ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 12, 2014

MARIA HEWA AWATAKA WANAINCHI WA KATA YA MAHINA KUWANYIMA KURA WATUMIAO LUGHA ZA MATUSI.









NA PETER FABIAN, MWANZA.

MBUNGE wa Vitimaalum Mkoa wa Mwanza, Maria Hewa (CCM), ameawataka wananchi wa Kata ya Mahina kutowapigia kura wagombea nafasi ya wenyeviti wa Mitaa na wajumbe wao wa vyama ambavyo wamekuwa wakiwatukana matusi na kuwadhalilisha wagombea wenzao jukwaani.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa jana, wakati wa kuwanadi wagombea wa nafasi za wenyeviti wa mitaa 20kupiutia Chama chake, alisema kuwa wakati huu wa kampeni kumeibuka baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakiwatukana hadharani wagombea wenzao na kusema uongo jambo ambalo wananchi mnatakiwa kuwa makini na kutopiga kura za hasira.

“Tunapokuja kwenu na wagombea hawa kuwanadi jambo la busara ni kuwauliza maswali nini watafanya mkiisha wachagua kuwatumikia katika majukumu yao kwenye mitaa yenu, lakini pia watatekeleza sera na ilani za vyama vyao katika kuwaleta maendeleo pamoja kuwahojijinsi gani wamejipanga kuzitafutia ufumbuzi wa haraka kero mbalimbali zilizopo kwa jamii,”alisisitiza.

Hewa aliwahasa wananchi kutopiga kura kwa ushabiki wa kisiasa pia kwa hasira baada ya kuchochewa na baadhi ya wanasiasa badala yake wajitokeze kuwasikiliza kwa makini wagombea wakati huu wa kampeni za kujinadi ndipo mfanye uamuzi sahihi siku ya Desemba 14 mwaka huu ya upigaji kura ili kuwapata viongozi bora watakaowatumikia kwa weredi.

“Pamoja na CCM kupoteza uwakilishi wa Ubunge wa Jimbo la Nyamagana na Udiwani Kata ya Mahina tumeendelea kutekeleza ahadi zetu kwa wananchi, lakini mimi kama Mbunge wa vitimaalum Mkoa wa Mwanza kupitia CCM nimehakikisha utekelezaji wa daraja la Mahina unakamilika ikiwemo kumaliza migogoro ya viwanja katika baadhi ya maeneo ya mitaa ya katani hapa,”alisisitiza.

Naye Rajabu Jumanne anayegombea nafasi ya mwenyekiti wa mtaa wa Ipuli kwa niaba ya wagombea ujumbe wa kamati ya mtaa, akijinadi kwa wananchi alisema kwamba amekuwa mstari wa mbere kushughulikia mgogoro wa viwanja katika maeneo yote ya Ipuli, ambapo hadi sasa malalamiko yameisha na wananchi wamepata haki yao.

Jumanne alisema, wananchi wa mtaa wa Ipuli na mtaa wa jirani wa Mahina wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo nivyema wakawachagua viongozi watakaoshirikiana nao kuhakikisha wanazitafutia ufumbuzi na wananchi wanapata huduma badala ya kuchagua watu ambao wamekuwa wakiwatelekeza wananchi na kuanza visingizio.

“Wananchi tunaomba kura zenu kwa wagombea wote wa mitaa ya Kata ya Mahina kupitia CCM kwani tumekuwa tukishirikiana kwa karibu na wananchi katika matatizo mbalimbali ya kijamii, tumeendelea kuwa wasikivu kwenu na kero zote zilizojitokeza tumezishughulikia kwa kushirikiana na viongozi wa CCM Kata na Wilaya ya Nyamagana,”alisema.

Mkutano huo wa kuwanadi wagombea wa Kata hiyo kutoka mitaa 20 ya Kisiwani, Shigunga, Mandu, Kasota, Maswa Mashariki, Maswa Magharibi, Sokoni, Nyanguruguru, Mahina Kati, Mahango B, Mahango C, Mahango A, Mahango, Temeke, Susuni, Mwananchi, Igelegele, Bugarika, Ipuli na Mahina.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.