tunayoimalizia majira ya saa sita mchana, Catherine akiwa anaswaga ng'ombe wake wapatao 30 hivi na ushee kutoka nyumbani kwake kuelekea malishoni alipitisha mifugo hiyo katika shamba la Bi Tatu Wambura, ambalo hata hivyo lilikuwa halijalimwa wala halikuwa na mazao yoyote na ndipo alipoonwa na Bi Tatu alivamiwa na kupewa kipigo kikali kilichoambatana na makofi na mangumi hata kumpelekea mwanamama huyo kupata maumivu makali sambamba na uvimbeckatika baadhi ya sehemu zake za mwili hasa jichoni. 

Hadi kamera yetu inaondoka eneo la tukio suala hilo lilikuwa tayari limefikishwa mbele ya uongozi wa kijiji na tayari hatua za kisheria zilikuwa zimeanza kuchukuliwa ikiwa ni sambamba na taratibu za matibabu kwa Bi. Catherine. 

Tukio hili linatokea ikiwa ni siku chache tu taifa la Tanzania likitoka kuungana na nchi nyingine ulimwenguni kuadhimisha siku ya Mwanamke duniani ambapo suala la unyanyasaji na ukatili limekuwa likitizamwa na kukemewa huku mtu ambaye anatajwa sana kuhusishwa na ukandamizaji pamoja na ufanyaji ukatili akitajwa kuwa  ni mwanamme.

Lakini kwa taswira hii ya mwanamke kumpiga mwanamke mwenzie tena kwa kumshambulia   kiasi cha kutisha inaleta taswira gani? 

Ni moja kati ya baadhi ya nyumba majirani za watu wa kijiji cha Buhundwe wilayani Rorya mkoani Mara, maisha yanaendelea na hapa binti mdogo Robi akitimiza majukumu ya nyumbani kama mtoto.  PICHA NA ZEPHANIA MANDIA.

WIKI YA MAJI ILIVYO AZIMISHWA MKOANI SIMIYU.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mabiti alizindua moja kati ya miradi ya maji kwa kujaza ndoo na kisha kumtwika Bi. Anna Jilala.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Chief Paschal Kulwa Mabiti akifungua rasmi daraja la mto Ngegemo
Wanakikundi cha Ngoma wakipalilia zao la pamba katika kijiji cha Senani wilayani Maswa.
Palizi likiendelea.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Paschal Mabiti akipata maelezo kutoka kwa bwana Lupande Nila jinsi ya kuandaa shamba hadi kulima zao la pamba katika karne hii ambapo ushindani wa ubora unazingatiwa katika soko la ndani na lakimataifa.
Mkuu wa Mkoa Akiwa katika bwawa linalosabaza maji wilayani Maswa lipo katika kijiji cha Zanzui  ikiwa ni kilele cha wiki ya maji.
Baseki wapo kazini wakitumbuiza ukiwa mkoani simiyu utakutana nao wanachapa kazi wala sio maaskari ni wazee kwa shughuli uspime
Mkuu wa mkoa wa simiyu akikagua mradi wa maji katika kijiji cha kilulu kata ya bunamhala wilayani bariadi.akiwa na mkuu wa wilaya ya Bariadi Erasto Sima.
Mmoja wa wanakijiji wa kijiji cha Isanga wilayani maswa akicheza na Nyoka katika uzinduzi wa daraja la mto ngegemo linalounganisha vijiji vya Isulilo na Ngongwa.
Mkuu wa mkoa wa simiyu akipata maelekezo kutoka kwa mhandisi wa maji wilaya ya Maswa. PICHA NA MWANDISHI WETU FAUSTIN FABIAN. 

