ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 7, 2013

BONDIA FRANSIC MIYEYUSHO, KUMSAMBARATISHA DAVID CHALANGA WA KENYA

BONDIA Fransic Miyeyusho wa Tanzania amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi katika mchezo wake na  David Chalanga kutoka Kenya utakaofanyika Desemba 31 katika ukumbi wa Msasani Klabu mchezo uhu wa kufunga mwaka na kufungua mwaka utakuwa wa raundi nane

Utakuwa chachu kwa mabondia hawo wanaotamba Afrika Mashariki kugombea mikanda mikubwa ya ubingwa na kujiongezea rekodi ya ushindi mpambano huo unaosubiliwa kwa hamu na mashabiki  wa mchezo wa masumbwi kila kona ya tanzania sasa imekuwa gumzo

akizungumzia mpambano huo miyeyusho amesema yeye yupo fiti wakati wowote hule kwani ata sasaivi kama mpinzani wake yuko tayali yeye yupo kwa ajili ya kupigana katika mpambano huo kutakuwa na mapambano ya utangulizi

bondia Iddy Mnyeke ataoneshana ubabe na Cosmasi Cheka,Antony Mathias akizipiga na Fadhili Majiha Ibrahimu Class 'King Class Mawe' akizichapa na Mohamed Kashinde

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Floyd Mayweathar,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo huo vitakaokuwa vikitolewa na Super D kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha ngumi

STARS YATINGA NUSU FAINALI CECAFA 2013

TIMU ya Kilimanjaro Stars imefanikiwa kusonga mbele hatua ya Nusu Fainali baada ya kuwatoa Mabingwa watetezi wa Kombe hilo Uganda kwa ushindi wa changamoto ya penalti 3-2 katika michuano ya kombe la Chalenji inayoendelea jijini Nairobi, shujaa akiwa kipa Ivo Mapunda .
Katika mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Manispaa ya mji wa Mombasa,  Uganda ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza likifungwa na Daniel Sserunkuma katika dakika ya 16 akimalizia krosi ya Khamis Kiiza, bao ambalo halikudumu sana kabla ya Mrisho Ngassa kuisawazishia Stars kwa shuti kali  nje ya 18.
Baada ya bao hilo Stars walikuja juu na kufanikiwa kupata bao la pili likifungwa na Ngassa tena kwa mpira wa adhabu uliojaa wavuni katika dakika ya 39, matokeo ambayo yalidumu mpaka mwisho wa kipindi hicho cha kwanza.
Kipindi cha pili Stars inayofundishwa na kocha Kim Poulsen, raia wa Denmark, ilipata pigo katikati ya kipindi hicho baada ya kiungo wake Salum Abubakar 'Sure Boy' kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kucheza rafu, ambapo nafasi hiyo iliwapa nguvu Uganda kupata bao la kusawazisha kupitia Martin Mpuga matokeo ambayo yalibaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo na kuzipeleka mpaka kwenye matuta.

Katika mikwaju ya penalti golikipa Ivo Mapunda alikuwa shujaa baada ya kucheza penalti mbili za Waganda ya beki  Khalis Alucho na  ile ya mwisho iliyopigwa na Sserunkuma ambayo ndiyo iliyoivusha stars.
Ifuatayo ni orodha ya waliopiga penalti katika mchezo huo.

Kili Stars                                                   Uganda
Erasto Nyoni (kakosa)                     Godfrey Walusimbi (kakosa)
Mbwana Samatta (kakosa)                Emanuel Okwi (kapata)
 Amri Kiemba (kapata)                      Khalis Alucho (kakosa)
Athuman Idd (kapata)                        Hamis Kiiza (kapata)
Kelvin Yondani (kapata)                    Sserunkuma (kakosa)

MAKUNDI YA KOMBE LA DUNIA 2014 YAPATIKANA.

