ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 18, 2013

WATEJA WA MALIPO YA MWEZI (POSTPAID) AIRTEL SASA KULIPIA ANKRA ZAO KUPITIA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

Akizindua huduma ya Airtel money. Kulia ni Mkurugenzi wa kitengo cha  Airtel huduma kwa wateja adriana Lyamba akiongea na waandishi wa wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel Money leo. ambapo sasa inawawezesha wateja wake wa huduma ya malipo ya baadayekulipia bili zao za kila mwezi kupitia huduma ya Airtel money popote walipo. Kushoto ni afisa wa Airtel kitengo cha huduma ya malipo baadae Pauline Shoo akifuatilia uzinduzi huo leo.
Afisa malipo ya huduma kwa wateja wa malipo baadae Bi Pauline Shoo akielezea jinsi huduma hiyo inavyofanya kazi kupitia (Menu) au Orodha ya huduma ya Airtel Money. huduma hii inawawezesha wateja wa Airtel  wa malipo ya baadaye kulipia bili zao za kila mwezi kupitia huduma ya Airtel money popote walipo 
Kushoto ni Mkurugenzi wa huduma kwa wateja Adrina Lyamba na ofisa huduma kwa wateja wa malipo baadae bi Pauline Shoo wakiwa wameshikilia vipeperushi vya huduma mpya inayowawezesha wateja wake wa huduma ya malipo ya baadaye kulipia bili zao za kila mwezi kupitia huduma ya Airtel money popote walipo. Kushoto ni afisa wa Airtel kitengo cha huduma ya malipo baadae bi Pauline Shoo
Wateja wa malipo ya mwezi (POSTPAID)  Airtel sasa kulipia Ankra zao kupitia  huduma ya Airtel Money

Dar es Salaam 17, 2013 katika mwendelezo wa kutoa suluhisho na kuboresha huduma za kifedha,  Airtel Tanzania sasa inawawezesha wateja wake wa huduma ya malipo ya baadaye kulipia bill zao za kila mwezi kupitia huduma ya Airtel money.

Akiongea juu ya huduma hii mpya, Mkurugenzi wa kitengo cha huduma za wateja wa baadaye bi Adriana Lyamba alisema "Airtel Leo tunayo furaha kuwafahamisha wateja wetu wa malipo ya mwezi (postpaid) kuwa malipo ya ankra zao za simu za kila mwenzi yamerahisishwa zaidi kwa kupitia huduma ya Airtel money ambapo kwa sasa hakuna haja ya kwenda benki au kwenye ofisi za Airtel kulipia bill zao,  wateja wote wanaweza kufanya malipo kwa kupitia huduma ya Airtel money.

Tunao wateja wa mashirika ya binafsi , Umma, serikali, UN agencies, NGO na mashirika madogo madogo SME  kutoka katika mikoa mbalimbali nchini wanaotumia huduma zetu za  malipo ya mwisho wa mwenzi yaani huduma ya Postpaid

Tumeanzisha huduma ya kulipia bill kwa kupitia Airtel money  ili kuweza kukabili changamoto mbalimbali tulizokuwa nazo huku tukiongeza mapato katika ukusanyaji wa madeni na kuwaondelea wateja wetu usumbufu wa kutembea umbali mrefu kufanya malipo na kutoa rahisi katika huduma zetu.

Bi Adriana Lyamba alisema, Tunaamini huduma hii italeta ufanisi mkubwa katika huduma zetu na kuongeza wigo mpana wa malipo ya anka zao. Na nachukua fulsa hii kuwashukuru wateja wetu kwa kutumia huduma zetu mbalimbali katika kuendesha shughuli za kibiashara, kiuchumi na kijamii

Akiongea jinsi ya kulipia ankra za simu Afisa huduma za baada Bi Pauline Shoo  alisema Kupata huduma hii ni rahisi , piga *150*60#  na kuunganishwa na menu ya Airtel money, kisha bonyesha kulipia bill, andika neno la biashara postpaid - malipo ya mwenzi, ingiza kiasi , number ya account yako ya post paid kisha bonyeza ok na mojakwamoja utapa uthibitisho wa malipo yako.

huduma ya Airtel money yaani pesa mkononi ni huduma ya kifedha inayotolewa na Airtel ikiwa na lengo la kurahisisha malipo ya anka mbalimbali na kuwezesha upatikanaji wa pesa yaani  kutuma na kutoa fedha kuwa rahisi na uhakika mahali popote nchini

kwa sasa Airtel kupitia promosheni yake ya hakatwi mtu hapa inawawezesha wateja wake nchi nzima kutuma na kutoa pesa BURE bila makato yoyote .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.