ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 16, 2013

CHEKSHIA DANSI LA AZONTO NA DJIBRIL CISSé KWENYE KINYANG'ANYIRO CHA KUMSAKA MNYANGE WA RDC UK.


Mc: "Huyu ni Gjibril Cisse anayekiputa kwa mkopo katika klabu ya Al-Gharafa akitokea Queens Park Rangers kama mshambuliaji. Anapiga pamba za uhakika, kwetu Kongo tunaita 'Sapele' (kibongobongo ametokelezea)." 
Mc: "Nataka kusema kitu cha utofauti ambacho nakiona kwake, wewe sawa unaasili ya afrika na haujazaliwa Afrika bali umezaliwa Ufaransa, kuna watu wengi sana hata humu ndani ambao wanaishi hapa uingereza, ni waafrika waliozaliwa na waafrika na wazazi wao wako Afrika, lakini hawajui kabisa tamaduni zao."  "Nataka kujuwa wewe umewezaje kukonect na kuzimudu tamaduni za Afrika wakati wewe ni mfaransa, umefanya nini hasa?" 

Gjibril: Kiukweli nimekuwa nikitembelea mila na tamaduni mbalimbali duniani, mwisho wa siku nimegundua kuwa Afrika kuna utamaduni wenye nguvu zaidi ya zote na hata ninapotembelea bara la Afrika najihisi kuwa niko mahala pa upekee zaidi".

Ni katika kinyang'anyiro cha kumsaka Miss RDC UK mwaka 2012.

Friday, March 15, 2013

'WACHA MACHO YAPEPESE MWAMAWANE'

Jina la burudani ya kale radio ya watu.

Ni kiota cha P Funk au cha Rastafarian mmoja?

Sio ya Dar bali ya Zoo.....

Hata wao wanasoma habari...

Maji safi tena salama ya kunywa usiyo hitaji kuchemsha BUReEEEee... kwa hisani ya TBL.

BAR 5 KUSHINDANISHWA JUMAPILI HII KATIKA SAFARI LAGER NYAMA CHOMA COMPETITION MWANZA

Meneja wa Bia ya Safari Oscar Shelukindo (katikati) akifafanua kuhusu shindano la Safari Lager nyama choma competition kwa jiji la Mwanza wengine katika picha ni Meneja mauzo wa bia ya Safari Lager Kanda ya Ziwa Malaki Sitaki (kushoto) na jaji wa shindano hilo Deogras Sakibu.
Shindano la uchomaji nyama kwa bar mbalimbali nchini linalojulikana kwa jina la Safari Lager Nyama choma Competition wiki hii katika siku ya jumapili linahamia mkoani Mwanza katika viwanja vya Furahisha.

Kwa mujibu wa meneja wa Bia ya safari Oscar Shelukindo amesema kuwa lengo la mashindano hayo ambayo yanatimiza miaka 6 sasa tangu kuanzishwa kwake ni kuboresha Afya za walaji ambao ni wananchi kwa kuzingatia ubora na kanuni za afya.

Vilevile Shindano hilo la nyama choma limenuia kuongeza uelewa kwa waandaaji wa nyama choma nchini.

 Jaji wa shindano la Safari Lager Nyama Choma 2013 Deogras Sakibu akitoa maelezo ya jinsi washindi wanavyopatikana vigezo na sifa zao huku akisikilizwa kwa umakini na meneja wa Bia ya Safari Oscar Shelukindo .
Shindano hilo la nyama choma linatoa uelewa kuanzia vifaa bora vya kutumia wakati wa kuandaa nyama choma, moto utakaotumika, waya malum wa kuchomea nyama, usafi wa mchomaji mwenyewe na uchangamfu wake kwenye biashara.
Jaji wa shindano la Safari Lager Nyama Choma 2013 Deogras Sakibu akitoa maelezo ya jinsi washindi wanavyopatikana vigezo na sifa zao huku akisikilizwa kwa umakini na meneja wa Bia ya Safari Oscar Shelukindo pamoja na meneja mauzo wa bia ya Safari Lager Kanda ya Ziwa Malaki Sitaki
"Mwezi uliopita mwishoni nilikuja kuendesha semina elekezi ambayo tuliongelea vigezo na taratibu zote ambazo zinahusiana na uchomaji wa nyama kwa washiriki wa shindano pamoja na wengine wa baa mbalimbali ambao walijitokeza kwa wingi ili kupata nafasi kujifunza mbinu mbalimbali  na kanuni zake kuboresha suala zima la uchomaji nyama hivyo ni yangu matumaini si siku nyingi mtaona mabadiliko ya ubora kwa bar nyingi za hapa jijini Mwanza" alisema Sakibu ambaye ni jaji wa shindano hilo.