Hapana shaka wapenzi wa soka barani Afrika pamoja na kuomboleza kifo cha Nelson Mandela wamekuwa wanafuatilia Droo ya kombe la dunia kufahamu nani wapinzani wa timu tano zinazowakilisha bara hilo.
Cameroon wamejikuta katika kundi gumu la A pamoja na wenyeji Brazil, Mexico na Croatia.
Dua ya Ivory Coast ya kuepuka kundi gumu sana wakati huu inaonekana imesikika, wako katika kundi C pamoja na Colomboa, Japan na Ugiriki.England watakuwa na kibarua kigumu kwenye kundi D ambapo wapinzani wao ni Italia, Uruguay na Costa Rica.Mabingwa watetezi Uhispania watakuwa katika kundi B pamoja na Netherlands waliokutana nayo fainali kombe lililopita, na timu zingine ni Chile na Australia.
Kwenye kundi E Ufaransa inacheka usiku huu kwani imepangwa pamoja na Uswizi, Ecuador na Honduras.Mabingwa wa Afrika Nigeria wako katika kundi F pamoja na Argentina Iran na Bosnia Harcegovinia, ambayo inashiriki kombe la dunia mara ya kwanza.
Ghana ndiyo inayoonekana kuwa matatizoni miongoni mwa timu za Afrika. Wamejikuta katika kundi G ambapo watapamaba na na Ujerumani, Marekani na Ureno.Timu ya tano ya Afrika Algeria itakuwa kwenye kundi H na wapinzani hapo ni Ubelgji, Korea Kusini na Urusi.

MAKUNDI KWA URAHISI ZAIDI:-
Group A:
Brazil, Croatia, Mexico, Cameroon
Group B:
Spain, Netherlands, Chile, Australia
Group C:
Colombia, Greece, Ivory Coast, Japan
Group D:
Uruguay, Costa Rica, England, Italy
Group E:
Switzerland, Ecuador, France, Honduras
Group F:
Argentina, Bosnia-Herzegovina, Iran, Nigeria
Group G:
Germany, Portugal, Ghana, USA
Group H:

Friday, December 6, 2013

SAKATA LA ZITTO LAWACHOMOA VIJANA 200 CHADEMA MWANZA

Na Peter Fabian.                                    
MWANZA. 

UMOJA wa Vijana wa Kata ya Mahina Wawapongeza Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa Wilaya ya Nzega Hessein Bashe na aliyekuwa Mjumbe wa Baraza kuu UVCCM Taifa toka Mkoa wa Mwanza Barnabas Mathayo kwa kufanikisha harambee yao na kupata kiasi cha milioni 10.7 Wilayani Nyamagana.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa UVCCM Gwalis Ahamada baada ya kumalizika kwa zoezi la harambee lililotanguliwa na ufunguzi wa mashina matano ya  vijana katika mitaa ya Bugarika (Shina la Igelegele), Buzuruga (Shina la Mwananchi), Nyakato (Shina la Isegenge ), Igoma (Shina la Machinjioni) na Mahina (Shina la Nyangulugulu) ambapo yalipatiwa fedha kiasi cha milioni 1.8 kwa yote.

Akizungumza kabla ya kuanza kuchangisha waalikwa na wananchi mgeni rasimi Mathayo aliyeongoza harambee hiyo kutokana na Bashe kuwa na majukumu mengine ya kikazi aliwaeleza vijana kuwa wajibu wao ni kuitumikia jumuia hiyo kwa kila hali na kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinazidi kuongoza na kuunda serikali pamoja na kutekeleza Ilani yake kwa vitendo.

Mathayo ambaye alipokea vijana 200 walioamua kujiunga kuwa wanachama wapya wa  UVCCM  na CCM Kata ya Mahina kwa madai kuwa wamechoshwa na hila na vurugu zinazoendelea kwenye Chama cha Demkrasia na Maendeleo (CHADEMA) na hivyo kuamua kukitosa chama hicho na kujiunga kwenye jumuiya hiyo na CCM Katani humo.

Mjumbe huyo mstaafu aliwakumbusha vijana hao kanuni na taratibu za jumuiya na CCM ambapo inawataka kuwa wanachama waaminifu na watiifu na kuachana na tabia yakuwa wanachama ndumilakuwili kwa kuwa na Kadi za Vyama vingine vya siasa kama ilivyo kwa wanasiasa wengine.

“Msiwe kama Yule Babu ambaye ni Katibu wa Chama fulani lakini anakadi ya CCM na amekuwa akiwajibu watu kuwa ni mali yake na ametunza kumbukumbu ya wajukuu zake hivyo nawahasa kuacha kufuata nyayo hizo kwa kuwa huo ni “umalaya” wa siasa na watu kama hao hawafai kuongoza Taifa letu kwa vile lengo lao ni uchu wa madaraka tu na si kuwatumikia wanachama”alisisitiza.

Mathayo alisema kwamba wanachama wa UVCCM na CCM wakiwa na umoja na kufuata kanuni na taratibu zilizopo za Katiba hakuna chama ambacho kitaweza kuishinda CCM katika chaguzi zijazo kwa kuwa chama kitakuwa na mvuto na ukizingatia nyinyi ni vijana mliokubali kwa ihali yenu kujiunga .

