ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 11, 2014

RAIS KIKWETE AFUNGUA DARAJA LA KISASA LA MABATINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiweka jiwe la ufunguzi wa daraja la Kisasa la mabatini Mwanza.
* Amfagilia Meya wa Jiji la Mwanza kwa kueleza mipango ya maendeleo na kusema anglipata Mameya kama yeye nchi ingepiga hatua.
*Azindua miradi miwili ya Daraja la kisasa la Mabatini.

*Aweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya kiwango cha lami ya Usagara-Kisesa yenye urefu wa kilomita 16 

Rais Dk Kikwete amagiza viongozi wa serkali ya Mkoa, Wilaya na wananchi kwa kushirikana na vyombo vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua kali watu wanaohujumu miundombinu ya daraja hilo wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa polisi Mabatini.

“Haiwezekani watu waachwe wakiharibu ili kurudisha nyuma maendeleo ikiwemo kukamilika ka daraja hili la kisasa kabisa nchini kote chukueni hatua mara moja kwani kero ya majanga ya ajali, vifo na msongamano ndo kulipelekea serikali kujenga daraja hili,”alsisitiza.

Pia amewaagiza madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela ndani ya Jiji kweka mipango ya maendeleo na kuanza kufikiria ujenzi wa shule za awali, msingi na sekondari kwa kwenda juu ikiwa ni majengo ya gorofa ili kuondokana na uhaba wa maeneo.
“Make kwa pamoja kwa kushirikiana ili kuona njinsi gani mtatekeleza ujenzi huo na mkubaliane maeneo ya kutekeleza ujenzi wa majengo ya shule hizo kwa manufaa ya wanafunzi na Jiji hili ambalo linakuwa kwa kasi”alisema.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea daraja la kivuko cha juu lililojengwa eneo la Mabatini jijini Mwanza akiwa ameambatana na waziri wa Ujenzi, mkuu wa mkoa wa Mwanza, Meya wa jiji, Meya wa Manispaa ya Ilemela na wakuu wengine.
Juu kwa juu daraja la Mabatini Mwanza.
Umati uliofurika kushuhudia uzinduzi huo wa daraja.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia.
Rais Dk Kikwete alisema kufunguliwa kwa daraja hilo kumesaidia kumaliza kero ya ajali za kugongwa watu lakini pia msongamano umepungua na sasa TANROAD wanaendelea na upanuzi wa njia tatu kuanzia eneo la Natta hadi eneo la stendi ya mabasi Buzuruga.

“Tunzeni viwatunze na daraja hili litawezesha kulitangaza Jiji hili na Mkoa wa Mwanza hivyo ni vyema mkashirikiana katika utunzaji kwa wanaofanya uaribifu wa miundombinu yake ikiwa ni pamoja na kupitisha pikipiki, kuvunja taa na wengine kupanda na mawe kwa lengo la kuponda magari yanayopita chini hivyo vyombo vya ulinzi na usala vipo wachukulieni hatua kali,”alisisitiza.

Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuri akihutubia.
Naye Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuri alisema tayari Mkandarasi ameisha pewa kazi ya kusanifu daraja la kisasa na kubwa zaidi eneo la Furaisha ambapo Wizara imeisha toa fedha na litatumia shilingi bilioni moja ili kuwezesha eneo hilo kuwa na daraja pia.

“Tangu umeingia madarakani na kuona inafaa kukusaidia ambapo sikukuhonga ili unipe uwaziri bali kwa kuona inafaa zaidi, umeweza kujenga mtandao wa barabara za lami kwa kilomita 11,154 nchini kote ili kurahisisha watanzania kufika kila mahali hakika umetimiza wajibu wako kilichobaki ni kukuombea kwa mwenyezi mungu utakapo maliza muda wako na tutakukumbuka sana,”alisema.
Dk Magufuri pia alisema tayari Wizara yake imishatoa fedha kwenye Halmashauri ,mbalimbali nchini kwa ajili ya ujenzi wa barabara za vijijini ambapo Jiji la Mwanza limepata Sh. bilioni 1.1 na Manispaa ya Ilemela Shilingi bilioni 1.0.

“Nimshauri Mbunge Wenje auhudhulie vikao vya Baraza la Madiwani ili kupanga maendeleo badala ya kuhamasisha vijana kufanya maandamano na vurugu na kwa kupita kwenye barabara zilizojengwa na Rais Dk Kikwete, serikali ya CCM na hata kwa ujenzi wa daraja hili litasaidia kupunguza maandamano,”alisema huku akishangiliwa kwa nguvu kwa vijembe hivyo.