Friday, March 21, 2014

MAN U USO KWA USO NA BARYERN MUNCHEN: DROO YA UEFA QUARTER FINAL 2014

 Manchester United imepangwa kucheza na Bayern Munich katika michuano ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya huku Chelsea ikipangwa kukutana na Paris St-Germain.
Fainali ya michuano hiyo itapigwa katika uwanja jijini Lisbon wa Estadio da Luz tarehe 24 mwezi Mei.Mechi zao za mzunguko wa kwanza zitaanza tarehe 1 mpaka 2 mwezi Aprili na marudiano yatakuwa tarehe 8-9 Aprili. 
 Mabingwa wa ligi ya Uhispania, Barcelona watapambana na Atletico Madrid, huku Real Madrid ikipangwa kukutana na Borussia Dortmund.
 Chelsea inayoongoza kwenye msimamo wa ligi itaifuata PSG nchini Ufaransa katika mzunguko wa kwanza.
 Manchester na Bayern wanakutana tena tangu mwaka 1999 kwenye fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa, ambapo Ole Gunnar Solkjaer na Teddy Sheringham waliiwezesha Manchester kutwaa kikombe chini ya Kocha wao Alex Ferguson.
Mara baada ya kupangwa kwa timu hizo nchini Switzerland, kiungo mshambuliaji wa Bayern, Philipp Lahm amesema kuwa hawawezi kutetereshwa na nafasi waliyonayo United kwa sasa katika ligi kuu na kusema kuwa watasafiri mpaka Manchester kwa kazi moja tu, nayo ni kufunga magoli. THANX 2 BBC SWAHILI.

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA LATOA TAARIFA JUU YA UTEKELEZAJI WAKE WA MPANGO KABAMBE WA MIAKA KUMI 2014-2023

Pichani ni Postamasta Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania,Bwa.Deos Mndeme akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye Makao makuu ya Ofisi hizo jijini Dar mapema leo kuhusiana na taarifa juu ya utekelezaji wa Mpango Kabambe wa miaka kumi (2014-2023) wa shirika la Posta Tanzania,wakati Tanzania ikielekea kuadhimisha miaka 50 ya Muungano
Pichani Kulia ni Meneja Mkuu Uendeshaji wa Biashara,Bwa.Fortunatus Kapinga akifafanua jambo kuhusiana na taarifa juu ya utekelezaji wa Mpango Kabambe wa miaka kumi (2014-2023) wa shirika la Posta Tanzania,wakati Tanzania ikielekea kuadhimisha miaka 50 ya Muungano.

Amesema kuwa Shirika la Posta limeanza utekelezaji mpango kabambe wa miaka kumi (2014-2023) ikiwa ni dira na mwelekeo wa kuliongoza shirika hilo liweze kujiendesha kibiashara,kubuni na kutoa huduma mbadala,kutumia teknolojia maridhawa na kukidhi mahitaji ya soko la huduma za mawasiliano jumuishi.Kushoto kwake ni Postamasta Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania,Bwa.Deos Mndeme. 
Pichani kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Masuala ya Kimataifa wa Shirika la Posta Tanzania,Bwa.Elias Madule akifuatilia mkutano huo akiwa sambamba na mdau mwingine wa shirika hilo la Posta.
Waandishi wa Habari wakisikiliza taarifa juu ya utekelezaji wa Mpango Kabambe wa miaka kumi (2014-2023) wa shirika la Posta Tanzania kutoka kwa Viongozi wakuu wa Shirika hilo,katika mkutano uliofanyika mapema leo,ndani ya Makao makuu ya Ofisi hizo jijini Dar.

REHEMA MBEGU AIZAWADIA VIFAA KAMBI YA NDONDI YA MWANANYAMALA.

Katibu wa UVCCM akitoa msaada wa gloves kwa Mwinyi Mzengela.
Hapa katibu wa UVCCM akizichapa na mmoja kati ya mabondia wakati wa makabidhiano ya vifaa vya mchezo.
"Hata mimi naweza, ngumi ni mchezo wa wote" ndivyo inavyoonekana akisema bi Rehema Mbegu, hapa akizipiga na bondia Martin Shekivuli
Issa Ommary Peche akizichapa na Mbena.
Bi. Rehema Mbegu akiwa navijana wa kituo cha BigBright pindi alipotembelea kituo hicho.