“Niwapongezeni sana kwa uamuzi wenu sahihi na kwa wakati sahihi kutaongeza ari ya vijana wengine kujiunga na jumuiya na Chama kwa kuwa ndicho chama pekee kimbilio la wengi chenyekuwajali vijana na watanzania kwa kuhakikisha usawa na demkrasia inaendelea kuwa imara ndani ya chama hiki kikongwe Barani Afrika ” alisisitiza.

Mmoja ya wanacha wapya aliyejiunga na CCM katika Kata hiyo ambaye alikuwa Katibu wa Shina la CHADEMA eneo la Buzuruga William Mahene alipopatiwa nafasi ya kusalimia alisema kuwa CCM ni chama bora afrika kitaendela kutawala kutokana na kufuata vyema kanuni na taratibu za Katiba yao na si CHADEMa kila siku ni kufukuzana hakina dira bali ni kuwahamasisha vijana ili kupata umaarufu tu si kushika dola.

“Nilikuwa huko lakini kitendo walichofanyiwa wanasiasa na wengine kuenguliwa kwa hila akitolea mfano wa Dr. World Kaburu (Kigoma) , David Kafurila (Mbunge) na sasa Mbunge Zitto Kabwe (Naibu Katibu Mkuu), Dr Kitilya Mkombo (Mjumbe Kamati Kuu) kwa hila na njama za kina Godbless Lema (Mbunge-Arusha) John Mnyika (Mbunge-Ubungo) , Freeman Mbowe (Mwenyekiti) na Dr. Wilbroad Silaa (Katibu Mkuu)” alisema.

Wachangiaji wa Harambe hiyo ni Bashe (laki tano), Mathayo (milioni 3), Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (milioni 3), Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mahina James Bwire (milioni 2) walioongoza waalikwa wengine kuwachangia na kufikia lengo lililokusudiwa katika harambee hiyo.

AIRTEL BINGWA KUFUNGUKIA MBAGALA ZAKHIEM KESHO

 
WASANII WAKALI NEY WA MITEGO NA YOUNG KILLER KUONYESHANA NANI BINGWA … KATIKA HIP HOP MBAGALA

Haya sasa mabingwa woote WA AIRTEL BINGWA  kula bata pamoja wikiendi hii Mbagalaaaaaa

Kama wewe ni bingwa wa kusakata kabumbu na kuonyesha umahili wa kumiliki mpira njoo KESHO tuonyeshe jumamosi hii MBAGALA ZAKHIEM kuanzia saa sita mchana mpaka saa 12 na nusu…..zawadi kibao kutolewa jezi, tisheti, ……….

On stage atakuwa wasanii huku atakuwa Ney wa Mitego pande ya huku atakuwapo Young killer  bila kuwasahau Vinoko shackers ndani,

Piaaaa wadada kumi wazuriii watachuana kupiga dana dana live.

Huku tukishuhudia draw ya Mimi Bingwa watu wanavyojishindia mamilioni na ticket ya kwenda old Trafford kuangalia live mechi za  Man U bureee

Kama haitoishi Sasa screen kubwa ya ukubwa zaidi ya mita  4 itaonyesha live mchezo wa Man u na Newcastle united

Kiingilio ni BUREEEEE

Bata hili linaletwa kwenu na Airtel kupitia Promotion ya Mimi ni bingwa

KIDUMU AWASILI TZ KWA SHOO YA TTC "CLUB E" ITAKAYOFANYIKA LEO MLIMANI CITY

1.      Ticket zinauzwa katika vituo vifuatavyo; Samaki Samaki (Mlimani City na Samora), Engen Petrol Station (Mbezi na Mikocheni), TCC Club Chang’ombe, Rose Garden, Shoppers Supermarket (Mikocheni na Masaki) na Dar West Park Tabata.

2.      Kwa Maelezo Zaidi kuhusu Event na Ticket piga simu… 0787 33 33 15
Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidumu” akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku kuja kutumbuiza katika Shererhe ya  “CLUB E”- LICENCE TO PARTY  inayotarajiwa kufanyika usiku wa leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Gari iliyombeba msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidumu”.
“CLUB E” PRESENTS…….. LICENCE TO PARTY!!
Mlimani City Hall – Leo Hii Ijumaa!.
Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidum”(kulia) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku kuja kutumbuiza katika Shererhe ya Kampuni ya Sigara Tanzania(TCC) “CLUB E” inayotarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.Kushoto ni mwenye wake, Ather.
Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidum” (katikati) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku na waimbaji wake kuja kutumbuiza katika Shererhe ya Kampuni ya Sigara Tanzania(TCC) “CLUB E” inayotarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

KWAHERI NELSON MANDELA.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ameaga dunia.
Mandela amefariki huko Johannesburg akiwa na umri wa miaka 95 na yeye ndiye aliongoza Afrika Kusini kutoka mikononi mwa watawala wa ubaguzi wa rangi baada ya kufungwa jela kwa miaka 27.

