ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 31, 2013

BANDARI ZA MWANZA KASKAZINI NA KUSINI ZACHAFULIWA NA MGOMO WA MAKULI WADUMU KWA MASAA 7 WAFANYABIASHARA WALAANI

Nje ya lango kuu la Bandari ya Kaskazini jijini Mwanza ambapo lango hilo lilifungwa kwasababu za usalama.
 BANDARI ya Mwanza Kaskazini na Kusini yachafuka ni kutokana na mgomo wa wafanyabiashara na watu wanaofanya shughuli za kubeba mizigo (Makuli)  kugomea kutozwa VAT mala mbili ya kupakia na kupakua mizigo yao, ushuru na makato mengine na kusababisha shehena ya mizigo kutoka Bukoba kukaa ndani ya meli kwa masaa 7 Bandarini hapo Jijini Mwanza.

Sakata hilo lilitokea jana kuanzia majira ya saa12:30 na kudumu hadi saa 7:00 mchana baada ya Meli ya Mv Victoria kuweka Nanga  kwenye Bandari ya Mwanza Kaskazini kufatia Mamlaka ya Bandari nchini( TPA) kutoa maelekezo kwa uongozi wa TPA Mwanza kuwa muda wa mzabuni aliyekuwa akifanya kazi za kupakia, kupakua na kutoza ushuru wa mizigo kumaliza muda wake na kazi hiyo kufanywa na Mamlaka hiyo.
Askari wamezingira lango kuu la Bandari ya Kaskazini jijini Mwanza ambapo lango hilo lilifungwa kwasababu za usalama.

Askari akilinda lango kuu kuzuia watu wasitinge bandarini ambapo shughuli zote za huduma na biashara zimesimama.

 Akizungumza wakati wa kutekeleza mgomo huo Mwenyekiti wa Ushirika wa Wahudumu wa Bandari ya Mwanza Kaskazini na Kusini Rajabu Said alisema kuwa wao waliokuwa wazabuni wa kufanya shughuli za kupakia, kupakua na kutoza ushuru wa mizigo Bandarini hapo kugomea  na TPA kuendelea na kazi hizo kutokana na muda wa miaka miwili waliokuwa wamepewa kumalizika na kutakiwa kutjishughulisha tena.

Mwenyekiti Said alieleza kuwa kutokana na Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) kutoa mwongozo wa ukusanyaji mapato na ushuru baada ya kumalizika kwa muda wa USHIRIKA wa miaka miwili uliokuwa umetolewa kwa zabuni ambayo walishinda mwaka 2011 hadi kumalizika Agosti 30 mwaka huu aligubikwa na mizengwe na kuwa na usiri na kutowekwa bayana na viongozi wa TPA Mwanza.

Mwenyekiti Said akizungumza na chombo cha habari.
 “Muda wetu umekisha kama mzabuni aliyekuwa na tenda ya kufanya kazi Bandari ya Mwanza Kaskazini na Kusini lakini TPA hawajatangaza Tenda upya na walipotuita viongozi wa Ushirika na TPA kwenye kikao cha pamoja walidai kutupatia muda wa mwezi mmoja zaidi ili kutangazwa Tenda upya kumpata mzabuni atakayeshinda kufanya kazi hizo” alisema Said na kuongeza kuwa.


Baada ya Kikao hicho kumalizika kwa makubaliano yaliyoafikiwa  jambo la kushangaza asubuhi ya leo Agosti 31 mwaka huu wakati tulipofika Bandarini Mwanza Kaskazini tulikuta utaratibu mpya kwa walinzi wa Kampuni ya Ulinzi ya SUPREM na kuteleleza kuwa haturuhusiwi kufanya shughuli za kutoza ushuru, kutoza mizigo tutakayo pakua leo Jumamosi (Jana) na kupakia Jumapili na kazi hiyo iko chini ya TPA kuanzia sasa.

Said alisema baada ya taarifa hiyo tulipinga na kuwataka wafanyabiashara wa kutoka Mjini Bukoba kuacha kushusha mizigo hiyo hadi muafaka upatikane na wao waliafiki kwa kutuunga mkono kutokubaliana na uongozi wa TPA kwa vile ulilenga kuwatoza fedha zaidi kwa kulipia VAT mala tano kwa mizigo yao ikiwa ni kupakia kulipa VAT asilimia 18 kwa Marine na TPA ikiwa na kushusha na tozo la fedha za Makuli hao.

