ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 18, 2014

TIGO SASA NI MKONO KWA MKONO NA BODABODA MWANZA

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya ziwa Ally Maswanya akizungumza na waendesha bodaboda mkoani Mwanza, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo madereva wa Bodaboda na mpango wa Tigo kuwawezesha kukuza mtaji kwa kuwapa lita moja ya mafuta bure pindi wanaweka lita tatu au zaidi kwa kulipia kupitia Tigo Pesa. Kushoto ni Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza (RTO) Nuru Selemani.
Sehemu ya madereva wa bodaboda waliojitokeza katika viwanja vya Furahisha mkoani Mwanza, kuingia kwenye mpango wa kuwezeshwa na Tigo kwa kupata ofa ya lita moja zaidi (bure) pindi wanaweka lita tatu au zaidi kwa kulipia kupitia Tigo Pesa. Jumla ya Madereva 300 wameandikishwa mkoani Mwanza katika mpango huo. 
Meneja wa Tigo kanda ya ziwa John Tungaraza (katikati) akitoa maelezo wakati wa kuwaandikisha madereva wa bodaboda mkoani Mwanza, ili waingie kwenye mpango wa kuwezeshwa na Tigo kwa kupata ofa ya lita moja zaidi (bure) pindi wanaweka lita tatu au zaidi kwa kulipia kupitia Tigo Pesa. Jumla ya Madereva 300 wameandikishwa mkoani Mwanza katika mpango huo.
Msafara wa madereva wa Bodaboda ukiranda katika barabara za jiji la Mwanza kuelekea moja kati ya vituo saba vya mafuta vilivyoainishwa kwaajili ya kuingia kwenye mpango wa kuwezeshwa na Tigo kwa kupata ofa ya lita moja zaidi (bure) pindi wanaweka lita tatu au zaidi kwa kulipia kupitia Tigo Pesa.
Zoezi hili la Tigo limekuja ikiwa ni mara baada ya shughuli za usafiri wa Bodaboda kurasimishwa nchini na kutambulika kama sehemu ya ajira rasmi kati ya vyombo vya usafiri rahisi.
Msafara ulipendeza 'kinyama'
Kuelekea moja kati ya vituo vya mafuta kwaajili ya kupata huduma ya ofa ya lita moja kwa kila dereva.
Kituo cha mafuta cha MOIL kilichopo Sabasaba ilemela jijini Mwanza ni moja kati ya vituo saba vilivyoainishwa kwaajili ya mpango wa Tigo kwa kupata ofa ya lita moja zaidi (bure) pindi madereva Bodaboda wakiweka lita tatu au zaidi kwa kulipia kupitia Tigo Pesa.
Mapozi ya washereheshaji.
Mashine za Tigo.
Mpaka kuleEEEeee!!
Kisha msafara ulielekea katikati ya jiji la Mwanza.
Tukio hili licha ya kuwa sehemu ya uchumi na biashara pia lilionekana kama utalii kwa wapita njia.
Aidha John Tungaraza ambaye ni Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa amesema kupitia mpango huu Kampuni yake ikishirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama Barabarani, imeahidi kuandaa siku maalum kwa madereva hao wa Bodaboda mkoa wa Mwanza ambapo watapatiwa semina maalum itakayolenga kuboresha uendeshaji wao kuwa salama barabarani, kuwaepusha na ajali zinazozuilika, sambamba na kutoa leseni bure (zitakazo kuwa zimelipiwa na Tigo) kwa madereva watakao fuzu vyema mafunzo yatakayotolewa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.