Katika taarifa yake kwa watu wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, alisema kuwa Mandela amewaaga lakini yuko mahali salama.Mandela alikuwa anatibiwa homa ya mapafu nyumbani kwake baada ya kulazwa hospitalini kwa miezi mitatu.
Mnamo mwaka 2005, Mandela alitangaza kwa taifa kuwa mwanawe wa kume alifariki kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.
Rais Zuma amesema kuwa taifa limepoteza mtu waliyemjua kama mtoto wa taifa hilo.
Mandela aliwahi kushinda tuzo ya amani ya Nobel, na kutambulika kama rais aliyeheshimika sana hasa kwa kupatanisha watu wa Afrika Kusini baada ya kuondoka gerezani.
Hakuonekana sana hadharani tangu alipostaafu mwaka 2004.

Thursday, December 5, 2013

HAPA NA PALE VIJIJINI.

Hapa na pale na utalii wa ndani kwa vijiji vyetu.
Huduma ya usafiri wa gari la mwisho (mpaka kesho tena) katika eneo la kijiji cha Mugango kilichopo  Butiama mkoani Mara. 
Maji toka bomba la kijiji cha Mugango wilayani Butiama mkoa wa Mara.
Kushangaa muhimu...
Mtaani kunani ....katika eneo la Mugango.

Hakuna mitaro kwa njia hii ipitayo kijiji cha Dodoma wilayani Magu Mkoani Simiyu.
Kwamvua hii inayonyesha kwa upande wa mashamba ni neema tu kwa mkulima.
Njia haipitiki maji yamefurika barabarani.
Tumeshindwa kuendelea na safari.

MBINU YA MUUZA MAGAZETI NI 'CHIBOKO'

Kwa wale wanao 'peruzi na kudadisi' kisha wanasepa bila kununua magazeti hapa wamekomeshwaje...!?
Kabla ya mbinu hii, ilikuwa desturi ya wakazi wa eneo la Lamadi mkoani Simiyu kufika kwenye kiota hiki cha mchuuzaji magazeti, mara tu magazeti ya siku yanapotinga, watu walikuwa wanayasoma yakiwa mezani wakidai kwamba wanatizama yaliyomo kisha watanunua na mwisho wa siku wasinunue kwa madai kuwa hawajakuta habari wazitakazo, hali ambayo imekuwa ni hasara kwa muuzaji, mtu anapitia taarifa zote muhimu za gazeti kisha anasepa, wakiyaacha magazeti yamechakaa na kutota mafuta kutokana na kupitiwa na kila mkono wa msomaji. 
Magazeti yakawa yanamdodea sana jamaa na kila siku akiyarudisha kwa wakalawake, kuona hivyo ndipo alipokuja na mbinu hii ya kuweka wavu, kwamba gazeti unalitizama kwa mbaaaaaali kama kuku bandani.
Na imekuwa suluhu jamaa sasa anafanya biashara.

KIWANGO CHA UTOAJI PESA CHAONGEZEKA HADI KUFIKIA MILIONI 3 KWA SIKU BURE KUPITIA AIRTEL MONEY.

Meneja huduma ya Airtel Money Asupya Nalingigwa akiongelea ongezeko la kiwango cha kutoa pesa mpaka mil. 3 kwa siku kupitia huduma ya Airtel Money wakati kampeni ya kutuma na kutoa pesa BURE ya hakatwi mtu hapa ikiendelea. Vilevile wateja wa Airtel wanaweza kuweka mpaka kiwango cha shilingi Milioni 5 kwa siku kwenye akaunti zao za Airtel Money.
Airtel Money yaongeza kiwango cha kutoa pesa hadi mil. 3 kwa siku BURE

Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania, imetangaza ongezeko la kiwango cha kuweka na kutoa pesa kupitia huduma ya Airtel Money.

Kampuni hiyo sasa inawawezesha wateja wa Airtel kote nchini kutoa mpaka kiasi cha shilingi milioni 3 kwa wateja waliosajili laini zao kikamilifu kwa kila siku anapotaka kutoa pesa kwa siku.