“Hatukubaliani na kabisa na kilichofanywa na uongozi wa TPA kwani zabuni haijatangazwa nasi tukapata kutuma maombi yetu lakini imedaiwa kuwa kuna Chama cha Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo (TPA) Mwanza (DOWUTA) wamekisajili ili kuchukua nafasi ya Ushirika kufanya kazi hiyo na ndiyo maana Tenda hawajaitangaza na tumeelezwa na uongozi kuna mzabuni tayari nasi tumepinga na kugomea kukubaliana na utaratibu huo hivyo Bandari zote Makuli tumeomba uwazi uwepo na tenda zitangazwe” alisisitiza.

Ushirika huo wenye jumla ya wanachama 3000 na ulisajiliwa na kufanya kazi hizo Bandari za Mwanza Kaskazini na Kusini baada ya kushinda zabuni hiyo mwaka 2011 ulipunguza tatizo la ajira na kuwafanya wanachama hao ambao ni wafanyakazi wa kubeba mizigo wamekuwa na utaratibu wa kukopeshana, kuchaniana kwa matatizo ya ugonjwa na kutoa fedha kwa mwanachama anayefariki na wanaositaafu kubeba mizigo hulipwa milioni 1.5 ikiwa na hisa yake ya uanachama hivyo kutopewa kazi hiyo imedaiwa kuongeza watu kujihusisha na uhalifu mitaani na kuweka mashaka kwa wasafiri na mizigo yao kuanza kuibiwa na watu kwa kukabwa nakati za usiku na asubuhi.

Mizigo imedoda melini hakuna wapakuaji.

Ile hali meli ikiwa imejaa mizigo na bidhaa za ndizi baadhi ya wafanyabiashara waliamua wenyewe kupakua mizigo.


Vuta nikuvute nje ya lango la Mamlaka ya Bandari.

Baada ya vuta ni kuvute kutoka kwa wafanyabiashara na uongozi wa TPA Mwanza na Makao Makuu iliyotuma wawakilishi wake kujadiliana na kuona jinsi ya kumaliza mvutano huo na kumaliza mgomo wa Makuli hao na kupelekea kuibuka Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Huduma wa TPA Clementi Kiloyavaha na kueleza kuwa utaratibu uendelee kwa leo kama ilivyokuwa wakati wakianda Kikao cha pamoja.

Kiloyavaha alisema kwamba kutokana na maelekezo kutoka kwa Waziri wa Uchukuzi Dr.Harison Mwakyembe kwa Mamlaka hiyo ya TPA wamepewa utaratibu na hivyo utaanza kutekelezwa kuanzia Septemba mosi na kunachotakiwa kufanyika ni kikao cha pamoja baina ya wadau wa TPA na Wafayabiashara wanaotumia Bandari za Mwanza Kaskazini na Kusini kuwapa utaratibu mpya.

Kwa upande wa wafanyabiashara baadhi yao waliozungumizia sakata hilo na kukataa kutajwa majina yao walisema kuwa wao wanapinga kutozwa VAT asilimia 18 kwa kila tani moja na vifurushi wakati wa kupakia na kupakua mala mbili ikiwa ni kwa Kampuni ya Meli ya Marine na Mamlaka ya Babdari TPA pamoja na kutozwa VAT ya fedha za vibarua wa kupakia na kupakuwa wanayolipia kuwa ni kero kubwa kwao.

“Hili litatufanya kuacha kupitisha mizigo yetu katika Bandari hizi za TPA kwa vile utaratibu huu umelenga kuturudisha nyuma na kutukamua zaidi na kukosa faida kabisa na leo tumepoteza wateja na tutauza ndizi,mihogo na matunda kwa bei ya hasara na hili limetukera sana nibora wangetuarifu kwa matangazo badala ya kukurupuka na kuamua hata kama ni maagizo ya Waziri Mwakyembe” walisema .