Aliongeza kuwa Mbunge Wenje leo amesema mwenyewe kuwa yeye si tikiti maji lakini inaonyesha kuwa ni tikitimaji kwani amekuwa na busara ya kuomba kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kutambua hilo hata wenzake ndani ya CHADEMA kungelikiwa hakuna maandamano

Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akihutubia mbele ya Rais Jk na wananchi waliofurika uwanja wa Polisi Mabatini Mwanza.
Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula akitoa salamu za jiji hilo alianza kwa kunukuu maandiko ya vitabu vitakatifu kuwa “watuwangu wanaangamia kwa kukosa maarifa” akimaanisha vijana kutumika vibaya na baadhi ya wanasiasa kwa kuwa mstari wa mbele kufanya maandamano na vurugu kwa matarajio makubwa.

“Maendeleo ni Mipango na Jiji la Mwanza, Mhe. Rais Dk Kikwete limekuwa likiitekeleza ikiwa ni Ilani ya CCM ya uchaguzi ya mwaka 2010 lakini kupita Baraza lake la Madiwani ambapo limejenga barabara za km 9 kwa bilioni 15.2 za lami, barabara za mawe km 2.9 kwa bilioni 1.6,”alisisitiza.

Aidha Halmashauri ya Jiji la Mwanza imeendelea na ujenzi wa  vyumba 68 wa Maabara ambapo kila vyumba vitatu vinajengwa kwa kila sekondari moja ya Kata katika Kata 12 za Jimbo hili, Hlmashauri pia imetoa fedha za kusaidia ujenzi huo ambapo kila chumba kimoja imetoa shilingi milioni 20 na hivyo kila Kata itapewa milioni 60 kwa maabara tatu , awamu ya kwanza zimetolewa milioni 20.

“Tunatarajia ifikapo tarehe 21 Novemba tutakuwa tumemaliza ujenzi japo kuna baadhi ya watu na wanasiasa wanapita huko wakiwaambia wananchi wasichangie maendeleo lakini kiongozi mzuri ni yule anayewahamasisha wananchi wake anaowaongoza kuchangia shughuli za maendeleo ili kupatikana huduma bora za kijamii,” alishangiliwa na umati wa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza akitoa salamu zake.
Maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza wamefika uwanja wa Polisi Mabatini kumsikiliza Mhe. Rais Jk.
Kwaya iliyotia fora kwa ujumbe madhubuti kiasi cha kupata mwaliko siku chache zijazo kwenda jijini Dar es salaam kwenye dhifa ya kitaifa... AIC Vijana Makongoro Choir 'Wana Kekundu' ambao kwa sasa wanavuma kwa album yao iitwayo 'Keusi' wakitumbuiza.
Kiasili zaidi.
Shangwe zikilipuka.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akiwapongeza wanakwaya wa AIC Vijana Makongoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya pamoja na AIC Vijana Makongoro Choir.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya pamoja na viongozi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete picha ya pamoja na wafanyakazi wa TANROAD Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi wake.
Eneo la tukio daraja la Mabatini jijini Mwanza. 

 Awali Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Ezekial Wenje, alipopewa nafasi ya kusalimia alianza kwa kuwapongeza wananchi, walimu, askari na watumishi wengine kwa kukatwa kodi na kufanikisha ujenzi wa barabara, daraja na huduma mbalimbali za kijamii.

“Bila wananchi kulipa kodi, bila kuchangia kununua bidhaa hakika hakuna ujenzi wa daraja wala barabara za kiwango cha lami hivyo ni vyema wananchi mkajipongeza kwa hilo kwani fedha zilizojengwa hapa niza kwenu na si za CCM,” na kushangiliwa na vijana wafuasi wa CHADEMA.

Wenje alisema kuwa nawapongezeni kwa kufanikisha kutokana na kulipa kodi zenu ambazo matunda yake mnayashuhudia leo lakini nikuombe Rais uweze kutujengea barabara ya kutoka Igoma hadi Buhongwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 12.2 likiwemo daraja la Fumagila Igoma.

Awali Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Nishati) Charles kitwanga “Mawe matatu” Mbunge wa Jimbo la Misungwi alimpiga kijembe Mbunge Wenje kwa kusema kuwa vijana msitumike na sasa ni vyema mkajitambua kuliko kutumika kwani dunia ya leo niya Sanyansi na Teknolojia hivyo wajitambue ili kuendana na wakati.

“Acheni kutumika kwa maandamano na vurugu kwani havitawasaidia wala kuwaongezea maarifa hivyo ni vyema mkawa  vijana wenye kuelezwa kisha nanyi mkachanganya akili za kuambiwa na zenu ili msiwe kama Bayuwayi,”alisisitiza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.