Vilevile wateja hao wanaweza kuweka mpaka kiwango cha shilingi Milioni 5 kwa siku.
Akiongea wakati wa kutangaza ongezeko hilo, Meneja wa Airtel Money Asupya Nalingingwa alisema kwa sasa wateja watakuwa na uwezo wa kutoa na kuweka kiasi kikubwa cha fedha na kuepuka usumbufu wa kutoa au kuweka pesa mara nyingi.

“Wateja wa Airtel Money na wateja wote wa simu za mkononi wataweza kunufaika kwa kiasi kikubwa.  Wataepuka usumbufu na kujihakikishia usalama wakutosafiri na pesa nyingi kwa kuwa Airtel Money inaliwezesha hilo ambapo kwa sasa watatoa na kuweka kiasi kikubwa cha fedha tofauti na ilivyokuwa awali,” alisema Bw, Nalingigwa.

Aliongeza kwa kusema wateja wa Airtel Money ambao wameweshwa kwa muda mrefu kutuma na kupokea pesa bure kupitia huduma ya ‘Hakatwi Mtu hapa’ wanapata faida kwa kuokoa  kiasi cha shilingi elfu 20 kila wanapotuma  Milioni 3 Tzs na hivyo inasaidia kupunguza makali ya maisha na kurahisisha shughuli mbalimbali zikiwemo za kibiashara.

“Kama ningekuwa mfanyabiashara au mtu mwingine ambaye natumia pesa kwenye mzunguko kila siku, kupitia ongezeko hili ningejihisi mwenye faraja sana kwani shughuli zangu zingeenda vyema,” alimalizia Bw, Nalingigwa.

Kupitia ongezeko hilo kila mwananchi anaweza kutuma na kuweka kiasi cha fedha kulingana na mahitaji yake katika muda wowote unaomfaa.

UKATILI BADO UNAENDELEA KUITAFUNA JAMII YETU

Na Neema  Joseph

Mwanza

Baadhi  ya watoto  yatima  jijini Mwanza wameangukia  katika  janga  la  unyanyasaji wa kijinsia  bila  jamii  kujua   vitendo  vinavyoendelea  katika maeneo  ya  watoto  hao  wa mitaani  hali maarufu kama (Ghetto).

Ilikuwa ni  usiku wa saa  tano  hivi nilifanikiwa  kujichanganya  na kundi  moja  la watoto hao  wa mitaani, huku nami  nikijifanya  ni  muumini wa makundi  hayo, nakumbuka  ilikuwa ni   wa mtaa  mmoja   katika  barabra  ya  Nyerere,  kando  ya barabara  hizo  utakutana  na nyumba  za ghorofa, maeneo  hayo  ndiyo makazi  ya watoto  hao wa mitaani  pamoja na maeneo  mengine jijini Mwanza.

Wakati  nilipokuwa  katika kundi  hilo la watoto wa kike walishuhudia  mwenzetu  mmoja  akifanyiwa  unyama mkubwa, kwani lilitokea  kundi jingine  la wavulana watatu  na kisha  kusogelea  kundi  hilo  na kuamua  kumchukua  binti  mmoja  ambaye alikuwa  amekaa  karibu na barabara na kisha kuingia  naye  kwenye  uchochoro  na  baada  ya muda  ilisikika  sauti  ya  binti  yule  ikiomba  msaada.

Licha  ya  kelele  zile  zilizoashiria  kufanyiwa vitendo    viovu  vya  kubakwa, baadhi  ya watu  waliokuwa kipita  eneo  lile  waliendelea  na  shughuli zao  bila hata  kuona  huruma  kwa kwenda  kutoa msaada. Nafikiri  hali  hiyo  inatokana  na historia  ya  vikundi  hivyo  kuwa ni vya kinyama  na vinatembea  na silaha mbalimbali  vikiwemo  visu , nyembe  na hata panga.

Bila  shaka  unyama  huo aliotendewa  binti  huyo  kwa mujibu wa  Chama  cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), ukatili  huo   unaangukia  katika  kundi la ukatili wa saikolojia  na unaweza kusababisha  mhusika  kujinyonga.

