ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 3, 2014

KIKUNDI CHA RUGU CHANYAKUWA UBINGWA BALIMI NGOMA FESTIVAL 2014.

Baadhi ya wacheza ngoma wa kikundi cha Rugu kutoka Karagwe mkoani Kagera wakishangilia na kitita cha Shilingi 600,000/=mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Balimi Ngoma Mkoa wa Kagera yaliyofanyika katika Uwanja wa Kaitaba Bukoba mjini.
Baadhi ya washiriki na mashabiki wa Balimi Ngoma wakishuhudia fainali za mashindano ya Ngoma mkoa wa Kagera yaliyofanyika  katika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mjini.
Kikundi cha Ngoma cha Rugu- Karagwe chatwaa ubingwa wa Mkoa Balimi Ngoma Kagera.

FAINALI za mashindano ya Ngoma za Asili ngazi ya mikoa zijulikanazo kama “Balimi Ngoma Festival 2014” Mkoani Kagera kikundi cha Rugu chenye makazi yake Karagwe kimefanikiwa kuwa au bingwa wa Mkoa wa Kagera na kuzawadiwa fedha taslimu Shingi 600,00/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa wa Kagera katika fainali za Kanda zinazotarajiwa kufanyika Augusti 16,2014 Mkoani Mwanza.

Nafasi ya pili ya mashindano hayo ilichukuliwa na Kikundi cha Rugolo ile cha mjini Bukoba ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 500,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa katika fainali za Kanda.

Nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha Abagambakamo cha Muleba ambacho kilizawadiwa fedha taslimu Shilingi 400,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Alute Continue ambacho kilizawadiwa fedha taslimu shilingi 300,000/=.

Nafasi ya tano mpaka ya kumi ilichukuliwa na Uviti Ruzinga, Chupukizi, Kasharu, Kabete cha Ihangilo, Jipe Moyo na Upendo Musira hivi vilizawadiwa kifuta jasho cha 150,000/= kila kikundi. Jumla ya Vikundi 11 vilijitokeza kushiriki fainali hizo za Mkoa wa Kagera ngazi ya Mkoa kwa Mwaka 2014.

Akizungumza na kwa nyakati tofauti Meneja matukio wa Kanda yaZiwa, Erick Mwayela alisema Sababu msinigi ya kuwepo kwa Mashindano ya Balimi Ngoma za Asili ni kuenzi na kulinda utamaduni wa Kitanzania.

Mwayela aliongeza pia kuwa wao Kampuni ya Bia nchini ni sehemu yao ya kurudisha fadhila kwa watumiaji wa Kinywaji cha Balimi Extra Lager pamoja na vinywaji vyote vya Kampuni ya Bia Tanzania(TBL).

Fainali za Mkoa wa Kagera zilifanyika katika Uwanja wa Mkoa wa Kaitaba na fainali za Kanda za mashindano ya Balimi Ngoma zinatarajiwa kufanyika August 16,2014 jijini Mwanza kwa kushilikisha vikundi viwili viwili kutoka Tabora, Shinyanga, Bukoba,  Musoma na Wenyeji wa mashindano Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.