Meneja mauzo wa bia ya Safari Lager Kanda ya Ziwa Malaki Sitaki akizitaja zawadi.
Pamoja na promosheni mbalimbali zitakazofanyika kwenye viwanja vya Furahisha Kirumba na viburudisho mbalimbali, Zawadi kwa washindi itakuwa kama ifuatavyo:- 
Mshindi wa Kwanza atajipatia kitita cha shilingi milioni 1,
Mshindi wa pili shilinhi laki 8,
Mshindi wa tatu shilingi laki 6,
Mshindi wa nne shilingi laki 4, na 
Mshindi wa tano shilingi laki 2.

Wakazi wa Mwanza na vitongoji vyake wameombwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia ni baa ipi itanyakuwa ushindi katika Safari Lager Nyama Choma Competition mkoa wa Mwanza huku wakipata ladha safi ya bia ya Safari iliyonyakuwa hivi karibuni tuzo za Bia bora Afrika katika mashindano yaliyofanyika Acra nchini Ghana.

BANDARI YAITAFUNA FALCON 2-0 LIGI KUU ZANZIBAR

Mchezaji wa Falcon (kulia) akimkwatua mshambuliaji wa Bandari katika pambano la ligi kuu ya Grand Malt ya Zanzibar kati ya Bandari na Falcon kwenye uwanja wa Amaan mjini Zanzibar jana. Bandari iliisambaratisha Falcon mabao 2 - 0..


Mlinzi Rashid Omar wa Bandari (kulia) akimzuia mshambuliaji wa Falcon, Mbarouk Marshed asiende na mpira katika pambano la ligi kuu ya Grand Malt ya Zanzibar kati ya Bandari na Falcon kwenye uwanja wa Amaan mjini Zanzibar jana. Bandari iliisambaratisha Falcon mabao 2 - 0.
Picha zote na Martin Kabemba.

HII HAPA VIDEO ILIYOMUWEKA MATATANI MKUU WA USALAMA CHADEMA



Lwakatare alikamatwa juzi makao makuu ya chama hicho na kupelekwa katika Makao Makuu ya Polisi kwa mahojiano.

Bakari Kiango na Nuzulack Dausen, MWANANCHI
Polisi wamezidi kumbana Mkuu wa Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare baada ya kupekua nyumbani kwake kwa siku ya pili mfululizo.

Lwakatare, ambaye ni mbunge wa zamani wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CUF, alikamatwa juzi mchana kwa kutuhumiwa kwa kufanya uchochezi wa uvunjifu wa amani baada ya kunaswa kwenye picha ya video iliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii.

Upekuzi wa pili
Nyaronyo Kicheere, ambaye ni Mwanasheria wa Lwakatare, aliliambia gazeti hili jana kuwa mteja wake, ambaye anashikiliwa na polisi hao, alipelekwa nyumbani kwake Kimara-King’ong’o jijini Dar es Salaam kwa ajili ya upekuzi huo.

Ilikuwa mara ya pili kwa Lwakatare kupekuliwa kwani mara ya kwanza ilikuwa juzi jioni baada ya kuhojiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi. Lwakatare, ambaye alitolewa Kituo cha Kati cha Polisi, alipelekwa jana kwa msafara wa magari mawili ya polisi chini ya ulinzi mkali.

Nyaronyo alisema kuwa msafara huo uliondoka saa 10.00 jioni kwa ajili ya safari hiyo ya Kimara wakitokea katikati ya Jiji la Dar es Salaam kilipo Kituo cha Kati cha Polisi. Alisema kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya kikao kizito kati ya maofisa wa Idara ya Upelelezi (DCI) na wale wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP).
“Hawa watu walikuwa na kikao kirefu siku nzima ya leo (jana) nadhani walikuwa wanaangalia kama kuna uwezekano wa kumshtaki au la mteja wangu.Walipomaliza kikao waliamua turudi tena nyumbani kwa Lwakatare ili kuendelea na upekuzi,” alieleza Kicheere.

Kama ilivyokuwa juzi, upekuzi kwa Lwakatare uliongozwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Obadia Jonas.