Hapo  ndipo nilipomuuliza  mmoja wa marafiki  wale  niliokuwa nao  sehemu ile  naye  akiwa ni mtoto wa mitaani, aliniambia  kuwa hali  hiyo ni ya kawaida  katika maisha yake  ya mitaani na wao  wameyazoea . Hapo ndipo nilipotaka kujua  msaada  wowote  wanaoupata  hasa kutoka kwa askari wa doria, ndipo  binti  huyo  aliyejitambulisha  kwa jina  Mary , ikiwa ni jina  la  bandia  nililompa  aliniambia  kuwa   hakuna  msaada  wowote  wanaoupata  kwa askari wanaokuwa doria, pindi  wanapofanyiwa vitendo  hivyo  katili

Hapo nilizidi kupata  picha nyingine  tofauti  kwa kujiuliza  inakuwaje  hata mamlaka za  usalama  kama  jeshi la polisi   kutotambua unyama  huo wa watoto  wa mitaani  ?. Kimsingi    kunakuwa na makundi mengi  ya watoto  hao wa mitaani, wanazidiana  kwa rika  na  umri, hivyo wale  wakubwa wanakuwa na sauti  dhidi  ya wale wadogo wanaoingia  kwenye  maisha  hayo.

Pia  uchunguzi wangu ulibaini  kuwepo kwa vyeo  ndani  ya makundi  hayo, kuna wanaojiita  King, ikiwa ndiyo  viongozi wa makundi, na kuna wale  wa ngazi  ya  kati wanaotumwa  na viongozi  wao hasa kwenda kufanya  uhalifu  sehemu  fulani na kuleta  watakachokipata  huko.

Katika  ukatili wa jinsia  makundi  hayo  yanahusika kwa kiasi  kikubwa, kwani  king  au  mtawala  anapohitaji  kufanya  tendo  la  ngono, basi atatoa  amri  ya kuletewa binti  katika  maskani  yake  na wale  wa kati watatekeleza jukumu  hilo  kwa kuhofia  kupatwa  na  adhabu kama watashindwa kutekeleza jukumu hilo.

Ni muda  muafaka  sasa  jamii  kusimama  na kuungana  na  Chama  cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania (TAMWA )kupinga  ukatili  huo  wanaofanyiana  watoto  hao wa mitaani .

Nazo  takwimu  za benki ya  dunia  zinaonyesha  kuwa  wanawake  wenye  umri  wa kuanzia  miaka  15 – 44   wapo  katika  hatari  kubwa  ya   kubakwa kuliko  kuugua  saratani, kupata   ajali , vita   na mlaria.

Pia  licha  ya  sheria  ya  nchi  inayoeleza kuwa endapo  mtu  atabainika kuhusika  kufanya  ubakaji  atahukumiwa  miaka  thelathini  jela, lakini  bado  vitendo  hivyo  vinaendelea, lakini  swali la msingi ni  nani  anasimamia vitendo  hivyo   kwa makundi kama watoto wa mitaani? Je watoto hao wa mitaani  wamepewa  elimu    ya  kuripoti  vitendo  hivyo  vya kinyama.

Wednesday, December 4, 2013

ZAWADI ZA BALIMI MBIO ZA MITUMBWI ZAWEKWA HADHARANI.

Meneja Mauzo na Usambazaji wa TBL, Kanda ya Ziwa , Malaki Sitaki(kulia) akimkabidhi kikombe Mwenyekiti wa Chama cha mbio za Mitumbwi Taifa, Richard Mgabo ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza wanaume katika fainali za mashindano ya mbio za mitumbwi yanayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki katika ufukwe wa  Mwaloni jijini Mwanza kwaudhamini wa Bia ya Balimi Extra Lager.Kushoto ni Mratibu wa Mashindano hayo, Peter Zacharia.
Mwanza.
KAMPUNI ya Bia Tanzania(TBL) kupitia Bia yake ya Balimi Extra Lager, leo imetangaza Zawadi za washindi wa mashindano ya mbio za mitumbwi zinazotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki, Desemba 7,2013, katika Ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja mauzo na usambazaji wa Kanda ya Ziwa, Malaki Sitaki alisema bingwa wa mashindano hayo wa mwaka 2013 upande wa wanaume ataibuka na kitita chafedha taslimu shilingi 2,700,000/=, Kikombe pamoja na medali za dhahabu.

Mshindi wa pili atazawadiwa fedha taslimu shilingi 2,300,000/=,mshindi wa tatu, 1,700,000/=, mshindi wa nne 900,000/= na washindi wa 5 hadi wa kumi watapatiwa kifuta jasho cha fedha taslimu shilingi 400,000/= kila kikundi.

