ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 11, 2014

Airtel YAWEZESHA MAFUNZO KWA WANAFUNZI WA AFYA KIJIJI CHA MBOLA TABORA.

Mfanyakazi wa huduma za afya bi Amina Wakasuvi akitoa huduma kwa moja ya familia katika kijiji cha mbola mkoani Tabora  ambapo Airtel chini ya mradi wa millennium village imewawezesha wafanyakazi hao kutumia mtandao wa mawasiliano kutoa huduma za Afya.
Akitoa mafunzo kwa wafanyakazi wa huduma za afya katika kijiji cha Mbola mkoani Tabora namna ya kutumia huduma ya mawasiliao ya simu kutoa huduma za kiafya Ambapo Airtel imewapatia wafanyakazi hao huduma ya internet , message na simu bure na kuwawezesha kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia maeneo mengi zaidi.
Wafanyakazi wa huduma za afya katika kijiji cha Mbola mkoani Tabora wakijaribu namna ya kutumia simu zao mara baada ya mafunzo ambapo Airtel inawawezesha kutumia simu zao kutoa huduma za Afya chini ya mradi wa millennium village
Wafanyakazi wa huduma za afya katika kijiji cha Mbola mkoani Tabora wakijaribu namna ya kutumia simu zao mara baada ya mafunzo ambapo Airtel inawawezesha kutumia simu zao kutoa huduma za Afya chini ya mradi wa millennium village

Airtel yawezesha mafunzo kwa wafanyakazi wa Afya kijiji cha Mbola Tabora
·         Airtel yajikita kuboresha mazingara ya jamii  vijijini
Tabora Junanne 10 Juni 2014, wafanyakazi wa afya wa kijiji cha mbola mkoni Tabora wametoa shukrani zao kwa Airtel kufatia technologia ya huduma ya mawasiliano inayoyowawezesha kutoa huduma za afya kwa wigo mpana na kuwafikia wakazi wengi zaidi.

Wafanyakazi hao wa afya walipata mafunzo ya namna ya kutumia technologia ya huduma ya afya kupitia simu iitwayo COMCARE, iliyoanzisha kwa msaada wa Dagiba  inapatikana kupitia simu za smart phone zenye application maalumu inayowawezesha wafanyakazi wa afya kukusanya takwimu za wagonjwa na kutuma repoti kwenye vituo vya afya.

Akiongea wakati wa mafunzo mmoja wa wafanyakazi wa afya Ms Amina Wakasuvi alisema” Tekinologia hii mpya  ya kisasa itatuwezesha kufatilia kazi zinazofanywa na wafanyakazi wa afya wakiwa katika maeneo mbalimbali na wafanyakazi hao wataweza kutuma repoti zao kwa wakati kila siku kupitia mtandao wa Airtel. Hivyo tunawashukuru sana Airtel kwa ubunifu huu na huduma ya vifurushi vya internet vya bure vinavyotuwezesha kufanya kazi zetu kwa wakati.

Akionge wakati wa tukio hilo Meneja huduma kwa jamii bi Hawa Bayumi alisema” kwa miaka mitatu sasa Airtel imewekeza katika kuleta mapinduzi ya kupatikana kwa  huduma kwa jamii husasani katika maeno ya vijiji vya Tabora  kwa kushiriki katika mradi wa  Millennium village kama mtowaji mkuu wa huduma za mawasiliano.

Katika mradi huu Airtel inatoa njia ya mawasiliano kwa kuwezesha jamii inayoishi katika maeneo ya pembezoni kupata huduma za Afya. Wafanyakazi wa afya katika maeneo hayo wameunganishwa na mtandao wa kisasa unaowapatia huduma ya internet na simu na kurahisisha kazi zao pindi wakiwa kazini. 

Sasa wafanyakazi hawa wanaweza kukusanya takwimu kwa kutumia simu na pia kuwawezesha wagonjwa walioko vijijini kuongea na madakitari specialist walioko mjini na kupata huduma za afya kupitia simu za mkononi” Bayumi aliongeza mpaka sasa tumeiwezesha miradi mitatu kupata huduma ya kupiga simu, ujumbe mfupi na vifurushi vya internet bure, Airtel inaendelea na dhamira yake ya kuwaleta watanzania karibu na huduma muhimu za jamii kupitia technologia ya mawasiliano.

Akiongea kuhusu mradi huo, Mkurugnzi wa mradi wa Millennium Village Dr. Gerson Nyadzi alisema “ Mtandao wa 3G wa Airtel umetuwezesha kwa kiasi kikubwa  kufikia maeneo ya vijijini  ambapo huduma ni duni na haba. Kuanzia mradi huu uanzishwe  kumekuwa na ongezeko la 85% la  upatikanaji wa huduma muhimu za afya hapa Mbola.

Kwa kuongeza mradi wa Child count katika techonologia ya huduma za afya ya CommCare kutawezesha zaidi ya wakazia 97% kupata huduma za afya kupitia watoa huduma wetu wa afya wenye vyenzo hizi muhimu za kutendea kazi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.