Polisi wanasemaje
Msemaji wa Polisi, Advera Senso alisema kuwa bado wanaendelea kumshikilia Lwakatare huku wakiendelea na uchunguzi wa suala hilo. “Kama kukiwa na taarifa za ziada nitawajulisha msiwe na wasiwasi,” alisema Senso na kukata simu.

Lwakatare alikamatwa juzi saa saba mchana katika makao makuu ya chama hicho na kupelekwa katika Makao Makuu ya Polisi kwa mahojiano.

Juzi siku nzima mitandao ya kijamii ilikuwa imetawala na habari picha ya video ikimwonyesha Lwakatare akidaiwa kupanga mikakati ya kumteka Mhariri Mtendaji wa Mwananchi, Dennis Msacky kwa madai kuwa anashirikiana na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, kutengeneza migogoro.
Pia, Lwakatare alionekana akitoa maelekezo kwa watu , ambao sura zao hazikuonekana, akiwataka kufuatilia nyendo za Msacky.

Chadema wapinga
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema mkanda wa video unaoonyeshwa kwenye mitandao ya kijamii ukimwonyesha Lwakatare akipanga njama za uhalifu hauna uhalisia na kwamba huo ni uzushi ulioratibiwa na kufanikishwa na vyombo vya dola.
Pia Dk Slaa alidai kuna mpango mwingine kabambe unaofanywa na idara za dola kuhakikisha kuwa Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa anakamatwa kutokana na sumu anazotema bungeni na kwingineko dhidi ya Serikali.

Dk Slaa alisema kuwa taarifa za kuwapo njama za kukichafua chama chake kupitia mkanda huo wa video alizipata kutoka ndani ya Serikali Jumatatu iliyopita hata hivyo, wakati akiendelea kupanga mkakati wa kushughulikia tayari ulikuwa umeshaingizwa katika mitandao ya kijamii.

Thursday, March 14, 2013

TGNP YASHINDA KESI YA JENGO MAHAKAMA KUU

Jengo lenyewe la TGNP.


Usu Mallya
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), walinunua  jengo la ofisi hii kutoka kwa Mfilisi wa iliyokuwa Tanzania Sewing Thread Manufacturers Limited (TSTML) yaani Benki ya Rasilimali ya Tanzania mnamo tarehe 15th June, 1997.
Wapangaji wasiohalali walikwenda mahakamani wakiwashitaki Benki ya Rasilimali ya Tanzania pamoja na TGNP na kesi ilifunguliwa tarehe 16th July 1997 kesi ilipewa Na. 215/1997. Madai ya washitaki yalikuwa yafutayo:
    a)        TGNP ilipendelewa katika mchakato mzima wa tenda ya manunuzi ya jengo hili na kwamba TGNP hawakuwa wazawa.
   b)        Utoaji wa tenda kwa upande wa Beki ya Rasilimali Tanzania ulikuwa batili kwa sababu haukufuata/haukuzingatia sheria ya nchi ya manunuzi na hivyo kukiuka haki za kimsimgi (failure to observe the law, public policy and the rules of natural justices)

TGNP kama washitakiwa walishinda kesi hiyo ya  madai namba 215/1997 iliyofunguliwa na waliokuwa wapangaji. Jengo lenye kesi ni jengo la gorofa moja zilipo Ofisi za Makao Makuu ya Shirika Mabibo Dar es salaam.

Chini ya Mhe. Jaji T.B. Mihayo, 15 Oktoba 2009, TGNP Ilishinda kesi hiyo na walalamikaji walidai kuwa TGNP imependelewa. Oktoba 19, 2009, walifungua rufaa katika makahakama kuu ya Rufaa ya Tanzania, wakiipinga hukumu ya kesi ya msngi namba 215/1997 na kukawa na kesi ya rufaa namba 129/2009 ili pia waendelee kukaa kwenye jesngo hilo.

TGNP iliiomba mahakama kufuta ombi la walalamikaji la kuendelea kuwa kwenye jengo ili shirika liweze kufanya shughuli zake, kesi ambayo ilisikilizwa na majaji watatu waheshimiwa jaji Msasali, jaji Msofe, na jaji Rutakanga Julai 22,2011.