Wakati upande wa wanawake bingwa ataibuka na zawadi ya fedha taslimu shilingi 2,300,000/=, Kikombe na medali za dhahabu, mshindi wa pili 1,700,000/=, mshindi wa tatu 900,000/=, mshindi wan ne 700,000/= na washindi wa 5 hadi 10 watapewa kifuta jasho cha fedha taslimu shilingi 250,000/=

Malaki alisema jumla ya timu 16 za wanaume na timu 11 za wanawake ziatarajia kuchuana siku hiyo na hatimaye kuwapata mabingwa wa mwaka 2013.

Aidha Malaki alivitaja vikundi vilivyotinga fainali upande wa wanaume kuwa ni Beach Boys Kigongo kutoka Kigoma, Dautius Kiiza kutoka Kagera, Katonga A kutoka Kigoma, Costantine Lusalago kutoka Mwanza, Leonard Kasunzu kutoka Mwanza, Toto Sebastian kutoka Ukerewe, Simon Fundi kutoka Ukerewe,  J.J.Buna kutoka Mara, Makila Camp kutoka Kigoma, Zaidock Kaiza kutoka Kagera, Daniel Mgenha kutoka Mwanza, Totoji Mazige kutoka Mara, Benidicto Chamba kutoka Mara, Bernadr Charles kutoka Mara, Emanuel Petro kutoka Kagera na mabingwa watetezi kikundi cha Eliud Prosper kutoka Kagera

Wakati upande wa wanawake ni kikundi cha Elizabeth Manoni kutoka Mara,Nyamiti Juma kutoka Mara,Muhate Mwocha kutoka Ukerewe,Jenifer Elias kutoka Ukerewe,Tabu Daudi kutoka Mwanza, Regina Kazungu kutoka Mwanza, Levina Costantine kutoka Kagera, Salome Ernest kutoka Kagera, Mwangongo Star kutoka Kigoma,Akina Mama Lemba kutoka Kigoma na mabingwa watetezi kikundi cha Nyamizi Deo kutoka Mara.

Mwenyekiti wa Chama cha wakimbia mbio za mitumbwi Taifa, Richard Mgabo aliishukuru kampuni ya Bia Tanzania kupitia Bia yake ya Balimi Extra Lager kwa kudhamini mashindano hayo na kuwaomba waendelee kudhamini kwani hamasa yake inazidi kukua mwaka hadi mwaka.

Aidha Mwenyekiti alimtaja Mkuu wa Mkoa wa jiji la Mwanza, Injinia Everisto Ndikilo ndiye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali hizo zitakazoanza kwa maandamano na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huyo.

Nae mratibu wa mashindano ya mbio za mitumbwi, Peter Zacharia  aliwaomba wapenzi, mashabi hususani wakazi wa Mwanza waje siku hiyo kushuhudia fainali hizo zitakazo sindikizwa na burudani lukuki ikiwemo Ngoma ya Bugobogobo ya Mang’ombe ga Kijiji kutoka Misungwi.

UKATILI WA BABA WAKWAMISHA NDOTO ZA MSICHANA JULIANA.

