ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 18, 2014

TUME YA MIPANGO WATEMBELEA BANDARI YA BUKOBA

Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwasili kwenye Bandari ya Bukoba, walipofika kujionea bandari hiyo kongwe iliyopo kwenye fukwe za Ziwa Victoria, mkoani Kagera. Waliotangulia mbele ni Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Wapili kulia). Wengine ni baadhi ya wajumbe wa msafara huo kutoka kushoto ni Bw. Omary Abdallah, Bibi Zena Hussein (Wapili kushoto) na Bw. Julius Edward (Kulia).
Madhari ya gati la Bandari ya Bukoba.
Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye ngazi za kupandia kwenye meli zinazotia nanga kwenye Bandari ya Bukoba.
Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye Ofisi za Bandari ya Bukoba. Jengo la Ofisi hiyo limejengwa takriban miaka 70 iliyopita.
Sehemu ya kupumzikia abiria ya Bandari ya Bukoba.
Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye moja ya maghala ya kuhifadhia mizigo kwenye Bandari ya Bukoba. 
PICHA NA SAIDI MKABAKULI

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.