Tarehe 23. 08.2011, TGNP iliamua kwa mujibu wa sheria kuwatoa kwa nguvu wapangaji hao ambao kwa muda wote wa zaidi ya miaka 10 wamekuwa wakifanya shughuli zao kwenye jengo la TGNP bila kulipa kodi wala ruhusa yao, lakini siku chache baadaye walirudi. Pamoja na ushindi walioupta TGNP bado waliendelea kuheshimu maamuzi ya mahakama kutokana na shauri walilolipeleka mahakamani.

Mwaka 2012 walalamikaji walienda tena Mahakama Kuu wakiomba kurekebisha majina ya watu waliosomewa hukumu kuwa  watu wengine walio hukumiwa hawakuwa sehemu ya kesi hii!!  TGNP tuliona kuwa hii ni  mbinu tuu ya kuchelewesha  kesi ambayo imekuwa ikitumika  kwa miaka mingi. Jaji Mwaikugile aliikubali hiyo barua akitaka wakaandike vizuri zaidi ili hoja yao isikilizwe. Kesi hii imepangiwa kusikilizwa tena hapo tarehe 26 Februari 2013, lakini hadi tarehe 08.03.2013 hawakuwa wamewasilisha na leo tarehe 13.03.2013 jaji ametupilia mbali ombi lao.
Kesi hii imekuwa ni changamoto kwa TGNP, huu ni mwaka wa 16 tangu shirika linunue jengo hili.
Sote kwa pamoja tunaamini katika haki na na rasilimali lazima zirudi kwa wananachi!
Imetolewa na

Imetolewa na:
Usu Mallya
Mkurugenzi Mtendaji TGNP

Wednesday, March 13, 2013

BREAKING NEWS: MOSHI MWEUPE WAFUKA VATICAN, PAPA MPYA NI KUTOKA AGENTINA CARDINAL JORGE BARGOGLIO ATAITWA PAPA FRANCIS

Hatimaye hivi punde moshi mweupe umefuka, kengele zimelia kuashiria Kiongozi mpya wa 266 wa Kanisa Katoliki duniani amekwisha chaguliwa (Papa kapatikana) kilicho bakia kwa sasa ndani ya jumba hilo Papa huyo anaulizwa maswali kama yuko radhi kutumikia nafasi hiyo ndipo atatolewa nje akiwa na jina jingine nao watu waliofurika nje ya jumba hilo la himaya ya papa wapate kumuona.... Nini hatma ya shughuli nzima? Basi fuatilia video hii hapa chini kwa kilichotokea.

MWANZA NA ZAIDI UIJUAVYO.

Kutoka angani eneo la mashamba ya Ilemela karibu na Air Port Mwanza.

Nyuma ya Capripoint.

Jicho la kamera likielekezwa  Mwanza North. 

Uvuvi ukiendelea ziwani Victoria.

Miamba ya maji.

Ni chombo cha usafiri (Buganda) ambacho hii leo kimegeuzwa kuwa sehemu ya chumba cha hoteli Tilapia iliyoko Capripoint wilayani Nyamagana jijini Mwanza.
PICHA ZOTE NA Moiz Husein.

BADO MOSHI MWEUSI VATICAN, PAPA MPYA HAJAPATIKANA.

Moshi mweusi umetokea kwenye dari la hekalu ya Sistine mjini Roma, kumaanisha kuwa makadinali walioko ndani ya hekalu wameshindwa kuafikiana juu ya Papa mpya anayetarajiwa kuchaguliwa.
Moshi mweupe utaashiria kupatikana kiongozi mpya wa kanisa Katoliki la Roma.
Makadinali hao wanatarajiwa kupiga kura mara nne kwa siku hadi pale thuluthi mbili ya makadinali wote watakapoafikiana juu ya Papa mpya.
Walipiga kura yao ya kwanza ambayo haikuleta maafikiano hapo usiku wa Jumanne. 