Hali ililejea majira ya saa 7:00 mchana makuli na wafanyabiashara kuendelea na utoaji wa bidhaa zao na kupakia baada ya kuishusha ili iliyotoka Mji wa Bukoba na kusababisha mgomo wa masaa 7 na kuasilika kwa makundi ya wafanyabiashara wa ndizi mbivu na mbichi, matunda na mihogo katika masoka mbalimbali ya Jiji la Mwanza kama ilivyozoeleka Meli ya Mv Victoria inapofika Jijini Mwanza toka Mjini Bukoba.

WAKAZI WA MTWARA WAIPOKEA KWA SHANGWE SEMINA YA FURSA KWA VIJANA HII LEO

Meneja Kiongozi,Uhusiano NSSF Makao makuu jijini Dar,Eunice Chiume  akizungumza mapema leo kwenye semin ya FURSA iliyofanyika kwenye ukumbi wa Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana Mtwara, kulia ni Meneja wa NSSF mkoani Mtwara Bwa.Stanley Mullanzi na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Vipindi Clouds Media Group, Ruge Mutahaba pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iramba (ambaye pia ni mzaliwa wa Newala mkaoni Mtwara), Mh.Yahya Nawanda wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa ukumbini humo.

Semina hiyo inaratibiwa na Clouds Media Group na kufadhiriwa na NSSF,Lake Oil,Zantel,MaxMalipo na wengineo imewashirikisha wadau mbalimbali wa Mtwara na vitongoji vyake wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
  Baadhi ya Wakazi wa Mji wa Mtwara na vitongoji vyake wakifuatilia kwa makini  yaliyokuwa yakijiri kwenye semina ya Fursa kwa Vijana iliyofanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa  Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana mkoani Mtwara.
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba (ambaye pia ni mzaliwa wa Newala mkaoni Mtwara),Mh.Yahya Nawanda akizungumza na wakazi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kwenye semina ya Fursa kwa Vijana mapema leo, Mh.Yahya alizunguma mengi zikiwemo fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya mkoa wa Mtwara na Singida namna ya kuzifanyia kazi katika suala zima la kujikwamua na maisha. 
Mkurugenzi wa Vipindi Clouds Media Group,Ruge Mutahaba  akihitimisha semina ya Fursa kwa Vijana mapema leo mchana,ndani ya ukumbi wa ukumbi wa Pentecoste Ligula B,uliopo mkabala na Kituo cha Vijana Mtwara,kulia kwake ni Meneja Kiongozi,Uhusiano NSSF Makao makuu jijini Dar,Eunice Chiume pamoja na Meneja wa NSSF mkoani Mtwara Bwa. Stanley Mullanzi.

Semina ya Fursa kwa vijana tayari imekwishafanyika mikoa ya Tabora,Kigoma,Singida na sasa Mtwara.
PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPO.COM

Friday, August 30, 2013

MWILI WA ASKOFU KULOLA KUWASILI JIJINI MWANZA KESHO

Dar es Salaam. Mwili wa Askofu Kulola utasafirishwa kutoka jijini Dar es salaam hadi jijini Mwanza kesho Jumamosi ya tarehe 31/08/2013 majira ya jioni kwa ndege mara baada ya kuagwa katika kanisa la EAGT Temeke. Atazikwa kwenye Uwanja wa Kanisa la EAGT Bugando.

Vilio, simanzi na maombi ya kunena kwa lugha vilitawala jana katika Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Temeke Dar es Salaam wakati waumini na ndugu wa Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Dk Moses Kulola (83) walipopata taarifa za kifo cha kiongozi huyo.
Katibu Mkuu wa EAGT, Brown Mwakipesile alisema kuwa Askofu Kulola alifariki dunia jana saa tano asubuhi kwenye Hospitali ya Africa Medical Invesment (AMI), Dar es Salaam.
Mwakipesile alisema afya ya Askofu Kulola ilianza kubadilika Mei mwaka huu akiwa mkoani Mwanza ambako alipelekwa Hospitali ya Rufaa Bugando ambako alibainika kuwa na matatizo ya moyo.
Alisema kifo hicho kimeacha pengo kubwa ambalo haliwezi kuzibwa kwa sasa. Hata hivyo, wanafarijika kwa upande mwingine wakiamini kwamba Mungu amemchukua mtumishi wake kwa wakati alioukusudia.
Askofu Kulola ni mmoja wa viongozi wa dini waliokuwa na jina kubwa nchini na alifanya kazi za utumishi wa kanisa kwa miaka 53 kwa kuhubiri na kuwaombea wenye matatizo mbalimbali.
Mtoto wa kwanza wa askofu huyo, Goodluck Kulola alisema wamejifunza mambo mengi katika maisha ya baba yao, ikiwamo upendo na unyenyekevu ulioongozwa na uchaji Mungu.
Askofu Kulola ameacha mke wake aitwaye Elizabeth, ambaye alibarikiwa kupata naye watoto 10 na wengine wawili wa kuasili. Hata hivyo, watoto watatu walishafariki dunia. Ameacha wajukuu 44 na vitukuu 10.
Askofu Kulola, ambaye alizaliwa 1928, alianza Shule ya Misheni ya Ligsha Sukuma mwaka 1939, baadaye alijiunga na Shule ya Bwiru kabla ya kusomea Usanifu Majengo huko Israel kisha kuanza kazi ya kumtumikia Mungu mwaka 1950.
Alifuzu Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Theolojia katika Chuo Kikuu cha California State Christian Marekani.

