ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 28, 2014

KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII YAFANYA ZIARA KATIKA MIRADI MITATU YA NSSF JIJINI Dar

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abubakar Rajabu (aliesimama) akizungumza wakati wa kuwakaribisha Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii,waliofanya ziara ya kutembelea na kuangalia maendeleo ya miradi mitatu inayofadhiliwa na NSSF ambayo ni Mradi wa Daraja la Kigamboni,Mradi wa nyumba wa Mtoni Kijichi na Mradi ujenzi wa kijiji cha kisasa kiitwayo 'Dege Eco Village',iliopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.Katika ziara hiyo ya Wabunge chini ya Mwenyekiti wao,Mh. Said Mtanda (katikati) walivutiwa sana na maendeoe ya miradi hiyo na hivyo kulipongeza Shirika la NSSF kwa kazi nzuri wanayoendelea kufanya.Picha zote na Othman Michuzi.
Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudencia Kabaka (aliesimama) akifafanya jambo mbele ya Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii waliofanya ziara ya kutembelea na kuangalia maendeleo ya miradi mitatu inayofadhiliwa na NSSF ambayo ni Mradi wa Daraja la Kigamboni,Mradi wa nyumba wa Mtoni Kijichi na Mradi ujenzi wa kijiji cha kisasa kiitwayo 'Dege Eco Village',iliopo Kigamboni jijini Dar es Salaam
Mbunge jimbo la Lindi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Salum Barhan akifatilia kwa makini taarifa ya Mradi wa Daraja la Kigamboni iliyokuwa ikitolewa na Meneja Miradi wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi John Msemo (hayupo pichani)
Meneja Miradi wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi John Msemo akielekeza jambo wakati akitoa taarifa ya Mradi wa Daraja la Kigamboni mbele ya Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii waliofanya ziara ya kutembelea na kuangalia maendeleo ya miradi mitatu inayofadhiliwa na NSSF ambayo ni Mradi wa Daraja la Kigamboni,Mradi wa nyumba wa Mtoni Kijichi na Mradi ujenzi wa kijiji cha kisasa kiitwayo 'Dege Eco Village',iliopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Manyovu Mkoani Kigoma,Mh. Albert Obama akiuliza swali kwa Meneja Miradi wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi John Msemo kuhusiana na mradi huo wa Daraja la Kigamboni.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii wakisikiliza kwa makini taarifa ya Mradi wa Daraja la Kigamboni.
Meneja wa Mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF),Mhandisi Karim Mattaka (katikati) akiwaeleza Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii namna wanavyopanga nondo ili kuweka uhimara wa daraja la Kigamboni ambalo linatarajiwa kumalizika mapema mwakani.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Said Mtanda (wa tatu kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau (wa nne kushoto) wakati wajumbe wa kamati hiyo wakitembelea Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es salaam.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii wakiangalia namna maji yanavyotolewa chini kwa ajili ya kuweka nguzo za Daraja la Kigamboni.
Waheshimiwa wakijadiliana wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau (wa pili kulia mbele) akimuongoza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Said Mtanda alieambatana na ujumbe wake wakati wakitembelea miradi mitatu inayofadhiliwa na NSSF ambayo ni Mradi wa Daraja la Kigamboni,Mradi wa nyumba wa Mtoni Kijichi na Mradi ujenzi wa kijiji cha kisasa kiitwayo 'Dege Eco Village',iliopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Maendeleo ya Mradi wa Daraja la Kigamboni.
 Ubao wa Maelezo ya Mrad wa Kijiji
Baadhi ya Nyumba za Mradi wa Kijichi.
Mh. Obama akiangalia Mandhali tulivu ya Kijichi.
Wadau wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa ziara hiyo.
Majengo yanayoendelea kujengwa katika eneo la Mradi wa Kijichi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau akielekeza jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii. 
Mh. Maua Daftari
Mh. Sugu.
Baadhi la Majengo ya Mradi wa Kisasa wa Dege eco Village yakiendele kujengwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Said Mtanda akizungumza na wanahabari walioambatana nao kwenye ziara hiyo.
Picha ya pamoja ya Wabunge Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii pamoja na Viongozi wa Shirika la Taifa la Hifadhi za Jamii (NSSF) mara baada ya kumalizika kwa ziara.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.