ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 26, 2013

KUNDI LA Cash Money, LATOA MSAAA KWA WAGOJWA HOSPITALI YA TEMEKE

Wana kikundi cha Cash Money wakiwa tayali kwa kutoa msaada katika hospitali ya Temeke

Mlezi wa Kikundi cha Cash Money ,Ratifa Masasi kulia akimkabibi muhuguzi wa wodi ya watoto bi, Nuswe Ambokile zawai mbalimbali walizoleta kwa ajili ya watoto waliolaza katika hospital ya Temeke

Baadhi ya wana kikundi cha Cash Money wakiwa katika picha ya pamoja na wahuguzi wa word ya watoto Hospitali ya temeke baada ya kukabidhi msaada





Na Mwandishi Wetu MSANII nguli wa muziki wa dansi aliyestaafu, Muhidini Gurumo, atapanda  jukwaani leo kutumbuiza na mkewe, sambamba na kupewa zawadi za heshima.
Gurumo atatoa  burudani hiyo ikiwa ni sehemu ya kuwaaga mashabiki, ambapo shughuli hiyo itaambatana na uzinduzi wa kundi la Cash Money, la Tandika mjini Dar es Salaam.
"Tumeandaa zawadi kwa mzee Gurumo kutokana na heshima kubwa aliyonayo katika tasnia ya muziki na kujenga maadili kwa taifa kutokana na nyimbo zake.
Hivyo zawadi zetu zitaenda sambamba na uzinduzi, ambapo tumepanga hivyo, ili lee mwenye chochote ampe mzee wetu,"Aliongeza Latifa Masasi mlezi wa kundi hilo.
Uzinduzi huo unafanyika kwenye ukumbi wa Equator Grill, Mtoni kwa Aziz Ali, Dar es Salaam na utapambwa na bendi mbalimbali za taarabu zikiwemo Coast na G Five.
Kundi la Cash Money ambalo lilianzishwa mwaka 2011, pia limetoa vitu mbalimbali kwa wodi ya watoto, na vituo vya watoto yatima jana, ikiwa ni sehemu ya uzinduzi huo


Mlezi wa kikundi cha Cash Money akimfaliji mama Samir Nassoro, Naomi Ramadhani walipokutana wakati kundi hilo likitoa msaada kwa wagojwa katika hod ya watoto

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Cash Money wakimfariji Bi Naomi Ramadhani

Msanii wa bendi ya Msondo ngoma Saddy Ally katikati akisalimiana na wanakikundi cha cash money walipokutana katika hospitali ya Temeke wakitokea kutoa msaada

Wana kikundi wa chass money kushoto Amina Uredi 'Mmanyema ' na Zulfa Kasongo

Mlezi wa kikundi cha cash money bi, Ratifa Masasa akimfariji mtoto Salimu Ally wakati walipokwenda kutoa msaada katika hospitali ya temeke dar es salaam mwingine ni mama mtoto Tabu Salumu mkadhi wa Tandika

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.