ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 29, 2014

MMILIKI WA TIMU YA MAN UNITED, AFARIKI DUNIA BILA KUKANYAGA DIMBA LA OLD TRAFORD.

Mmiliki wa timu ya Manchester United, Malcolm Glazer, amefariki dunia huko nyumbani kwake Marekani akiwa na umri wa miaka 85.
Glazer aliinunua klabu hiyo mwaka 2005 kwa pauni milioni 790 sawa na shilingi trioni 2.2, na akashuhudia timu hiyo ikipata mafanikio kadhaa ikiwemo kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya na ya Ligi Kuu ya England.

Hata hivyo, Chini ya umiliki wake uliosabibisha deni kubwa kwa klabu hiyo ''the Red Devils'' walishinda taji la premia ya Uingereza mara tano na vile vile taji la klabu bingwa mwaka wa 2008 .
Wanawe mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuadhiri umiliki wa United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo .
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenyehisa katika soko la hisa la NY stock Exchange.
Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl .
Bwenyenye huyo ambaye hakuwahi kanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.
Glazer inasemekana alianza kisiriri kuwashawishi wenye hisa wa klabu hicho kumuuzia hisa zao tangu mwaka wa 2003 kabla ya kutwaa umiliki wama wa 2005.
United ambayo msimu uliopita ilitangaza faida kubwa ya asilimia 20 yaani pauni milioni 418 inakabiliwa na deni la zaidi ya pauni milioni 400.
Glazer aliyeugua kiharusi tangu mwaka wa 2006 amewawachia wanawe sita umiliki wa klabu hiyo ya Uingereza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.