MWANADADA HELEN JOSEPH AKWEA KILELE CHA UBINGWA WA IBF


Helen Joseph, bondia mwanadada ambaye anaishi katika jiji la Accra, nchini Ghana akipigana ngumi yuko mboni kupanda kilele cha mafanikio katika maisha yake ya ngumi. Ni wakati ambao Helen Joseph anayetoka katika nchi ya Nigeria aliokuwa anaungojea katika maisha yake ya ngumi.
Helen Joseph akipozi kama bondia.
Mwaka jana alikutana na bondia Dahianna Santana katika jiji la San Domingo, nchini Dominican Republic kugombea ubingwa wa dunia wa IBF katika uzito wa Unyonya (Fearherweight). Taabu na kashikashi zote alizozipata wakati wa patashika ile ya mwaka jana zimekuwa fundisho tosha kwa Helen wakati anapojiandaa kukutana na Marianna Gulyas kutoka nchini Hungary kugombea ubingwa wa IBF wa mabara katika uzito wa unyoya.
Mpambano huo, unaoandaliwa na kampuni maarufu ya kukuza ngumi ya GoldenMike Boxing Promotion Syndicate ya nchini Ghana unategemea kuwa wa patashika kweli kutokana na mabondia wote wawili kuwa na ujuzi tele ulingoni. Wawili hawa watakutana tareeh 30 March katika uwanja wa michezo wa Accra na mpambanohuu utarushwa moja kwa moja na luninga ya Super Sports.
Ni mapromota wachache na mameneja wachache  ambao wanaweza kuwekeza kiasi kikubwa hivyo cha pesa katika mchezo wa ngumi namna ambapo kampuni ya GoldenMike Boxing Promotions Syndicate ya nchini Ghana imewekeza katika kuinua kipaji cha mwana dada Helen Joseph.
Kwa upande wake Helen ambaye ni nadhifu, mtanashati na mwenye nidhamu ya hali ya juu, mchezo wa ngumi ndio unaomlisha katika maisha yake na atatumia uwezo wake wote kuhakikisha kuwa taji hli kubwa la ngumi linabaki barani Afrika na kulitumia kama ngazi ya kukutana tena na Dahianna Santana katika ubingwa wa dunia! 

Tuesday, March 12, 2013

AIRTEL YAMZAWADIA MKAZI WA RUFIJI MILLIONI 15 KUPITIA PROMOSHENI YA AMKA MILLIONEA

Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (kulia) akimkabithi mshindi wa mwenzi January wa promosheni ya Amka millionea  bi Agnes Hassan Chakame mfano wa hundi ya shilingi million 15 baada ya kuibuka mshindi wa promosheni ya Amka millionea na Airtel na kujishindia kitita cha shilingi million 15. Agnes ni Mkulima na mkazi wa Rufiji mkoa wa pwani. Akishuhudia ni Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde


Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde akimkabithi mshindi wa mwenzi January wa promosheni ya Amka millionea bi Agnes Hassan Chakame mfano wa hundi ya shilingi million 15 mara baada kuamka mshindi wa promosheni ya Amka millionea na Airtel na kujishindia kitita cha shilingi million 15. Agnes ni Mkulima na mkazi wa Rufiji mkoa wa pwani. Promosheni ya Amka millionea bado inaendelea ili kujiunga andika neno SHINDA AU MILLIONEA kwenda namba 15595.

Mshindi wa mwenzi January wa promosheni ya Amka millionea bi Agnes Hassan Chakame akionyesha  mfano wa hundi ya shilingi million 15 mara baada kuamka mshindi wa promosheni ya Amka millionea na Airtel na kujishindia kitita cha shilingi million 15. Agnes ni Mkulima na mkazi wa Rufiji mkoa wa pwani.

MWIMBAJI LEVO ZA KIMATAIFA GOODLUCK GOZBERT ATHIBITISHA KUWEPO NDANI YA PASAKA GOSPEL FESTIVAL 31/03/2013 MWANZA.

Mwanamuziki wa muziki wa injili ambaye pia ni produza toka K Records ya jijini Mwanza, Goodluck Gozbert  (pichani) tayari amethibitisha kushiriki katika kusanyiko la Pasaka Gospel Festival litakalofanyika ndani ya uwanja wa CCM Kirumba tarehe 31/03/2013 ambapo humo ndani atakutana na wakali wengine kama Enock Jonas anayetamba na wimbo 'Zunguka' , Neema Mwaipopo 'Raha jipe mwenyewe' na wengine wengi waliothibitisha .

Sikiliza songi lake jipya hapa chini. 
 BIOGRAPHY
Goodluk Gozbert ukipenda waweza tumia jina lake la jukwaani Gozbert, ni msanii wa muziki wa injili nchini Tanzania toka Rock City (Mwanza).

Alizaliwa mnamo mwaka 1991 na kuanza kuonyesha kipaji chake mapema tu mwaka 2005 akitumikia kwaya ya Tumaini ya kanisa la KKKT Imani Mwanza.