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA BIMA TANZANIA YATOA MSAADA KWA KITUO CHA NYUMBA YA WATOTO WAB AFRICA MWANZA

Kamishna wa Bima nchini Israel Kamuzora (kushoto) akikabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vikiwemo vyakula, vuandarua na mashuka katika kituo cha Kulelea watoto yatima cha Nyumba ya watoto wa Afrika kilichopo eneo la Igoma jijini Mwanza.
Wadau wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima (TIRA) walitoa vitu vifuatavyo:-
 Sukari kilo 100
Mchele kilo 100
Unga wa Sembe kilo 100
Vyandarua 100
Shuka pea 100 ambapo ni idadi ya shuka 200
Biskuti kwaajili ya chai na viburudisho vya soda
Vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 3.2
Wafanyakazi na viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Tanzania wakishusha msaada wa vifaa mbalimbali vikiwemo vyakula, vuandarua na mashuka katika kituo cha Kulelea watoto yatima cha Nyumba ya watoto wa Afrika kilichopo eneo la Igoma jijini Mwanza.

Ni vyakula kwa kituo..

Ni wadau wawakilishi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima kutoka mikoa ya Zanzibar, Arusha, Dar, na Mwanza.

Matandiko kama shuka na neti ni sehemu ya msaada.

Ni Biskuti kama viburudisho kwa watoto.

Sukari kilogram 100 kwaajili ya kituo.

Kamishna wa Bima nchini Israel Kamuzora amesema kuwa dhumuni la ujio wao jijini Mwanza ni kuhamasisha suala la Umuhimu wa Sekta ya Bima ambapo watoto wanapata fursa ya kuishi bila wasiwasi mara baada ya wazazi wao kufariki dunia either kupitia maradhi au harakati mbalimbali za maisha. 
Wafanyakazi na viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Tanzania wakigawa vinywaji kwa watoto wa kituo cha cha kulelea watoto yatima cha Nyumba ya watoto wa Afrika kilichopo eneo la Igoma jijini Mwanza.

Wafanyakazi na viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Tanzania wakigawa vinywaji na pipi kama viburudisho kwa watoto wa Kituo cha cha kulelea watoto yatima cha Nyumba ya watoto wa Afrika kilichopo eneo la Igoma jijini Mwanza.

Hakika ilikuwa siku yao njema kufurahi pamoja kwa watoto wa kituo hiki kilichoanzishwa zaidi ya miaka 15 iliyopita, ambapo kwa sasa kina watoto 108.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Tanzania walipata fursa ya kuzungumza ana kwa ana na watoto wa Kituo cha cha kulelea watoto yatima cha Nyumba ya watoto wa Afrika

Kila mmoja na mtoto wake.

Furaha na watoto.

Picha ya Group.

Neno la shukurani kwa mapokezi yaliyoonyeshwa na watoto na uongozi wa kituo kwa wadau wa Usimamizi wa Shughuli za Bima.

Bango la kituo cha nyumba ya Kituo cha kulelea watoto yatima cha Watoto wa Africa.

DIAMOND AMFANYIA SUPRISE MZEE GURUMO KWENYE UZINDUZI WA VIDEO YAKE,AMPA GARI KAMA SHUKRANI YA MCHANGO WAKE KWENYE SANAA YA MUZIKI NCHINI TZ.