REHEMA  MBEGU AZAWADIA MABONDIA

MGOMBEA wa kiti cha ukatibu UVCCM  jimbo la kinondoni  bi Rehema Mbegu leo amewazawadia mabondia wa kambi ya bigright ya mwananyamala vifaa vya michezo vyenye thamani kubwa vikiwemo bukta za ulingoni jozi  nane za gloves, vilinda chini(groin guard), na vilinda kinywa (mouth guard).
Bi Rehema mbegu ambae ni katibu wa UVCCM kata ya mwananyamala na kiongozi wa timu ya garden queen ya kinondoni  alitoa vifaa hivyo baada ya kuombwa kwa muda mrefu na vijana hao ambao  yeye pia akiwa kama mlezi wao  awasaidie kufanya hivo.
Akizungumza na wanahabari hizi bi Rehema mbegu alisema  kuwa “kutoa ni moyo na wala si utajiri,niwajibu wetu viongozi kusaidiana katika sekta mbalimbali,  mimi sina uwezo mkubwa  wa kuwatosheleza  kwa  kila kifaa cha mazoezi mnachokihitaji ila ninatoa hivi vichache viwasaidie na kila nipatapo uwezo  sitawaacha nitakuwa nanyi  pamoja kama ilivyo sasa, na  wengine wenye uwezo nimewafungulia njia wajitokezee kuwasaidia mabondia wetu  na ninawaomba wadau wengine wa michezo ,wasiwatenge wanamichezo hasa mabondia, kwani ngumi ni mchezo mgumu na vifaa vyake ni ghali mabondia wenyewe hawamudu kutokana na kipato chao kidogo.hivo tuwasaidie vijana wetu ili tuwaokoe na majaribu ya madawa ya kulevya  na mambo mengine ya kihuni kama wizi, ukabaji na kadhalika.

Nae  kiongozi wa gym ya bigright boxing  ya mwananyamal   amemshukuru  bi Rehema mbegu kwa msaada wa vifaaa hivyo ambavyo wamesema watavitunza na kuvitumia vizuri , na tumepata vifaa hivi katika muda muafaka  hasa katika kipindi hiki cha mashindano  mfululizo yaliyo mbele yetu, kwa  mfano bondia wetu Issa omari nampepeche  atacheza tarehe 29 march na bondia toka Tanga zuberi kitandula katika  pambano la raundi sita kuwasindikiza Japhet kaseba akiminyana na Thomas mashali kugombania ubingwa wa UBO katika ukumbi wa PTA sabasaba, hivyo vifaa hivi vichache vitatusaidia sana katika mashindano haya yanayotukabili tufanye vizuri

SKYLIGHT BAND INAKUFANYA UANZE WEEK-END YAKO KWA KUTABASAMU NI LEO NDANI YA THAI VILLAGE.

DSC_0302
Meneja wa Band Aneth Kushaba AK47 akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita kwenye uwanja wao wa nyumbani Thai Village Masaki jijini Dar huku akisindikizwa na Digna Mbepera pamoja na Winfrida Richard.
DSC_0313
Winfrida Richard na Hashim Donode wakisongesha burudani sambamba na Aneth Kushaba AK47 pamoja na Digna Mbepera.
DSC_0346
Mashabiki wakijimwaga na burudani ya Skylight Band ambapo kila Ijumaa wanapatikana pale Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0363
Aneth Kushaba AK47 akiburudika na shabiki wa Skylight Band.
DSC_0377
Pata picha burudani wanayoipata mashabiki hawa wa Skylight Band ambayo ni habari ya mujini kwa sasa..!!! Usipitwe njoo wewe na yule Ijumaa hii.
DSC_0371
Fursa ndio mpango mzima...njoo uonyeshe ufundi wako leo.
DSC_0401
Shake what'cha your Mama gave yaaa....!!! Wamejaaliwa mashalaah...
DSC_0414
Digna Mbepera na Winfrida pale waliponogewa burudani ya Bendi yao Skylight.
DSC_0397
Mzuka wa Aneth Kushaba AK47 pale burudani inapomkolea nae husindikiza mashabiki kwa style ya aina yake.
DSC_0393
Miziki ya Pwani ilihusika kama inavyooneka picha....Pale kati....!
DSC_0380
Mdau mkubwa wa Gerald Kilimo akishow love na Aneth Kushaba AK47.
DSC_0399
Winfrida na Petit Money wakipata Ukodak.
DSC_0340
Mdau Dagma (mwenye miwani) akiwa na marafiki ndani ya kiota cha Thai Village.
DSC_0300
Birthday Girl Mama Sabrina Chicago akilishwa kipande cha cake mupenzi wake Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha Thai Village huku Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akishuhudia tukio hilo adhimu.
DSC_0432
Kutoka kushoto Petit Money, Claudi wa Maisha Club na Aneth Kushaba AK47 wa Skylight Band.
DSC_0424
Neema Mbuya na Winfrida Richard wakishow love.
DSC_0459
Joshua Ndege (katikati) na ndugu zake.
DSC_0461
Mdau Alois Ngonyani na flowers wa Skylight Band.
DSC_0464
We are Skylight Band Fans!