Haikumchukuwa muda kwenda solo kwani mnamo mwaka 2008 akiwa na miaka 16 vilevile bado yu mwanakwaya wa Tumaini alifanikiwa kuachilia single zake za awali na hatimaye album iliyokwenda kwa jina NIMELIPIWA DENI, akimshirikisha Michael Malagila,  akiirekodi ndani ya studio za Ujumbe Records Mwanza, chini ya maproduza Selemani Muyomba na Charles Sokoro.

Akikulia kwenye viunga vya kitongoji cha Ghana Kirumba jijini Mwanza Goodluck ni mtoto pekee wa Bw. Gozbert Rweyemamu na Bi. Janeth Gozbert, baba yake alifariki dunia mwaka 1992 wakati Goodluck akiwa mdogo (umri wa mwaka mmoja tu) hivyo mama yake alimlea kwa msaada wa Good Summaritans pamoja na marafiki wa mama yake.
THE PRESENT AND FUTURE
In 2012 Goodluck began recording his Second album, titled NIMEUONAHe said “I’ve Decided to call it So not Just Because It is The Only Best Song In My Album But  Every Single Track In my Album got Power To carry The Tittle of an Album, Its Better for the audience to choose what they like,But This Seems To Be My Favourite On May 22, 2012, Gozbert announced via Facebook that the first single Wa MOYO would be released Very Soon....!!!! The song written by Himself


Interested in Swimming, and Drawing, Goodluck kept his musical aspirations to himself. As he grew up, Gozbert taught himself to play the piano, drums, guitar, and trumpet at K.K.K.T-Imani Church Under Tumaini Choir.

MSAADA WAKO UNAHITAJIKA ILIKUWEZA KUOKOA UHAI WA MTOTO SIMON MLOPE


Hivi ndivyo hali ya mtoto Simon Mlope ilivo kwa sasa.

Angalia Video ya  mtoto Simoni Mlope akiwa na Mama yake. 

Mtoto Simon Mlope akiwa na mama yake ambaye anaitwa Amina Ally.

Simon Mlope akijaribu kutembea kwa shida
Taarifa na Demasho news.
 Mtoto simon Mlope mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa eneo la mahenge katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma amelazimika kukatisha masomo yake ya shule ya msingi akiwa darasa kwanza  kutokana na mototo huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo .
Awali tulitoa habari za mtoto huyu akiomba msaada lakini hadi sasa bado hajapata msaada wowote ule wa kuweza kuokoa maisha yake. Nahivi sasa hali ya mtoto huyu inazidi kuwa mbaya kiafya .

 Mtoto simon Mlope alikubwa na ugonjwa  moyo  tangu mwaka 2001 mara baada ya kuzaliwa na kugundulika kuwa  moyo wake una tundu hali ambayo inasababisha  kuvuta pumzi kwa shida.
Mama wa mototo  simon mlope anayeitwa AMINA ALLY  anawaomba watanzania kumsaidia mtoto  wake fedha za matibabu Baada ya kuambiwa na madaktari kuwa simon anatakiwa kwenda nchini  india kutibiwa,baada ya kupata rufaa kutoka muhimbili mwaka 2006  huku familia yake ikiwa haina uwezo kabisa.

Majirani wa familia ya simon nao wanasema kuwa mototo simon anahitaji msaada wa haraka kwa kuwa hali yake sio nzuri na kuwaomba watanzania wamsaidie.
Kinachosikitisha zaidi baba wa mtoto huyo  anayejulikana kwa jina la SIMON MLOPE  ameondoka nyumbani hapo tangu mwaka 2011 na hajulikani aliko kwa sasa, ingawa mwanzoni alisema yuko nchini Msumbiji.
Kwa anayeguswa na tatizo hili na anataka kumsaidia  SIMONI MLOPE  atumie simu namba  0752732290

ATHARI ZA DIGITALI WAMILIKI TV WATISHIA KUZIMA MITAMBO


Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (Moat), Reginald Mengi .


