ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 19, 2013

MAN U IKIAMBULIA SARE, ARSENAL HIYOO KILELENI.

Goli la pili la kichwa la Mesut Ozil. 
Ushindi wa Arsenal dhidi ya Norwich umeiwezesha kwendelea kuongoza ligi kuu ya premier ya England.
Mesut Ozil amefunga mabao 2 miongoni mwa 4-1 yaliyofungwa na Arsenal kwenye uwanja wao wa Emerates.
Goli la kwanza limefungwa na Jack Wilshere kwa ustadi mkubwa kunako dakika ya 17 ya mchezo.Mesut Ozil amepiga la pili kunako dakika ya 57 kabla ya Norwich kupata bao lao lililoingizwa na Jonathan Howson dakika 10 baadae.
Aaron Ramsey amepachika goli la 3 la Arsenal kwenye dakika ya 82 na Ozil kufunga kazi dakika 3 kabla ya kipenga cha mwisho kulia.
Kwa ushindi huo Arsenal inaendelea kuongoza msimamo wa ligi ikiwa na alama 19 baada ya mechi 8 zilizokwisha chezwa.inafwatiwa na Chelsea yenye alama 17 sawa na Liverpool,lakini wanatofautiana kwa magoli.
Mchezo baina ya Newcastle na Liverpool umemalizika kwa matokeo ya sare ya 2-2, The Magpies wakitangulia kulisalimia mara mbili lango la Liverpool lakini Steven Gerrard na Daniel Sturride walihakikisha kushea pointi za leo.
Wachezaji wa Southampton wakishangilia goli la kusawazisha dhidi ya Manchester United.
Jahazi la Manchester United limezidi kujaa maji baada ya kugawana pointI na Southampton ambao walirejesha goli kunako dakika za majeruhi mpira ukaisha kwa sare ya 1-1.
Wakati kocha Moyes wa Man U akiendelea kupata presha kwa timu yake kufanya vibaya Chelsea ambao waliikaribisha Cardiff darajani pale Stamford, wamenyakuwa ushindi wao wa tano kwa msimu huu kwa ushindi wa bao 4-1. Matokeo yanayo iweka timu hiyo nafasi ya pili nyuma ya washika bunduki.
In the other 3pm games, Everton beat Hull at Goodison Park, Swansea trashed Sunderland and Stoke vs West Brom finished goalless.
In the late kick-off Sergio Aguero struck twice as Manchester City picked up three vital points away at West Ham.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.