Nikikutajia Jina la Muhidini Gurumo
 basi utajua namzungumzia nani.
Nguli wa muziki wa Dansi nchini Tanzania.....
Takribani wikii imepita toka kusikika
kwa habari za kweli kuhusu kustaafu
muziki kwa Mzee Gurumo,binafsi sikuwahi 


kukutana nae hadi leo hii nilipokutana nae
kwenye uzinduzi wa Video yangu.
Nilimualika mzee huyu kwa mapenzi yote,niliskia
 juzi pia akisema amekuwa akipendezwa na
style ya muziki wangu na kucheza pia hayo ni moja wapo ya mambo pia
yaliyonivutia kutaka kumuona mzee huyu.
Nilipitia kwenye mitandao mingi uku ikiandikwa
kusemekana kutokana na kalui ya mzee
Gurumo ameweza kuwa kwenye fani zaidi
ya miaka 50 lakini akuwahi bahatika hata kuwa na Baiskeli....

Jambo ili lilinigusana na kuniumiza moyoni,
kuona nguli kama huyu wa muziki
kunena vile na kuomba msaada,
Binafsi leo usiku nimemtunuku Gari
Mpya mzee Gurumo kwenye uzinduzi wa Video yangu.

Nimeamua kutoa kwa moyo mmoja na
 kwa mapenzi yangu yote kwa mzee wangu.
Tukio ili limetokea tarehe 29.0.2013
nimeamua kukuwekea picha kadhaa
jinsi hali ilivyojri mara tu ya kumalizika
 kwa Launching ilikuwa
suprise kwa mzee wangu Gurumo....
By Diamond.

Mzee Gurumo akionesha Ufunguo juu baada ya kukabidhiwa Gari kama
zawadi toka kwa Diamond....
Furaha iliyoje ndani ya Moyo wangu (Diamond) kupewa baraka na Mzee wangu.....
Sauti yake tu.....Iliwafanya wageni wote kuimba nae muda huu....
Safari kuelekea Nje ya ukumbi kwa makabidhiano.....
Pembeni ya Diamond (kulia) ndio Gari alilomchukulia Mzee Gurumo.....

Habari zote zisome kwa kina zaidi kupitia: http://www.thisisdiamond.com/

Thursday, August 29, 2013

MAONYESHO YA NANE YA BIASHARA YA AFRIKA MASHARIKI KUANZA RASMI KESHO KATIKA VIWANJA VYA NYAMAGANA JIJINI MWANZA

Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara wa Viwanda na Kilimo Elibariki Mmari (katikati)  akizungumza na vyombombalimbali vya habari kuhusu ujio wa Maonyesho ya nane ya Biashara ya Afrika Mashariki, kulia ni Muweka hazina wa TCCIA Mwanza Bw. Majid Igangula na kulia ni Makamu mwenyekiti wa TCCIA Mwanza Bw. Leopard Lema . 
Maonyesho ya NANE ya Biashara kwa nchi za Afrika Mashariki (EastAfrica Tarade Fair) yanayoandaliwa na TCCIA mkoa wa Mwanza yanataraji kuanza rasmi  tarehe 30/08/2013  mpaka tarehe 8/09/2013 katika viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza yakihusisha makampuni mbalimbali ya bidhaa ndani na nje ya nchi.

Licha ya Maonyesho hayo kutumika kama jukwaa kwa makampuni mbalimbali ya ndani  na nje kuonyesha shughuli na huduma wanazozitoa pia itakuwa ni fursa ya yatatumika kama fursa ya kuanzisha mitandao katika dhana ya usambazaji wa bidhaa.


Mbali na kushirikisha wadau wa biashara, viwanda na kilimo wa nchi za Afrika Mashariki pia maonyesho hayo yatashirikisha makampuni ya wadau wa nchi za Misri, Singapole na China.


Bidhaa na huduma zisizoruhusiwa kwenye maonyesho hayo ni pamoja na Silaha za aina zote, Risasi, Mizinga (Bidhaa za kivita), pamoja na huduma za masuala ya  kisiasa na kidini kwani ni Biashara na Uwekezaji tu ndiyo umezingatiwa na kamati ya maandalizi

Maonyesho hayo yatazinduliwa nnamo tarehe 2 September 2013, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo.