Dar es Salaam. Wamiliki wa vituo vya utangazaji vya televisheni nchini, wamesema watasitisha kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokana na kushindwa kumudu gharama za uendeshaji.
Hatua hiyo inatokana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuzima mitambo ya analojia na kuhamia dijitali Desemba 31, mwaka jana kitendo walichodai kimepunguza mapato yanayotokana na matangazo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (Moat), Reginald Mengi alisema hakuna haja ya kurusha matangazo kwa hasara.
Mengi alisema kutokana na kuanza kwa mfumo wa dijitali, watangazaji wamesitisha kutoa matangazo kwa sababu wananchi wengi hawana ving’amuzi.
“Kama mamlaka itashindwa kurudisha ule mfumo wa analojia kuwa sambamba na dijitali hadi wananchi watakapokuwa na ving’amuzi, tutazima televisheni zetu ndani ya mwezi mmoja ujao,” alisema Mengi.
“Ibara ya 18 ya Katiba imekiukwa kutokana na wananchi kunyimwa fursa ya kupata habari, hivyo hali hii hatutaki iendelee,” alisema Mengi.
Mengi ambaye pia ni mmiliki wa vituo vya televisheni vya ITV, EATV na Capital TV, alisema licha ya nchi za Afrika, Tanzania imekuwa ya kwanza kuzima mitambo ilhali wananchi hawakuwezeshwa kumudu gharama za ving’amuzi.
“Nchi ambazo zimeendelea kwa kila kitu kama Uingereza, Marekani, Japan na kwingineko kuzima mitambo ya analojia walitumia zaidi ya miaka minane kwa nini sisi tumewahi hivi wakati hatujajipanga?” alihoji Mengi.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Sahara Media Group na mmiliki wa Kituo cha Star Tv, Samwel Nyalla alisema hivi sasa wanaendesha biashara hiyo kwa hasara.
Nyalla alisema hadi mwaka 2015, hali itakuwa mbaya kutokana na kukosa ving’amuzi.
Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA, Habby Gunze alisema wao hawakualikwa katika mkutano huo hivyo hawajui chochote. Gunze alimtaka mwandishi kwenda ofisini leo.

“Sisi hatujui chochote na kama unataka maelezo mengine njoo kesho (leo) ofisini kwetu uonane na Mkurugenzi Mkuu (Profesa John Nkoma), ili tuzungumze kwa ‘fact’ (kwa ushahidi) kipi kinachoendelea,” alisema Gunze.

Nukuu
“Kama mamlaka itashindwa kurudisha ule mfumo wa analojia kuwa sambamba na dijitali hadi pale wananchi watakapokuwa na ving’amuzi tutazima televisheni zetu ndani ya mwezi mmoja ujao labda TBC ndiyo itakayobaki”.
CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI

Monday, March 11, 2013

PPF YAONESHA NJIA YA KUSAIDIA KIKUNDI CHA HABARI Group

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki amewataka waandishi wa Habari wa Kike kutumia kalamu zao katika kuandika mambo yanayohamasisha amani na utulivu nchini.

Pia aliwataka kutumia kalamu zao katika kuandika na kuibua vitendo vya unyanyasaji na vya kikatili wanavyofanyiwa wanawake nchini.


Hayo aliyasema hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Lamada , wakati wa uzinduzi wa kikundi cha Habari Group kinachojumuisha waandishi mbalimbali wa habari hapa nchini.

Alisema ni vyema wakatumia fursa zao katika kufichua viashiria mbalimbali vya fujo kwa kuwa endapo itatokea uvunjifu wa amani wanaoathirika zaidi ni wanawake na watoto.

Kikundi cha habari kinajihusisha na ununuaji wa hisa, kukopeshana na kufanya miradi mbalimbali ya kikundi na mmoja mmoja hivyo aliwataka wanakikundi kujibidiisha zaidi na kuongeza wanachama wake.

“Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ni moja ya maadhimio 12 ya ulingo wa Belgin hivyo mnachofanya hapa ni katika kujikwamua wenyewe kiuchumi na kama mnavyofahamu wanawake wanamajukumu mengi katika familia na pia kutingwa na mambo mengi katika tasnia yenu lakini mmethubutu kufanya hivyo hivyo endeleeni,”alisema Kagasheki

Pia alitoa wito kwa wanawake kuhakikisha kuwa majukumu waliyonayo yasiwe kikwazo kwao kushiriki katika kukuza uchumi.

Alisema kinachotakiwa ni kuondoa fikra kuwa haiwezekani na kuhakikisha wanapiga vita mambo yanayomgandamiza mwanamke kwa kuondoa fikra kwamba haiwezekani kujikwamua kiuchumi.

Naye mlezi wa kikundi hiko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki alisema atakuwa bega kwa bega na wanakikundi hiko katika kuhakikisha kuwa kinasonga mbele.