Msichana Juliana  akiwa nyumbani  kwake  akiandaa  chakula  kwa ajili  ya wateja  wake 
Na. Revocatus Herman
Tumeshuhudia   jamii   ikikumbwa  na ukatili  wa  kijinsia   hasa kwenye  vipigo, lakini  kwa msichana  Juliana  mambo yalikuwa ni  tofauti  yeye  ni  mtu   aliyeonja  ukatili wa kijinsia  katika  Nyanja  ya  kielimu. Baba mzazi wa Juliana aliamua makusudi kuelekeza ukatili wa kijinsia  kielimu kwa binti yake, fuatilia  makala  hii  yenye  simanzi  na masikitiko.
Baba   hakutaka nisome  kabisa, kwani kila mara  nilipomwambia kuwa nahitaji  kusoma aliniambia  kuwa, kusoma kwa mtoto wa kike  hakuna  maana  yoyote mtoto wa kike  ana jukumu moja  tu, ambalo nikuolewa. Alisema Juliana alipokuwa akinisimulia  kisa  chake huku akitokwa na machozi.
Juliana  aliniambia kuwa  kila  mara  alijitahidi  kumshawishi Baba  yake  juu  ya  yeye  kupelekwa   shule  lakini  Baba yake    alilirudia  kauli  yake  kuwa, kusoma ni wajibu wa mtoto wa kiume. Baba  yake Juliana  alikuwa na watoto  wane, watatu  wakiwa wanaume, kwa upande wa  watoto wa kiume wote walipelekwa shule  kasoro ni  Juliana  tu  ambaye alinyima  haki ya  kielemu.
Ni ukweli  usiopingika  kuwa  kunyimwa   kwa fursa  kwa Juliana  kulimfanya Juliana  awepo  hapo nilipomkuta, nilikutana  na Juliana katika  standi kuu  ya  mabasi  ya Nyegezi   Jijini Mwanza akiwa  ameketi  kwa hudhuni huku pembeni yake  kukiwa na sufulia  la uji wa ulezi aliokuwa akiuuza.
Kutokana na kuwa mapema  sana  asubuhi wateja  walikuwa  hawajafika  eneo  hilo, hivyo basi nilipata  nafasi  ya kumuuliza juu ya  maisha yake   yaliyomfanya ajikute kuwa mama lishe  au ntilie , hapo ndipo aliporejea  historia  yake ya miaka  kumi  iliyopita iliyojaa  uchungu  na masikitiko  ya ukatili wa kijinsia  katika  Nyanja  ya  elimu.
Juliana alisema kuwa  kaka  yangu namini leo  hii  na mimi ningekuwa kama  mama  Anne Makinda ambaye ni spika wa Bunge la Jamhuri  ya Muungano wa Tanznaia,  endapokuwa  baba  yangu  hasingenitendea  unyama  wa kijinsia kwa kuninyima  haki  ya kuwa na elimu  basi  ningekuwa mbali  kaka  yangu, lakini  ndiyo  hivyo  tena naishia  kwenye kuuza uji.
Juliana    aliniambia  kuwa,   kaka yangu   makubwa yalinipata  kwani  nakumbuka  mara  kwa mara  nilikuwa  namkumbusha  baba  juu  ya  kiu  yangu  ya  kusoma, lakini  kuna siku  sitaisahau, kwani  nilipomkumbusha  baba  juu  ya  suala hilo, aliishia  kunipiga  huku  akiniambia  nishike  kichwa  changu kwa mikono  miwili  na kumzunguka  alipokuwa  amesimama  bila  idadi  ya mzunguko.

Ikumbukwe kuwa  katiba  ya  jamhuri  ya muungano wa Tanzania  ibara  ya  13: 6 inasema ni marufuku   kwa mtu  kuteswa, kuadhibiwa   kinyama  au kupewa  adhabu  au kumdhalilisha. Mimi  naamini  kama mwandishi  natumia  nafasi  hii  kupinga  ukatili   wa kijinsia  hasa kwa kutumia  mbinu  za   za kuripoti   ukatili  wa kijinsia   kama  TAMWA walivyoamua  kuwajengea  uwezo  waandishi wa habari  kuripoti  matukio  hayo.

Chama  cha  wanahabari  wanawake  Tanzania  (TAMWA)  kimekuwa  kikipiga  kelele    huu  ya  ukatili wa kijinsia , lakini  bado  kuna maeneo jamii    inaendelea  na vitendo  hivyo.  Ni wazi  kuna   Msichana  Juliana  alinyimwa  haki  yake  ya kusoma kwa kuwa  tu  yeye  ni  msichana, huo  ni ukatili  mkubwa wa kijinsia.

Kwa sasa  Juliana  anaendelea  na biashara  yake  ya  mamaNtilie  na  amejiwekea  malengo  ya  kukusanya  fedha  kidogo kidogo  na mwakani  ana  mpango wa kuanza  kujiendeleaza  kielimu  kwa kupitia elimu  ya watu  wazima.
Makala hii  imewezeshwa  na TAMWA

Tuesday, December 3, 2013

HII NDIYO CLOUDS 14.

Clouds Fm ikiwa inatimiza miaka 14 katika game, G.Sengo Blog inakupa 'fursa' kuwatambua  Vijana wa kazi mjengoni na kwa leo wacha tuanzie hapa pichani ni Producer wa Jahazi Elikuda (Left) na Producer wa XXL Suddy Brown (Right).
Ni XXL hapa Adam Mchomvu aka Baba Jonii (Left) na Artist wa Bongo Flavour Abdu Kiba. (Right)
"We salute www.gsengo.blogspot.com"
Dj. Zero aka 'Zegho'.
XXL On air .
That's very fun my brother..
Like 'Spider man'
Meneja wa Vipindi Clouds Fm Sebastian Maganga (R) akiwa na mtangazaji wa Power Break Fast Babra Hassan.
Mmoja wa watangazaji wa Jahazi Mussa Hussein (R) na Mbwiga wa Sports Xtra na Power Break Fast wakishow love mbele ya kamera ya G.Sengo Blog...!!