ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, September 1, 2014

BOB HAISA USO KWA USO NA BI SHAKILA.

“Nikiwa na umri mdogo sana nilijikuta napenda kusikiliza muziki na hata nikiwa shuleni mwalimu aliyeni vutia sana alikua wa michezo na muziki namkumbuka Mwl. Julieti aliyewahi kushika nafasi hiyo pale Mitindo shule ya Msingi. 

Siku za ijumaa tulitolewa mapema shuleni ili kujiandaa na swala ya ijumaa, kiukweli nilikua nawahi nyumbani kwa lengo la kusikiliza muziki wa mwambao kupitia RTD walikua wakipiga muziki huo muda wa saa saba mpaka saa nane.

Mmoja kati ya watu walionivutia sana katika kipindi cha muziki wa taarabu ni Bi Shakila ambae mara chache tu ndo kipindi kilimalizika bila wimbo wake kwenda hewani, uimbaji wake ulitukuka sana nafsini mwangu hapo nilikua mdogo kama miaka 12 hivi na tayari nilitamani kuimba muziki wa taarab ila kwakua nilikua mdogo, nilitumia shauku hiyo kwa kushiriki uimbaji wa Qaswida madrasa na kutumia vionjo vya Bi shakila katika kunakshi Qaswida jambo lililonifanya niwe star kwenye madrasa. 

Nilipomaliza shule ya msingi ilikua ndo mwisho wangu pia kushiriki madrasa na Qaswida zangu zilitulia kwa muda mpaka nilipojikuta naibukia kwenye muziki wa asili ya kisukuma baadae rap miduara na bongo flava ambapo umaarufu wangu ulibebwa na miduara zaidi kutokana na single ya 'Nipe mgongo' ambayo ilipelekea niingia kwenye orodha ya waimbaji wa muziki wa pwani na kunipa nafasi ya kukutana na wakali wengi wa muziki wa pwani wakongwe na wapya , Nakumbuka siku ambayo sikuamini maskio yangu pale nilipopokea simu kutoka zanzibar sauti nzito iliskika. 

Haloo Asalaam alaikum, niliitikia kisha baada ya maelezo nilitambua naongea na Yusuf Chuchu 'mungu amrehemu' na habari aliyonipa ndo ilinifanya nisituke zaidi kwani ni mwaliko wa kupiga show ya pamoja na Bi Shakila Ooh iliku siku nzuri sana kwani nilijikuta nakumbuka mengi sana na sikua na pingamizi na safari ya zanzibar ikaanza kutoka dar mpaka zanzibar.

Nilifika zanzibar na shauku yangu kubwa ilikua kumuona Bi Shakila ambae tulikutana nae ndani ya Chuchu Fm hapa ilikua kati ya 2008 na 2009 kwakweli nilisikia sauti ya Bi shakila akiimba huku nikimuona live wakati akifanyiwa mahojiano na hapo nilikumbuka mbali kwani licha ya umri wake kupea bado sauti ilikua ileile sikusubiri tena bali alipomaliza zamu yake ya kuongea tu nikamfata na kumnong'oneza ombi langu. 

Tafadhali mama naomba unifundishe kuimba, aliposkia neno lile alitabasam kidogo akanambia tutaongea kisha tuliendelea na mahojiano na zamu yangu ya kuhojiwa ilifuata baada ya joan, spider na wengine tuliokuanao pale redioni, muda ulipotimia tulienda ukumbini na show ilikua moto sana, tulimaliza na kubadilisha namba wote tuliokua tukitumbuiza pale ukumbini .siku iliyofuata ilikua jumapili jioni tulipokutana maeneo ya Forodhani na baada ya kupata urojo mishikaki ya samaki, nyama na pweza kwa ndizi na chips.

Mbali na mapochopocho hayo jumapili, hiyo ndo siku tuliyokubaliana kufanya kazi ya pamoja siku na saa ambayo hatukuipanga, tulitawanyika huku nikifikiria kazi ya kushirikiana na Bi Shakila je iwe taarab mduara au reggae? Sikupata jibu, miaka ikapita huku tukiwasiliana mara kadhaa mpaka valentine day ya mwaka 2013 pale nilipoalikwa tena na ndugu yangu Richard Luhende kwenda kutumbuiza morogoro sambamba na Bi Shakila tulipokutana alinikumbusha Vp mpango wetu tatizo letu wasanii twapanga mengi halafu hatutekelezi nilimuelewa  alichomaanisha nikamjibu Mungu hajapanga siku yetu.

Tukapiga show asubuhi tukaagana kwa kunywa chai pamoja mimi nikarudi misungwi na Bi shakila akarudi dar”. Bob Haisa
Itaendelea.....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.