“Nimefurahishwa sana na wazo la wanahabari hawa na nina ahidi nitakuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa kikundi kinakua zaidi na kuwatafutia fursa mbalimbali za kukiendeleza pia,”alisema Kairuki.

Naye Meneja Uhusiano wa PPF Lulu Mengele alisema wamekuwa katika mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwenye  saccos nchini kwa wanachama wao sehemu za kazi.

Alisema tayari wametoa mikopo kwa wanachama wake kwenye maeneo ya kazi  41 yenye thamani sh bil 48.7 lengo likiwa ni kumsaidia mwanachama akiwa kwenye ajira.

Aliendelea kueleza  kuwa PPF inachukua jukumu la kusomesha watoto wa wanachama ambao wazazi wao wamefariki kuanzia chekechea hadi kidato cha nne ambapo kwa sasa tayari wanasomesha 1333 katika shule mbalimbali.

Alisema PPF inatoa mafao saba ambapo aliyataja kuwa ni pamoja na uzee,ugonjwa,kiinua mgongo,kifo ,elimu,kujitoa, sambamba na kuandikisha wanachama kutoka kwenye sekta mbalimbali na kupata taarifa zaidi kupitia simu ya mkononi.

Naye mratibu wa kikundi cha habari group Rabia Bakari akisoma risala mbele ya mgeni rasmi alisema kikundi kinahitaji zaidi ya milioni 10 ili kila mmoja
aweze kupata mkopo kwa wakati bila kupeana kwa zamu ili kuharakisha shughuli za maendeleo.

”Kwa sasa katika akaunti yetu tumefanikiwa kuwa na milioni mbili na nusu tu, hivyo tunahitaji zaidi ya milioni 23 ili kufanikisha malengo tuliyojiwekea,”alisema Rabia.
 

Mara baada ya mgeni rasmi kuzindua kikundi kulifanyika harambee ambapo zilichangwa zaidi ya sh mil 6 ambapo mgeni rasmi alitoa mil 2 na mama mlezi wa kikundi alitoa 1.5 mbunge wa Busega Dk.Titus Kamani alitoa laki 2, Jumuia ya kukuza uchumi Ilala laki sita ,TAMADA laki 2 pamoja na wadau wengine.

AMSHA AMSHA YA KUELEKEA PASAKA ILIVYOKUWA JANA KATIKA ENEO LA BUHONGWA

Ni Amshaamsha ya pasaka, na hii  ni safari ya kuziandaa kwaya mbalimbali za jijini Mwanza kuelekea sikuu ya Pasaka ambapo COSU Entertainment wanataraji kuzindua studio za kurekodi muziki sambamba na video hapa ilikuwa katika eneo la viwanja vya michezo Buhongwa nje kidogo ya jiji la Mwanza.


Kwaya zinajinoa vilivyo kwa style kalikali viwanjani hapa sambamba na kuongeza ubunifu.


Shughuli imenoga kwa kwaya kuvalia sare zao maridadi tena za kupendeza, tukio limekuwa kama mashindano vile ya kwaya, kumbe laa hasha... ni maandalizi tu! kuelekea tarehe 31/03/2013 sikukuu ya Pasaka ambapo Enock Jonas anayetamba na wimbo 'ZUNGUKA' sambamba na Neema Mwaipopo anayetamba na wimbo wa 'RAHA JIPE MWENYEWE'  na waimbaji wengine toka mikoa mbalimbali hapa nchini watashuka CCM kirumba kuwasha moto wa injili kwa njia ya uimbaji.


Nao watu hawakukubali kupitwa na Amsha amsha hii ya kuelekea tarehe 31/03/2013 sikukuu ya Pasaka.
Nyang'omango


Macho kwenye Amsha amsha ya Pasaka.


Vikundi mbalimbali na ustaarabu wao.


Waimbaji wa moja ya kwaya wenyeji hapa Buhongwa.


Sound 'cheki' 


Pozi.... 


Akinamama na watoto wao wakiyawajibisha macho.


Kwa uhuru na amani viwanjani hapa.


Hapo vipi?




Vijana wa Mungu kazini....


Muacheni Mungu aitwe Mungu haya ni maandalizi tu katika 'Amsha amsha ya Pasaka', shughuli kamili itakayokuwa na kishindo kikuu ni siku ya tarehe 31/03/2013 CCM Kirumba kwa kiingilio cha shilingi 2000/= tu!


Burudani imenoga.