BAADA YA KUMALIZA KIFUNGO KWANEEMA FM YA JIJINI MWANZA YAREJEA HEWANI

Kituo cha Radio ya Injili Kwaneema Fm cha jijini Mwanza  ambacho mapema mwaka huu kilifungiwa na kuamriwa na serikali ya Tanzania kupitia TCRA  kusitisha urushaji wa matangazo yake kwa muda wa miezi 6, kutokana kutuhumiwa kuhusika na uchochezi wa kidini hususani katika suala tata la uchinjaji wa kitoweo cha nyama hatimaye muda wa kifungo hicho umemalizika na kituo hicho tayari kimeanza kurusha matangazo yake kwa mara nyingine tena.

Kwaneema Fm inarejea hewani ikiwa bado mmiliki wa kituo hicho Askofu Bishop Mpemba anasakwa na jeshi la polisi Mwanza na huku akiwa hajulikani wapi alipo.

Bishop huyo anakabiliwa na mashtaka ya kujibu  kwa kuchapisha DVD inayoitwa 'INUKA CHINJA ULE' inayotajwa kuwa na uchochezi wa kidini ndani yake.

Radio Kwaneema Fm 98.20 Mhz ya jijini Mwanza imeanza kusikika hewani kuanzia jana Jumatano August 28/2013 majira ya saa 11alfajiri chini ya masharti waliyopewa na TCRA.

MISS TANZANIA BRIGITTE ALFRED AKABIDHIWA BENDERA TAYARI KUTINGA MISS WORD 2013 NCHINI INDONESIA

Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara (wa pili kulia) akitoa nasaha zake kwa Warembo wanaowania taji la Redd's Miss Tanzania 2013, wakati wa hafla ya Chakula cha jioni ikiwa ni sehemu ya kumuaga Redd's Miss Tanzania 2012/13, Brigitte Alfred (pili kushoto) anaetarajiwa kuondoka hivi karibuni kwenda nchini Indonesia kushiriki Mashindano ya Urembo wa Dunia (Miss World). Hafla hiyo imefanyika usiku huu kwenye Hoteli ya Giraffe, Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni kutoka wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Herman Mwasoko na kushoto ni Mlezi na shoto ni Mlezi wa Kamati ya Miss Tanzania,Mh. Emmanuel Ole Naiko.
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara (katikati) akimkabidhi Bendera ya Taifa,Redd's Miss Tanzania 2012/13,Brigitte Alfred (pili kushoto) anaetarajiwa kuondoka hivi karibuni kwenda nchini Indonesia kushiriki Mashindano ya Urembo wa Dunia (Miss World 2013).Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni kutoka wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Herman Mwasoko (pili kulia),Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kulia) pamoja na Mlezi wa Kamati ya Miss Tanzania,Mh. Emmanuel Ole Naiko.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania,Hashim Lundenga akimuaga Redd's Miss Tanzania 2012/13,Brigitte Alfred (katikati) mara baada ya kukabidhiwa Bendera ya Taifa na Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara  (kulia) wakati wa hafla ya Chakula cha jioni kwa ajili ya kumuaga Mrembo huyo,iliyofanyika kwenye Hoteli ya Giraffe,Jijini Dar es Salaam usiku huu.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania,Hashim Lundenga akizungumza machache ikiwa ni pamoja na kuwaasa Warembo waliopo kambini hivi sasa kujitahidi kufanya vyema.

Mlezi wa Kamati ya Miss Tanzania,Mh. Emmanuel Ole Naiko akiongea machache kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kuzungumza.

Mkurugenzi Mkuu wa Hoteli ya Giraffe,Dkt. Charles Bekoni akitoa salamu.

Redd's Miss Tanzania 2012/13,Brigitte Alfred akikumbatiana na Mama yake Mzazi wakati wa Kumuaga.

Redd's Miss Tanzania 2012/13,Brigitte Alfred.
Redd's Miss Tanzania 2012/13,Brigitte Alfred akitoa shukrani zake wakati wa hafla hiyo ya kumuaga iliyofanyika usiku huu kwenye Hoteli ya Giraffe,jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania 2013 wakiwa kwenye hafla hiyo.
Sehemu ya Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania 2013 wakiwa kwenye hafla hiyo.Picha zote na Othman Michuzi